NMB YATOA MSAADA WA BATI WA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 13 IKIWEMO SHULE WANAYO SOMEA KANISANI

 

Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Magharibi Seka Urio akizungumnza katika Hafla ya kutoa Bati 200 katika Kijiji cha Kapanda kwaajili ya kusaidia ujenzi wa Shule ya Msingi Kapanda.


Na Walter Mguluchuma-Mpanda

Benki ya  NMB  imetoa  msaada wa  bati  400  zenye  thamani ya  zaidi ya  shilingi  milioni 13 kwa ajiri ya  ujenzi wa  Shule  mbili za  Msingi  katika  Halmashauri ya  Nsimbo  Wilaya ya  Mpanda  Mkoani  Katavi  ikiwepo  shule ya  Msingi  Kapanda  ambayo wanafunzi wake 280 wa kuanzia  darasa  la awali hadi darasa  la tatu wanasoma kwa kutumia jengo la  Kanisa  ikiwa ni kuunga  mkono jitihada  za kuunga  mkono Serikali ya  awamu ya sita  ya kusimamia  upatikanaji wa elimu bora .

Benki ya  NMB  imetoa  msaada wa  bati  400  zenye  thamani ya  zaidi ya  shilingi  milioni 13 kwa ajiri ya  ujenzi wa  Shule  mbili za  Msingi  katika  Halmashauri ya  Nsimbo  Wilaya ya  Mpanda  Mkoani  Katavi  ikiwepo  shule ya  Msingi  Kapanda  ambayo wanafunzi wake 280 wa kuanzia  darasa  la awali hadi darasa  la tatu wanasoma kwa kutumia jengo la  Kanisa  ikiwa ni kuunga  mkono jitihada  za kuunga  mkono Serikali ya  awamu ya sita  ya kusimamia  upatikanaji wa elimu bora .

Awali  kabla ya kukabidhiwa kwa  msada huo  Diwani wa  Kata ya Machimboni  Raphael Kalinga  alieleza kuwa   shule ya  Msingi Kapanda  iliyokabidhiwa  msaada huo  wanafunzi  zaidi ya wanafunzi 280 wa kuanzia  darasa   la awali  hadi la  tatu wanasoma  shule kwenye jingo la  kanisa  ambalo  hutumiwa pia  kwa ajiri ya  ibada  kijijini hapo .

Msaada huo wa  bati hizo umekabidhiwa  na  Meneja  wa  NMB   Kanda ya  Magharibi  Seka  Urio  katika  hafla ya  makabidhiano hayo  iliyofanyika  katika   Vijiji vya  Kapanda  Kata ya  Machimboni na  katika  Kijiji cha   Masewela    Kata ya  Ibindi 

Amebainisha kuwa   NMB  walipokea  maombi  kutoka  katika  Halmashauri ya Nsimbo  ya kuchangia  maendeleo ya  elimu  na walifarijika kupokea   maombi hayo  na  ndipo walipo amua  mara  moja   kuweza  kushirikiana na  Halmashauri hiyo  ili kuwa  chachu  ya maendeleo ya sekta ya  elimu  kwa jamii.

 Amesema  jumla ya  thamani  ya  vifaa  ambavyo wameweza  kukabidhi   kwa shule hizo mbili  ni  bati 400   yenye  thamani ya   shilingi  13,400 ambapo  shule ya  Msingi  Kapanda  imekabidhiwa  bati 200  yenye  thamani ya  shilingi  6,700,000 na  shule ya Msingi   Masewela  bati 200  zenye  thamani ya shilingi 6,700,000.

Meneja huyo amaesema Wanatambua   juhudi za  Serikali  ya  awamu ya sita  chini ya  Rais  Dkk  Samia   Suluhu  Hassan  za kusimamia  upatikanaji wa  elimu  bora  kwa  nguvu zote  kwa kuboresha  mazingira  ya  utoaji  wa elimu bora  kwa nguvu zote  kwa kuboresha mazingira  ya  utoaji  wa  huduma   hizi   mjini   na  vijijini .

  Seka   ameeleza kuwa   pamoja   na   makubwa   mengi  yaliofanywa  na  Serikali   NMB  kama  wadau  wanao wajibu  wa  kuunga  mkono  juhudi   hizi  maendeleo  kwa kusaidia   jamii kwani jamii  ndio  wanaifanya    NMB    kuwa   hapa  ilipo  na kuwa   kubwa kuliko   benki  yoyote  ili  hapa  nchini .

Vifaa  hivyo walivyotowa  kwa  Halmashauri hiyo  ni  moja wa   ushiriki  wao  katika   maendeleo  ya  jamii na wao  kama  benki   inayoongoza   Tanzania  hivyo wanao wajibu  wa kuhakikisha  jamii  inayowazunguka  inafaidika  kutokana na faida walioipata .

Amefafanua kuwa   kwa miaka   kadhaa  NMB   imekuwa  ikisaidia miradi mbalimbali  ya  maendeleo  kwa wananchi  kwa kujikita  zaidi  kwenye miradi  ya  elimu  na  afya  na  kusaidia  kwenye  majanga  yanapokuwa yametokea  kwa kutambua   wateja wao wengi wanatoka  kwa  hiyo kurudisha  sehemu ya  faida  kwenye jamii  wao ni  utaratibu wao .

Ameeleza kuwa  NMB  wamekuwa  wakipokea   maombi mengi  sana  ya kuchangia  katika  miradi ya  jamii  lakini  benki   hiyo  imejikita  zaidi  katika  maeneo  ya  elimu ,afya  na misaada  ya  hali  na  mali  katika  nyakati  ngumu  kama za matokeo ya  majanga .

Seka  amesema   Benki ya  NMB    imekuwa  mstari wa  mbele  kuchangia   huduma  za  kijamii  kwa  lengo  la kurejesha  sehemu  ya  faida  kwa  jamii  na wamekuwa wanafanya hivyo  kwa zaidi ya miaka  miaka saba sasa  mfululizo  kwa kutenga  asilimia  moja  ya faida  yao  kama sehemu ya  kwenye jamii  inayowazunguka .

Mbunge wa  Jimbo  la  Nsimbo  Anna  Lupembe  ameishukuru   Nmb kwa kuweza  kuwatowa  msaada huo kwa shule hizo mbili  kwa  kutambua  mahitaji  hayo  kwenye  shule  hizo kwa kuwa sehemu ya kumuunga  mkono  Rais  Samia   katika kuboresha miundo mbinu ya  elimu .

Alisema  watoto wanao soma kwenye  kijiji  hicho  mazingira sio  mazuri  sana  ambayo yalikuwa yakiwafanya  wanapofikia  darasa  la  nne     kwenda  kusoma  kwenye shule  nyingine  zilizombali na kijiji  hicho ndio maana wananchi wakaamua kujenga shule  kijijni hapo ambayo imepewa  msaada huo wa bati na NMB.

Amesema  majengo yaliyojengwa   shuleni Kapanda   yote saba na vyumba vya viwili vya walimu ni nguvu ya wananchi  lengo kubwa  la  kujenga  majengo hayo ya  shule ni watoto  kubaki  kwenye  mazingira ya Kijiji kwa sababu kutoka  kijiji  kimoja  kwenda  kijiji kingine  umbali ni  mrefu .

Lupembe  amesema  yeye  kama     Mbunge  amekuwa akitowa  fedha  za  mfuko wa jimbo kwa  kununua  vifaa vya  ujenzi  kwenye  shule ya  Kapanda  ambayo  imekabidhiwa  msaada wa   bati  200  na  benki ya  NMB  ambayo imetowa  msada huo pia kwa shule ya  Masewela .

Diwani  wa Kata ya  Machimboni  Raphael  Kalinga  alisema  wanaishukuru  Nmb  wa kuwapatia  msaada wa   bati   kwa ajiri ya shule ya Msingi  Kapanda  ambayo wanafunzi wake wa kuanzia  darasa la awali hadi la tatu wanasomea kanisani .

 Ameiomba  Halmashauri ya  Nsimbo  kupoleka  fedha  za  kuenzekea  paa  ya majengo ya shule  hiyo  ili   bati  walizopewa  na  NMB   ziweze kuenzekea  majengo  hayo  ili  watoto wanaosomea  kwenye jingo la     ibada  la Kanisa watoke na wahamie kwenye shule hiyo. 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages