WAKULIMA WA TUMBAKU WATAKIWA KUACHA KUTUMIA VIUATILIFU VISIVYOKUBALIKA

Emanuel Sanka Mrajisi Msaidizi na tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania akiwa hutubia wajumbe wa kikao hicho.


Na Walter Mguluchuma-Katavi

Wakulima wa Tumbaku  wanaotumia   viuatilifu  visivyokubalika  kwenye zao la Tumbaku wameobwa kuachakufanya hivyo kwani wanahatarisha soko la Tumbaku Duniani kunakoweza kusababisha Tumbaku ya Tanzania kukosa soko la Tumbaku kimataifa.

wajumbe wa    mkutano  mkuu wa    30 wa  Chama   Kikuu  cha  Ushirika  cha  Mkoa wa Katavi  Lactu wakiwa  kwenye   mkutano  wao ulifanyika   katika  ukumbi wa Manispaa ya  Mpanda wakijadili  mambo  mbalimbali  yanayohusu  maendeleo ya ushirika  wao

Wakulima wa  Tumbaku  wanaotumia   viuatilifu  visivyokubalika  kwenye zao la Tumbaku wameobwa kuachakufanya hivyo kwani wanahatarisha soko la Tumbaku Duniani kunakoweza kusababisha Tumbaku ya Tanzania kukosa soko la Tumbaku kimataifa.

Wito huu umetolewa  na  Meneja  wa  Chama  Kikuu  cha  Ushirika  cha  Wakulima wa Tumbaku    Mkoa wa  Katavi (LATCU ) Pius Killo  wakati wa mkuu tano  mkuu  wa 30 wa  Chama  hicho uliofanyika  katika  ukumbi wa Manispaa ya Mpanda .

Amebainisha kuwa wapo  baadhi ya  wakulima wa zao la  Tumbaku  wanahatarisha   soko  la Tumbaku  kwenye masoko ya  Kimataifa  kwa kutumia   viatilifu  ambavyo havitakiwi  kutumiwa  kwenye zao hilo  kama  vile viatilifu  vya kuua  Mbu .

Amewasisitiza wakulima kuacha kudanganywa  na  wafanya  biashara wanaouza  pembejeo za kilimo  ambazo  baadhi ya viatilifu  hivyo havisitahili kutumika  kwenye zao la Tumbaku .

Emanuel Sanka Mrajisi Msaidizi na tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania akiwa hutubia wajumbe wa kikao hicho.

Killo  ameeleza kuwa   hali ya  uzalishaji wa zao la Tumbaku  katika  Mkoa wa  Katavi imekuwa ikiongezeka  kutokana  na  Serikali kufanya  kazi kubwa ya  kufungua  masoko  tofauti na hali  ambayo iliyokuwepo  hapo  nyuma ya wakulima kukosa  masoko ila  kwa sasa masoko ni ya  uhakika  mkulima  hana kisingizio tena bali ashindwe  mwenyewe .

Amefafanua kuwa  kwa  msimu wa  kiliomo 2022/2023  wakulima wa zao  la  Tumbaku wa Mkoa wa Katavi wamezalisha kilo  11,150,776  zenye  thamani ya  Dola   za Kimarekani  zaidi ya Milioni 25.9 ambapo  kwa msimu  huu wa Kilimo wa  2023/2024 wamepanga kuzalisha kilo  Milioni 20.

Kuhusu pembejeo za kilimo amesema kuwa  msimu huu   mbolea    za Tumbaku zimefika kwa wakati  tofauti na huko nyuma  ingawa hadi sasa  changamoto walionayo wakulima  ya  vifungashio   aina  ya  nyuzi   aina ya  Jute  twine  na  New  Hessian   cloth.

Killo  ameiomba  Serikali  katika  kipindi hiki  cha  kuelekea  kwenye  msimu huu wa  ununuz wa  Tumbaku  wawasaidie wakulima kwa  kuboresha miundo  mbinu ya  barabara   zilizoharibika  kutokana na mvua za  msimu huu  ili  kuweza  kumwezesha  mkulima kuweza   kusafirisha  tumbaku yake kupeleka  kwenye soko bila   shida na kumfanya aweze kuuza kwa wakati .

Amesema kwa sasa  katika  Mkoa huu  unayomakampuni  matatu  ya ununuzi  wa zao hili  ambayo ni  Premium  Active  Tanzania  Limeted ,Mkwawa  Leaf  Tobacco  L td  na   Obamco  Tobacco   Ltd .

Nae Mrajisi Msaidizi wa vyama ushirika   na tume ya  Maendeleo  ya  ushirika Tanzania Emanuel Sanka  amesema kuwa zipo taarifa  za baadhiya  vyama  vinatumia  viatilifu   visivyokubalika  kwenye zao hilo  jambo ambalo ni hatari  kwenye soko la Tumbaku   nchini .

Amefafanua  kuwa soko la  Tumbaku linamwongozo  yake  na  lina takiwa   kukidhi matakwa  ya  Kimataifa  ikiwa  na   pamoja na kutumia   pembejeo  zinazokubaliwa  na  Halmashauri ya  Tumbaku  Tanzania

Amesisitiza kuwa juhudi zilizofanyika na serikali za kutafuta masoko ya Tumbaku haziwezi kukamishwa na watu wachache wasiofuata taratibu.

Sanka amesema kwa sasa  zoezi  la  upandaji miti   ngazi ya  AMCOS    bado  hairidhishi  hivyo alitowa  ushauri   kwa kamati  ya  Mkoa  inayokagua  miti  itengeneze  mpango  wa kuhakikisha  miti  inayooteshwa  kwenye  vitalu  inapandwa  mashambani   na  inafatiliwa  mpaka   inakuwa na  kusitawi .

Sanka ameipongeza  Latcu   Ltd  kwa  namna   inavyoendelea  kutimiza  majukumu yake  kwa kuzingatia  sheria   ya  vyama  vya ushirika  Namba   6 ya mwaka 2013 na  kanuni zake za mwaka 2015 pamoja  na miongozo mbalimbali waliojiwekea .

Nae mkulima wa zao hilo   Mohamed Said  ameiomba  Serikali  iwaangalie na wakulima wa zao la Tumbaku  kwa kuwapatia  mbolea  ya  ruzuku  kama ilivyo  kwa wakulima wa zao la  mahindi .

Nae  Fibelti  Ngula   Makamu   Mwenyekiti wa  Latcu   amesema  kumekuwepo na  changamoto ya  baadhi ya wakulima  kuchanganya  tumbaku wakati wa  masoko kwa kuweka  tumbaku chafu  hali ambayo imekuwa  ikihalibu    soko la tumbaku .

Chama kikuu cha ushirika lactu cha Mkoa wa Katavi kinajumla ya Wananachama 18 Amcos zinazolima zao la Tumbaku ambavyo vimekuwa mhimili wa kuchangia Mapato kwenye Halmashauri husika.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages