MRADI WA THAMINI UHAI WAPUNGUZA VIFO VYA AKINA MAMA NA WATOTO KATAVI.



Mganga Mkuu wa Mkoa, Dk Jonatham Mdemu.


Na Walter Mguluchuma,Katavi

Mradi wa THAMINI UHAI  unaotekelezwa katika Mikoa mitatu nchini  umesaidia sana  katika Mkoa  wa Katavi  kupunguza  vifo vitokanavyo na uzazi  mradi huu umekuwa sehemu ya kupunguza vifo hivyo kwa kuweza kuwaelimisha  watu    kuwa na wasindikizaji kwa   wajawzito  kwa kuwapeleka kwenye vituo vya kutolea huduma ya mama na mtoto   na siku ya kujifungua  kijifungulia kwenye vituo badala  kujifungulia nyumbani .

Afisa Mradi wa Thamini Uhai  Dr  Calist  Nzabuhakwa

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dk Jonathan  Mdemu amebainisha kuwa  kwa kipindi cha  miaka  mitano iliyopita vifo vya akina  mama vitokanavyo na uzazi vimeendelea kupungua  ambapo kwa mwaka 2018 vifo vya watoto wachanga vilikuwa 631 hadi kufikia  Desemba  2023 vifo vya watoto wachanga  vimetoka kwa  idadi hiyo hadi kufikia 270 ambavyo vimepungua kwa zaidi ya nusu .

Kwa upande wa vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi  vimeendelea kupungua  kwa miaka mitatu ya nyuma kulikuwa na vifo 50 mwaka 2022 kulikuwa na vifo 36 na  mwaka 2023 kulikuwa na vifo  27 vilivyotokea katika Halmashauri zote tano za Mkoa wa Katavi .

Ameeleza  mradi wa  THAMINI UHAI  umekuwa ni sehemu ya kupunguza vifo hivyo  kwa sababu  wakina mama  wameacha kujifungulia nyumbani  idadi yao  inakwenda chini kutoka na elimu ambayo imekuwa  ikitolewa na  THAMINI UHAI .

Dk Mdemu amefafanua kuwa  wajawazito wanapokuwa wamekwenda   kwenye vituo vya kutolea huduma wakiwa na wasindikizaji  wao wanawasaidia wanakaa nao wanakuwa  wanaona maendeleo ya hali zao  wanazokuwa nazo kabla ya kujifungua  ambapo hapo awali  walikuwa wakiwazuia wajifungulie nyumbani  kwa sasa wanawasindikiza kwenda hospitali.

Amesema kwenye Mkoa huo mradi wa THAMINI UHAI  umesaidia akina mama wanaojifungulia njiani  kupungua  ambapo kwa sasa  kuna zaidi ya asilimia 80 ya akinamama wanaojifungulia katika vituo vya Afya na kuhudumiwana wataalamu wa afya.

Mmoja wa wakazi wa Kijiji cha Mtambo Makazi ya Katumba  ambae ni mnufaika  wa mradi wa  THAMINI UHAI aliweza  kusindikizwa na msindikizwaji  hadi kwenye kituo cha Afya cha Katumba na kujifungua salama  licha ya  mwenza wake siku hiyo kutokuwepo nyumbani  akiwa  na mtoto wake aliyejifungua miezi kadhaa iliyopita

‘Mwanzoni  kulikuwa hakuna usiri  sasa hivi tuna vituo   vinane  vimewekwa  ambavyo  vimesaidia kuwepo kwa faragha wakati wa kujifungua  na kupelekea baadhi ya wajawazito kutoka wilaya ya Tanganyika kwenda kujifungua katika kituo cha Afya Ilembo Manispaa ya Mpanda…usiri huo umesaidia kwenda na wasindikizaji au wenza wao kuangalia mjamzito anavyosaidiwa’’ amesema Dk Mdemo.

Ameongeza kuwa ni zaidi ya asilimia kumi ya wanaume wameweza kuwasindikiza wenza wao  hivyo bado inatakiwa kuendelea kuhamasisha  halmashauri katika majengo yao wanayojenga au wanayoyakarabati  waone ni jinsi gani ambavyo wataweza kutengeneza  sehemu ya  faragha ya kujifungulia  kwa wajawazito kwani kuna vituo nane pekee kati ya 130 katika Mkoa wa Katavi vinatoa huduma hiyo.

Amesema wahudumu wa afya ngazi ya jamii  ni sehemu ya jamii  tunaelewa kuwa vituo vingi vya afya hazina watumishi wengi wa kutosha  na ukiangalia maeneo mengi wamekuwa wakitumiwa  katika maeneo mengi na alitowa mfano kumekuwa na magonjwa mengi ya mlipuko  kama pindupindu kilichotokea   mwaka jana huko Karema Wilaya ya Tanganyika  wailiweza  kuwa na wahuduma wa ngazi ya afya wawili kwenye kila Kitongoji ambao waliwasaidia kusambaza   vitakasa   maji  kwa wananchi .

 Project  Officer  Clinkar  wa Thamini Uhai  Dr  Calist  Nzabuhakwa amesema   huduma hii ya msindikizaji toka wameianzisha ina muda wa miaka mitano sasa na walianzia katika Mkoa wa Kigoma kwa Katavi wameanza mwaka  2020 na kwa Mkoa wa Katavi walianza na vituo nine kwa sasa vipo nane .

Huduma hii ya msindikizaji wakati wanaianzisha  walilenga kuangalia namna ambavyo  Thamini Uhai inavyoweza kusaidiana na Serikali  namna ya kupunguza vifo vya wajawazito au kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi walipanga   kutowa huduma ya mradi huu kwenye maeneo ambayo ni magumu kufikika  kwa sababu akina wajawazito wengi walikuwa wanafika kwenye vituo walikuwa wanafika kwa kuchelewa kutokana kukimbilia kwa wakunga wa jadi .

Waliona huduma hii ya msindikizaji  inaweza kusaidia sana  kuwaleta watu walikuwa wanajifungulia kwa wakunga wa jadi  kuweza kuwapeleka kwenye vituo vya kutolea huduma za  mama na mtoto  ambapo wanapatiwa huduma zilizosahihi kuliko kwa mkunga wa jaji ambae  hanauwezo wa  kumwongezea damu mama  mjamzito anapokuwa ameishiwa damu wakati wa kujifungua au ugonjwa wa kifafa cha uzazi .

 Amesema   huduma hii kwenye maeneo yote waliyoanzisha vifo  vya  mama na mtoto vinaendelea kushuka  na mategemeo yao ni kuhakikisha  vifo   vya akina  mama ninakwisha  vinabakia  sifuli  na wakushirikiana na Serikali wanapenda huduma hii iweze kusambaa nchi nzima  haina tatizo lolote inatowa matokea chanya kwa mja mzito anapokwenda kujifungua.

Mmoja wa boda boda wa Kijiji cha Mtambo ambae ambae anatumiwa   kwa ajiri   mradi wa THAMINI UHAI ambae    pikipiki yake inatumiwa na wajawazito kwa ajiri ya kuwafikisha kwenye kituo cha Afya cha Katumba  wakati wa kujifungua unapokuwa umefika ikiwa ni katika kuhakikisha  wajawazito wanafika  kwenye kituo kwa wakati na kuokoa uhai wa mama na  mtoto

Nae  mtoa huduma wa ngazi ya jamii katika Kijiji cha  Nduwi  Kata ya Katumba Wilaya ya Mpanda  Sofia Kayanda alisema  amekuwa   muhudumu wa afya kwa kipindi cha miaka mitatu amekuwa akitowa elimu kwenye jamii   umuhimuwa  msindikiza na wameisha andaa kamati ya kumsindikiza  mjamzito kwenda kujifungua hata kama mume wake anapokuwa hayupo .

Na  kunakuwepo na watu ambao wamekuwa wameandaliwa na wanapokuwa wamepewa taarifa wanamsindikiza  mjamzito kwenda kujifungua kwa kuambatana na msindikizaji wake ambae  anae kuwa amechaguliwa na toka awali na mjazito mwenyewe kwani msindikizaji  sio lazima awe mwenza  bali ni  mtu aliyemwamini mwenyewe  mamzito .

Mratibu wa huduma za afya ya uzazi na  mpango wa Mkoa wa Katavi  Hilida Machungwa  huduma ya msindikiza wamekuwa wakihakikisha wanafanya uzimamizi kwenye  vituo  vyote nane vinavyotowa huduma hiyo  kwa  kuhakikisha akina mama wanapata elimu kuanzia  kwenye  mahudhurio yao ya killiniki wa wajawazito  juu ya umuhimu wa wao kwenda  na wasindikizaji  wakati wa kujifungua .

Wasindikizaji hao wamekuwa wakipatiwa elimu toka awali  ili pale   mjamzito anapokuwa amepata uchungu atakwenda nae kituoni  kwa ajiri ya kujifungua kwa kuwamsindikizaji huyo atakuwa amepata elimu ya kujua majukumu yake wakati wa kujifungua .huduma hii imeleta  ufanisi mkubwa  kwa idadi kubwa  kwa sasa kwenda  kujifungulia kwenye vituo hivyo vya kutolea  huduma kwa kuwa mazingira yameboreshwa.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages