Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Kaster Ngonyani akifunga Mdahalo awamu ya Tatu baina ya waandishi wa Habari na Jeshi la Polisi |
Na Walter Mguluchuma-Katavi
Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Katavi
wameaswa kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili
ya kazi zao ili kuondoa migongano baina yao
na jeshi la Polisi linapokuwa linatimiza majukumu
yao ya utendaji wa kazi kwenye matukio mbalimbali .
Waandishi wa Habari Mkoa wa Katavi wakiwa katika picha ya paomoja na kamanda wa polisi mkoa wa Katavi Kaster ngonyani baada ya mdahalo huo
Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Katavi wameaswa kufanya kazi zao kwa kuzingatia maadili ya kazi zao ili kuondoa migongano baina yao na jeshi la Polisi linapokuwa linatimiza majukumu yao ya utendaji wakazi kwenye matukio mbalimbali
Wito huu umetolewa na Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi Kaster Ngonyani wakati akifunga
mdahalo wa awamu ya tatu uliowashirikisha Wandishi
wa Habari wa Mkoa wa Katavi uliofanyika katika
ukumbi wa ST Mathias wenye lengo kuimalisha
uhusiano wa kazi baina ya wandishi na jeshi la polisi
na ulinzi na usalama kwa wandishi wakati wa matukioya hatari .
Amesema ilikuweza kuondoa mingano
ambayo inaweza kutokea kati ya wandishi wa Habari
na Jeshi la Polisi wanapokuwa wanateleza majumu
yao ni vema wandishi wakafanya kazi zao kwa
kuzingatia maadili yao na vilevile polisi nao wafanye kazi
kwa kuzingatia maadili yao ya kazi .
Kamanda Ngonyani amewahakikishia wandishi
wa Habari kuwa jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi
linaendelea kuwalinda na kuhakikisha wanakuwa salama pindi
wanapokuwa wanatimiza majukumu yao kwani wao hilo ni jukumu
lao la kuhakikisha wandishi pamoja na wananchi
wanakuwa salama .
Amesema jeshi la Polisi linatambua kuwa
wandishi wa habari ni watu muhimu sana kwenye shughuli
zao za kila siku kwani wamekuwa wakiwatumia kutowa
taarifa zao mbalimbali kwenda kwa wananchi kupitia
vyombo vyao na kuendelea kuufanya Mkoa wa Katavi
kuendelea kuwa salama zaidi
Kamanda Kaster Ngonyani
amewashukuru Muungano wa Club ya Wandishi
wa Habari Tanzania (UTPC) kwa kuweza
kuandaa midahalo hiyo mitatu kwani iweza kujenga
zaidi mahusiano katika ya jeshi la polisi na wandishi
wa habari .
Nae Afisa wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi Juma Jumanne amewahimiza kutoandika habari ambazo zinaweza kujenga chuki kwenye jamii.
Aidha amewasisitiza wasitumie vitisho wakati wanapokuwa wanatafuta habari kwani kunaweza kuwafanya usalama wao ukawa hatarini pia waepuke kuwa washabiki wa chama cha siasa kunawafanya washindwe kuaminiwa na kujengewa chuki kwenye jamii.
Katibu wa Club ya Wandishi wa Habari
Mkoa wa Katavi Pascal Katona amesema midahalo
hiyo walioifanya imefanya kuwepo na uwelewa
mkubwa zaidi wa utendaji kazi kwa wandishi wa habari na
polisi hasa kwenye maeneo yanayohusu usalama .