TAKUKURU KATAVI YABAINI UWEPO WA KASORO KWENYE MIRADI

 

Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Katavi,Faustine Maijo akitoa taarifa ya taasisi hiyo ya utekelezaji wa utendaji kazi ya kipindi cha mienzi mitatu iliyopita.

Na Walter Mguluchuma,Katavi

TAKUKURU Mkoa wa Katavi kwa kipindi cha miezi mitatu imefatilia  utekelezaji  wa  miradi  11 ya maendeleo  yenye thamani ya zaidi ya   shilingi  Bilioni 9.5 katika  sekta  mbalimbali  zikiwemo na  sekta ya  Elimu  na afya  na kubaini mapungufu  mbalimbali yakiwemo  kutofuata  taratibu za   manunuzi.

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi Faustine Maijo akitoa taarifa mbele ya waandishi wa Habari

TAKUKURU  Mkoa wa Katavi kwa kipindi cha miezi mitatu imefatilia  utekelezaji  wa  miradi  11 ya maendeleo  yenye thamani ya zaidi ya   shilingi  Bilioni 9.5 katika  sekta  mbalimbali  zikiwemo na  sekta ya  Elimu  na afya  na kubaini mapungufu  mbalimbali yakiwemo  kutofuata  taratibu za   manunuzi.

Wameweza kupokea malalamiko   65 ambapo  taarifa zinazohusu rushwa zilikuwa  35 na  zisizohusu rushwa  30 huku  serikali za mitaa  ikiwa  ilaongoza kwa  kalalamikiwa na wananchi waliopelela  malalamiko  yao.

Hayo yamebainishwa na  Mkuu wa Takukuru wa  Mkoa wa Katavi, Faustine  Maijo wakati akitowa taarifa ya utendaji kazi wa Taasisi hiyo ya  Kuzuia na Kumbana na  Rushwa(TAKUKURU) Mkoa wa Katavi ya utendaji kazi wa kipindi cha miezi mitatu ya Otoba 2023  hadi  Desemba 2024 kwa wandishi wa Habari.

Maijo  ameeleza  kuwa kwa kuzingatia  kuwa  serikali imepeleka  miradi  mingi ya  maendeleo  kwa wananchi  na kupeleka  fedha  nyingi  kwa ajili ya utelelezaji wa miradi  mbambali ya  Maendeleo kwenye  maeneombalimbali ya  wananchi.

Baadhi ya waandishi wa Habari mkoa wa Katavi wakiwa katika mkutano na mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi 

Kwa kutambua hilo TAKUKURU Mkoa  wa  Katavi  katika  kipindi hicho  imefatilia  jumla ya  miradi 11  inayotekelezwa  katika Mkoa huu  yenye  thamani ya   Tshs 9,579,630,108 kwenye sekta za  elimu , afya na  ufundi  sitadi (VETA )

Katika  kufatilia miradi hiyo inayoendelea kutekelezwa  TAKUKURU  wamekuwa wakiifatilia  kwa karibu sana  na  katika  ufatiliaji wa  miradi hiyo 11  wameweza kubaini  baadhi ya  mapungufu kwenye miradi hiyo  ikiwemo  ucheleweshaji  wa  miradi  na pia kutofuatwa kwa  taratibu za  manunuzi.

Kuhusu malalamiko  Maijo ameeleza kuwa  wameendelea kupokea  malalamiko  mbalimbali  kutoka kwa wananchi  yanayohuasiana na Rushwa ambapo wameweza kupokea  malalamiko 65 kati ya hayo 35 yalihusu Rushwa   na 30 hayakuhusu Rushwa  na  malalamiko hayo yalihusu  sekta za  Serikali za Mitaa 23,  Kilimo 2,Binafsi  2 TFS  1, Maji 1, Ardhi  1,  Makazi  ya Wakimbizi 2, Polisi  1  na  Afya 1.

Amefafanua  kuwa  taarifa   zinazohusu Rushwa  zimeshughulikiwa  kwa  mujibu  wa  sheria ya  Kuzuia na  Kupambana na  Rushwa  Namba 11 ya mwaka 2007 hali  ambayo  imepelekea  Takukuru  Mkoa wa Katavi  kuanzisha  uchunguzi wa  majalada  35 ya uchunguzi wa awali  kati   ya  hayo  majalada  matatu yamekamilika  na  katika kipindi hicho  mashauri 2 yamefunguliwa  Mahakamani  na kufanya  kesi zinazoendelea kuwa 9.

Mkuu  huyo wa Takukuru  Mkoa wa Katavi  amesema  katika  kipindi cha  Januari   hadi  Machi 2024 wameimarisha  juhudi za  Kuzuia  Rushwa  kwa kuendelea  kufatilia   utekelezaji  wa  miradi  ya  maendeleo.

Kwa   kuhamasisha  na kutoa  elimu  ya ushiriki   ya ushiriki  wa wananchi  katika  vita  dhidi ya  Rushwa  kupitia  vyanzo mbalimbali  za  uelimishaji  ikiwemo vipindi vya  radio na  katika mikusanyiko mbalimbali  kwa  kutumia   mwongozo wa TAKUKURU  RAFIKI.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages