Na Walter Mguluchuma -Mpanda
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Fransis Agustino Nilanga amekamatwa akiwa na Jeneza lililokuwa ndani na mwili wa marehemu mtoto wake alioufukua makaburini kwa lengo la kwenda nao nyumbani ili kuuombea uweze kufufuka .
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Fransis Agustino Nilanga amekamatwa akiwa na Jeneza lililokuwa ndani na mwili wa marehemu mtoto wake alioufukua makaburini kwa lengo la kwenda nao nyumbani ili kuumbea uweze kufufuka .
Mwenyekiti wa Mtaa wa Kapalangao Fransis Feruzi amesema tukio hilo la kusikitisha na
lilozua tahaluki kwa wananchi wa Mtaa huo na Manispaa
ya Mpanda limetokea usiku wa kuamkiajuzi katika makaburi ya Kazima Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.
Amemtaja
marehemu huyo aliyefukuliwa kwenye kaburi
la na baba yake mzazi kuwa ni Imelda
Nilanga aliyefariki mwaka jana mwezi wa saba akiwa na
umri wa mwaka mmoja na nusu .
Amebainisha kuwa siku
hiyo ya tukio majira ya saa tisa na nusu usiku alipigiwa simu wakati
akiwa amelala nyumbani kwake alipigiwa simu na jeshi la
Polisi iliyokuwa inamtaka kueleza kama anamjua mtu
anaejulikana kwa jina la Fransis Agustino Nilaga na baada ya kutajiwa jina hilo aliwajibu kuwa anamfahamu .
Baada ya kuwa amekubali
kuwa anamfahamu alitaalifiwa kuwa amepatikana akiwa na
jeneza ambalo ndani yake Kulikuwa na mwili wa
marehemu mwanae na anashikiliwa katika kituo cha Polisi cha
Wilaya ya Mpanda baada ya kuwa wamepewa taarifa na
mwendesha bajaji ndipo walipoweza kumkamata.
Kufatia taalifa hiyo
alilazimika kwenda nyumbani kwa baba yake na mtuhumiwa huyo
kwa kuwa walikuwa wanaishi nae jirani iliaweze kupata ukweli kama aliyekamatwa
ndie mtoto wake basi kwa Mzee nilanga ni jirani
alienda kumfunguza na baada ya kumfunguza alimuuliza
mwanao Fransis yupo ndani akasema ngoja
amwangalie chumbani kwake na alimwangalia hamkuweza kumkuta chumbani kwake .
Feruzi amesema ndipo
alipomweleza mzazi wake kuwa mwanao yupo kituo cha polisi
amekamatwa akiwa na jeneza lenye mwili
wa marehemu aliyemfukua makaburini .
Amebainisha baada ya kuwa
wamefika kwenye kituo cha polisi kweli walikuta sanduku lilikuwa na mwili
wa marehemu na ndipo walipo pewa maelezo
kuwa Fransis Nilanga amekutwa na jeneza likiwa
na mwili wa marehemu katika maeneo ya makaburi ya Kazima baada ya
kumwomba mwendesha bajaji amsaidie kubeba sanduku hilo
kwenda nalo nyumbani kwake .
Kufatia
kupatiwa maelezo kituoni hapo yeye pamoja
na mzee Nilanga waliomba wapewe nafasi
ya kuweza kumwona Fransis ili waweze kumtambua kama ni yeye na
waliweza kumtambua kweli ni yeye na katika mazungumzo yake
alisema aliamua kufanya hivyo kutokana na huzuni ya muda
mrefu ya kumkosa mwanae aliyekuwa wa kwanza .
Alitumani
kwamba katika maombi ambayo angemfanyia mwanae licha ya
kuwa amekufa toka mwaka jana angweza kufufuka
ndipo siku hiyo uzuni ilipokuwa imemshika
usiku alichukua uamuzi wa kutoka na jembe na kwenda
makaburini kufukua mwili wa marehemu mtoto wake alikwenda
kuufanyia maombi kwa kutumia Bibilia Takatifu
Mwenyekiti huyo
wa Mtaa ameeleza kuwa kwa dalili za historia yake
inaonyesha alikuwa na shida ya afya ya akiri ndio inawezekana ilimfanya
achukuwe maamuzi hayo yeye kama mwenyekiti wa
mtaa analithibitisha tukio hilo limetokea na mwili wa marehemu huyo
walikabidhiwa ndugu zake na waliweza kuuzika kwenye kaburi
lilile alikuwa amezikwa mwanzo .
Nae mkazi wa
Mtaa huu Mona Joseph amesema kuwa tukio hilo kwake ni la kwanza toka
alopoanza kuishi kwenye mtaa huo alikuwa haja wahi kuona tukio kama hilo