RC AWAGIZA VIONGOZI WA MKOA NA WILAYA KUSIMAMIA BEI ELEKEZI YA SUKARI

 

Mwanamvua Mrindoko Mkuu wa Mkoa wa Katavi akizungumnza na waandishi wa Habari ofisini kwake 

Na Walter mguluchuma-Katavi

Mkuu wa  Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko  amewaagiza  Wakuu  wa Wilaya za  Mkoa wa Katavi   kuhakikisha wanafatilia na kuthibiti   bei ya  Sukari elekezi  iliyopangwa kuuzwa  Mkoa wa Katavi inauzwa kwenye maeneo yote .

Baadhi ya waandishi wa Habari mkoa wa Katavi wakiwa katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Katavi

Mkuu wa  Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko  amewaagiza  Wakuu  wa Wilaya za  Mkoa wa Katavi   kuhakikisha wanafatilia na kuthibiti   bei ya  Sukari elekezi  iliyopangwa kuuzwa  Mkoa wa Katavi inauzwa kwenye maeneo yote .

Mkuu wa  Mkoa  ametoa  maagizo hayo wakati alipokuwa akitowa taarifa  mbele ya wandishi wa  habari ofisini kwake juu ya hali ya upatikanaji wa  sukari ndai ya Mkoa huu ambapo  hadi sasa  hakuja tokea hali ya upungufu wa  sukari .

Amebainisha kuwa  hadi sasa  Mkoa umepokea sukari ya kutosha ambapo kwa kipindi cha mwezi mmoja na nusu wamepokea  tani 244   za sukari  na zipo kwa wasambazji wakubwa wawili na  tayati  zimeisha anza kuuzwa  kwa wafanya biashara wengine.

Florence Chrisant  katibu tawala masiadizi sehemu katibu tawala msaidizi sehemu ya biashara na uwekezaji Mkoa wa Katavi[ wa tatu kulia] Katikatikati Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Sophia Kumbuli .

Amesema kuwa  kwa kipindi hiki hawatarajia  mwananchi kukosa sukari dukani  na pia  hawatarajia mfanya biashara yoyote wa  reja  reja kukosa bidhaa ya sukari dukani kwake .

Mrindoko ameeleza kuwa  sukari hii inatolewa kwa utaratibu  ambapo Serikali imeisha lipia kodi na ndio maana imeweka bei elelezi  kwa kupitia walaka  wa GN  ya  Serikali   namba  40  A na  B   ya  tarehe 23   ya  mwezi Januari  2024 na kwa mujibu wa  GN  hiyo  bei  elekezi ya  Sukari kwa  Mkoa wa  Katavi  kwa reja  reja ni kati ya tshs 2,900 na  tshs 3200 kwa kilo moja ya sukari  na  bei hiyo inauzwa  kwa Mkoa mzima  bila kujali yuko Wilaya gani .

Kwa  hiyo bei hii  elelezi  kwa  mapenzi yake   makubwa kwa wananchi  Rais  Samia  Suluhu  Hassan ameisha ilipia kodi  na ndio maana kukawa na walaka elekezi  ambayo haita husisha  maswala ya kodi  na  hasa kwa  mlaji wa  mwisho ambae ni  mwananchi .

Bidhaa ya sukari ikiwa inashushwa katika mkoa wa Katavi kwaajili ya kupunguza tatizo la uhaba wa sukari

Amesisitiza kuwa wafanyabiashara wakubwa wanaosambaza  sukari  wahakikishe  wanapouza wazingatie  bei elelezi na wanapouza  lazima wauze kwa wafanya biashara  wa rejareja ambao wanaleseni  za biashara na pia  wakati wa kuuza na kununua wazingatie sheria za Serikali  na kutowa resiti wakati wa  mauzo .

Amewaagiza wafanya biashara wote  wa rejareja  kuhakikisha wanauza bei  elekezi ya sukari kwa kilo moja kwa tshs 2.900 na 3,200 na kwamaana hiyo    anapiga  marufuku  katika  Mkoa wa  Katavi sukari kuuzwa kwa zaidi ya bai hiyo  hivyo wananchi wanunue kwa kuzingatia bei hiyo na sio zaidi ya hapo .

Kwa  hiyo vyombo vya dola katika Mkoa wa Katavi wamekuwa wakipita   kila maeneo  kuona kama kuna  mtu ambae   amekiuka  maelelezo hayo  ya  Serikali na  ndio maana siku ya juma tano tarehe 28 mwezi huu wa pili wamewakamata wafanya biashara wa rejareja wakiuza sukari  kwa bei ya juu ya elekezi na  tayari hatua  mbalimbali za kisheria zimechukuliwa  na  serikali ya Mkoa wa Katavi haitachoka iwe   mchana au usiku wakipata taarifa ya mfanya biashara kuuza bei ya juu watamkamata tuu.

Amewagiza wakuu wa Wilaya zote za Mkoa huu kupitia  kamati zao za usalama kuhakikisha  wanafatila na kudhibiti  bei elelezi ya sukari ndio inayouzwa kwenye maeneo yao  yote .

amewataka viongozi   dola ngazi  ya  Mkoa pamoja na   ngazi ya  Wilaya  Tarafa Kata   na  Vijiji  pamoja   mtaa  washirikiane kusimamia jambo hili  na kuhakikisha sukari inafika kwa wananchi  na inauzwa katika bei elelezi .

Nae  Salome  John   Mkazi wa  Mtaa wa  Kawajense  amesema kuwa  hari ya  upatikanaji wa  sukari kwenye maduka yalipo kwenye mtaa wake  ni yakuridhisha kwani  haja wahi kufika  dukani anapokuwa anahitaji sukari na kukosa muda wote sukari ipo .

Kwa  upande wake Michael  Lumalisha    mkazi wa  Mtaa wa  Majengo amebainisha kuwa  yeye  changamoto ya sukari amekuwa akiisikia tuu kwenye   vyombo vya habari kwenye  baadhi ya  Mikoa  lakini kwa  Mkoa wa Katavi   hajawahi kusikia kuwepo   na changamoto hoyo kwani sukari muda wote inapatikana. 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages