Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi,ACP Kaster Ngonyani akizungumza kwenye mdahalo awamu ya pili ulioandaliwa na UTPC. |
Na George Mwigulu, Katavi.
Ushirikiano uliopo baina ya Jeshi la Polisi na Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Katavi kupitia mpango wa jeshi hilo wa polisi jamii umekuwa chachu kubwa wa kutokomeza vitendo vya kihalifu mkoani humo.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa
wa Katavi, ACP Kaster Ngonyani amezungumza hayo leo kwenye mdahalo maalumu
ulioandaliwa na Umoja Klabu za Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) na kufanyika
katika ukumbi wa St Mathias uliopo Manispaa ya Mpanda.
Lengo la mdahalo huo awamu ya
pili ni kuelimishana kitaaluma,kujenga na kuimarisha mahusiano ya mashirikiano
ya kikazi baina ya Jeshi la Polisi na Waandishi wa habari utakao saidia kuepuka
migongano inayoweza kuhatarisha zaidi usalama wa waandishi wa habari.
ACP Ngonyani amesema Jeshi la
polisi katika kutoa elimu kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi waandishi wa habari
wamekuwa kiungo muhimu kupitia vyombo vyao vya habari kuweza kuufikia umma kwa
haraka.
“Ushirikiano huu tuliokuwa nao
mwaka 2023 naomba uendelee mwaka 2024...katika kutoa elimu wanahabari ni chachu
yetu hadi sasahivi mkoa wa Katavi upo salama uharifu umepungua sana hata
ukiingia kwenye RB zetu kwenye vituo vya polisi makosa ni machache sana kwa
kuwa waandishi wa habari na jeshi la polisi pia tumeshirikiana kupinga uhalifu”
Amesisitiza ACP Ngonyani.
Akiwasilisha mada ya kuendeleza mahusiano mazuri ya jeshi hilo na vyombo vya habari,SSP Juma Jumanne amesema kuwa wanatambua umuhimu wa vyombo vya habari kwani huelimisha jamii juu ya madhara ya uhalifu,umuhimu wa utoaji taarifa za uhalifu na wahalifu mambo ambayo ni kazi ya msingi ya jeshi hilo.
SSP Juma Jumanned akitoa mada ya kuendeleza mahusiano mazuri kati ya Jeshi la Polisi na Vyombo vya habari. |
Afisa Mipango Msaidizi wa UTPC akiwasilisha mada katika mdahalo uliojumuisha jeshi la polisi na waandishi wa habari Mkoa wa Katavi ambapo amesisitiza mahusiano mazuri ya kikazi. |
SSP Jumanne amefafanua kuwa waandishi
wa habari wanaingia kwenye migogoro na jeshi la polisi pale ambapo kila mmoja
kutokutambua majukumu ya mwingine jambo ambalo linapaswa kuepukwa kwa
kujengeana uwezo wa kitaaluma.
Amesema vyombo vya habari vinanafasi
na jukumu la kuandika habari za kisayansi,kijamii,kimichezo,kimahakama na
uchunguzi kwa ufundi,kitaalamu, kiuchambuzi wa kina na kupaswa kuepuka kuripoti zaidi kuliko
kuelimisha jamii juu ya madhara ya uhalifu.
“ nitoe nukuu hii
mnielewe...mwanzilishi wa kampuni ya magazeti ya Scrips Mr Willing Scripts, aliwahi kusema jukumu la vyombo vya habari ni kuwastarehesha
wale wanaotaabika na kuwataabisha wanaostarehe na Msimamizi wa habari wa Ikulu
ya Marekani Mccury alisema huwezi kuwastarehesha au kuwataabisha watu bila
kuwapa habari bora” Amesema SSP Jumanne wakati akisisitiza waandishi wa habari
kuzingatia maadili ya kazi.
Edmund Kipungu,Afisa Mipango msaidizi wa UTPC amesema lengo la UTPC Klabu za waandishi wa habari hapa nchini zinajenga ushirikiano wa kazi kwa kuwa hufanya kazi zinazofanana japo jeshi la polisi limepewa mamlaka ya kusimamia sheria.
Afisa Mpingo huyo ameeleza kuwa
mahusiano yakiimarishwa kwa vitendo utajenga usalama kwa waandishi wa habari
pamoja na kutokomeza zaidi uharifu.
Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi
wa habari Mkoa wa Katavi, Walter Mguluchuma wakati akifunga mdahalo huo amesema
kuelekea uchanguzi wa serikali za mitaa mwaka huu na uchanguzi mkuu wa mwaka
2025 waandishi wanapaswa kuepuka kujihusisha na masuala ya kisiasa kwani
yatawapunguzia Imani kwa wananchi na kuhatarisha usalama wao.
Mguluchuma amesema waandishi wa habari wanapaswa kufanya kazi kwa kunzingatia maadili na kuepuka kuvuja sheria za nchi kwa sababu wao ni waandishi kwani watashughurikiwa kama wahalifu wengine.