JESHI LA POLISI KATAVI LAPONGEZWA KWA KUDHIBITI UHALIFU WA DAMU CHAFU.

  





Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akihutubia kwenye tamasha la Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Katavi.

Na Walter Mguluchuma,Katavi

MKUU wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko  amepongeza  jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kwa  kuweza kufanikiwa  kufanya kazi nzuri ya kuweza  kudhibiti  kikundi cha  uhalifu kilichokuwa  kinatishia amani kwa wananchi hasa wa maeneo ya Manispaa ya Mpanda.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akifanya vipimo vya afya katika moja ya banda kwenye kwenye tamasha maalumu.

Pongezi  hizo amezitolewa wakati  akiwahutubia  askari wa Jeshi la  Polisi pamoja na wananchi  wakati wa  sherehe ya Polisi  Famiy  day  iliandaliwa  na  jeshi hilo kwa kushirikiana na  Klabu ya Wandishi wa  Habari na kufanyika katika  viwanja vya michezo vya polisi.

Amebainisha kuwa vitendo vya  uhalifu  vilivyokuwa vinafanywa  na vikundi  vinavyoitwa damu  chafu  katika  Mkoa wa Katavi na  hasa  katika  eneo la  mji wa Mpanda  kwa kiasi kikubwa kwa  zaidi ya asilimia  ya  asilimia 99.5 jeshi la Polisi  limeweza kufanikiwa  kudhibiti  uhalifu huo.

Mrindoko   amesema wameshuhudia   katika  kipindi cha   mwezi Desemba  na Januari  wameona hali ya utulivu  imeendelea kuimalika  na matukio  yale  ya  damu   mchafu yamepungua  kwa  kiasi cha asilimia hizo.

Amewataka kuhakikisha  hicho kiasi kidogo kilicho baki  kinakwisha kabisa  ndani ya  Mkoa wa Katavi  na uhalifu  mwingine  wowote  ambao unaleta bugudha kwa jamii  ambapo  unaleta  madhara  kwa watu  wakati mwingine unatowa  uhai wa  baadhi ya watu.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi,ACP Kaster Ngonyani akifanya vipimo vya afya katika moja ya banda.
Baadhi ya asikari wa Jeshi la Polisi wakifanya onesho maalumu wakati wa tamasha maalumu.

Hivyo  amewahakikishia  Wananchi wa Mkoa wa Katavi kuwa jeshi la Polisi  Mkoa wa Katavi   lipo  kwa utayari kwa kuhakikisha  hali ya usalama inaendela kuimarika zaidi  kupatikana  na amewaomba wananchi kuendelea  kutowa ushirikiano  kwa jeshi hilo kwa kuwajulisha  mapema  matukio ya uhalifu kabla  hayaja tokea.

Mrindoka  ameviagiza vyombo vyote vya usalama katika Mkoa huu kuhakikisha  wanaongeza  jitihada  za  kudumusha  hali ya  usalama   unaendelea kuwa  imara  zaidi na  zaidi ili wananchi waendelee kuishi kwa amani  na kwa utulivu.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Kaster  Ngonyani  amesema  siku  hiyo  ya  polisi ‘ Family Day’ wameamua kuifanya  kwa pamoja na wandishi wa habari ili  kuendelea kuwa  na  ushirikiano zaidi  baina yao na  jeshi la polisi   katika kitimiza  kazi  zao za pambe hizo mbili..

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages