KAMATI YA USHAURI YA MKOA WA KATAVI WAPENDEKEZA BAJETI YA BILIONI 126

 

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akiwa hutubia wajumbe kwenye kikao hicho

Na Walter Mguluchuma-Katavi

Kamati ya  ushauri ya  Mkoa wa  Katavi (RCC)  imepitisha  mapendekezo ya  Bajeti  ya  Serikali kuu na  Halmashairi zake zote  tano za  Mkoa huu ikiwa  imelenga kutatua  kero mbalimbali za wananchi na kutekeleza miradi mbalimbali ya  Maendeleo .

Wajumbe mbalimbali wakiwa katika kikao hicho cha Kamati ya ushauri Mkoa wa Katavi.

Kamati ya  ushauri ya  Mkoa wa  Katavi (RCC)  imepitisha   mapendekezo ya  Bajeti  ya  Serikali kuu na  Halmashairi zake zote  tano za  Mkoa huu ikiwa  imelenga kutatua  kero mbalimbali za wananchi na kutekeleza miradi mbalimbali ya  Maendeleo .

Mapendekezo  hayo ya  Bajeti ya    msimu wa  fedha wa 2024/2035 yamepitishwa  na  kikao  hicho cha  RCC kilichofanyika  katika  ukumbi  ya  ofisi ya  Mkuu wa  Mkoa wa  Katavi  na kiliongozwa  na  Mkuu wa  Mkoa wa  Katavi  Mwanamvua  Mrindoko .

Mkuu wa  Mkoa wa  Katavi  Mwanamvua  Mrindoko amewaambia  wajumbe wa Kikao hicho      cha  kamati ya  ushauri ya  Mkoa wa Katavi  kuwa  Mkoa wa  Katavi umeomba  kuinidhishiwa  Bajeti ya  kiasi cha  Shilingi  Bilioni  126 ambapo   bajeti ya  msimu  uliopita ilikuwa ni  kiasi  cha   shilingi Bilioni  ` 116   bajeti ya  msimu  huu ukiwa imeongzeka  la  asilimia    saba  sawa na ongezeko la  asilimia  sita

Mrindoko  amewweleza wajumbe wa kikao hicho kuwa  kwa  kipindi cha  miaka  miwili  Rais  Samia  Suluhu  Hassan  amefanya  kazi kubwa  katika   Mkoa wa Katavi  kwa  kuhakikisha  fedha  za  kuleta  maendeleo kwenye  Mkoa  huu  zinapatikana .

Na katika  kipindi hiki cha  miaka  miwili   ameweza  kuleta  kiasi cha   zaidi ya  shilingi  Bilioni   818  kwenye  sekta   mbalimbali   zilizopo  katika   Mkoa huu  vikiwemo  sekta  za  uchukuzi ,  afya   ,kilimo , maji   barabara   ,elimu  na  nyinginezo .

Amebainisha  kuwa   fedha  hizo   zimeweza kusaidia sana  kwa kuweza  kuongeza   huduma  mbalimbali kwa wananchi na kupunguza  baadhi ya  kero  zilizokuwepo .

Kikao hicho cha  RCC  Mkoa  wa  Katavi  kimepitisha  mapendekezo ya  kuanzisha  Wilaya   mpya ya  Mpimbwe  na   Jimbo   jipya  la  Karema    pamoja  na  Kata   mbalimbali na  vitongoji ,Mitaa  na  Vijiji.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages