Serikali
katika Wilaya ya Mpanda imesema ongezeko la Bajeti katika Halmashauri
zake inaonyesha ishara ya ukuaji na ongezeko la ukusanyaji wa Mapato ili
kuwahudumia wananchi kupitia Miradi mbalimbali.
Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Mpanda Josep Lwamba wa Pili [kushoto] akiwa na viomgozi mbalimbali katika kikao hicho.
Serikali katika Wilaya ya Mpanda imesema la Bajeti katika Halmashauri zake inaonyesha ishara ya ukuaji na ongezeko la ukusanyaji wa Mapato ili kuwahudumia wananchi kupitia Miradi mbalimbali.
Akiwahutubia
wajumbe wa Kikao maalumu cha Kamati ya ushauri ya Wilaya ya Mpanda kuhusu Rasimu
ya Bajeti kwa 2024/2025 kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda na Halmashauri
ya Wilaya ya Nsimbo Jamila amsema ongezeko hilo la Bajeti kwenye halmashauri
hizo litakuwa na tija katika kuwatumikia wananchi.
‘’Nizipongeze
Halmashauri zote mbili kwenye bajeti zao utaona Halmashauri zote zimepiga hatua
tofauti na bajeti ya Mwaka uliopita hongereni kwa jitihada hizo mlizozifanya
kwa kuhakikisha kunakuwa na ongezeko la bajeti’’ amesema Jamila.
Wajumbe mbalimbali wakiwa katika kikao hicho cha Kamati ya Ushauri Wilaya ya Mpanda. |
‘’ Rasimu ya
bajeti tuliyoipitisha hapa itakapo rudishwa niwajibu wa Halmashauri kuhakikisha
malengo ya bajeti yanafikiwa nilazima kujidhatiti kwenye eneo hilo la
ukusanyaji wa Mapato pamoja na kutdhibiti matumizi yake na matumizi yalenge
manufaa kwa wananachi wetu zile asilimia ambazo zinatakiwa kurudi kwa wananchi
ziludi kwa wakati ili kutatua kero za wananachi’’ amesisitiza Mkuu huyo wa
Wilaya.
Katika hatua
nyingine amemshuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan namna ambavyo amekuwa akileta
fedha nyingi za miradi ya Maendeleo katika Wilaya ya Mpanda katika sekta
mbalimbali ikiwemo afya elimu miundombinu na Kadhalika.
Leonard Kilamuhaa Kaimu afisa Idara ya Mipango akiwasilisha Rasimu ya Bajeti katika kikao hicho kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda. |
Leonard Kilamuhaa
Kaimu Idara ya Mipango Manispaa ya Mpanda akiwasilisha Rasimu ya Bajeti kwa
niaba ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda amesema
Halmashauri hiyo imepanga kukusanya na kutumia zaidi ya Shilingi Bilioni 27.5
Edger Mnyavanu Mkuu wa Idara ya Mipango na uratibu Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo akiwasilisha Rasimu ya Bajeti kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo. |
Kwa upande
wake Edger Mnyavanu Mkuu wa Idara ya
Mipango na uratibu Halmashauri ya Nsimbo akiwasilisha Rasimu ya Mpango wa
Bajeti kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo amesema halmashauri
hiyo kwa mwaka 2024/2025 imepanga kukusanya na kutumia zaidi ya Shilingi
Bilioni 26 .889.
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph [kushoto] akijadili jambo na Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli kwenye kikao hicho. |
Kikao hicho
kilikuwa na lengo la kupitisha Rasimu ya Bajeti kwa halmashauri ya Manispaa ya
Mpanda na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo pamoja na kupendekeza kuongezwa kwa
maeneo ya utawala kweye Halmashauri hizo.