RC AAGIZA JESHI LA POLISI KUFANYA UCHUNGUZI WA TUKIO LA MTOTO KUBAKWA NA MFUNGWA

 

Mkuu wa mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizungumnza na waandishi wa Habari ofisini kwake.


Na Walter Mguluchuma-Katavi

Mkuu wa  Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko amewaagiza  Makamanda wa Jeshi la   Polisi  na  Magereza  wa Mkoa wa Katavi  kuhakikisha  wanamchukulia hatua  mfungwa anae tuhumiwa kufanya kitendo cha ukatili  cha kumbaka   mtoto wa miaka 13 .

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi wa kwanza Kushoto akiwa na maafisa wa Magereza wakisikiliza maagizo ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi.

Mkuu wa  Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko amewaagiza  Makamanda wa Jeshi la   Polisi  na  Magereza  wa Mkoa wa Katavi  kuhakikisha  wanamchukulia hatua  mfungwa anae tuhumiwa kufanya kitendo cha ukatili  cha kumbaka   mtoto wa miaka 13 .

 Agizo hilo amelitowa leo wakati aliokuwa akizungumza na Wandishi wa  Habari ofisini kwake kuhusiana na tukio lililotokea wiki iliyopita  la  mfungwa  mmoja wa Gereza  la  Kilimo   la Kalilankulunkulu  kudaiwa kumbaka  msicha wa miaka 13 jina  limehifadhiwa wakati alipokuwa akitoka shambani kupanda  mpunga .

Mrindoko  alisema  kama  ambavyo  ilivyotararibu za  sheria  ilivyo   kwa mtu yeyote ambae  atakae  husika  katika  kufanya tukio    lolote la ubakaji bila kujari  cheo   hali yake  na umri  wake ni lazima  sheria   zichukuwe  mkondo wake .

Amesema   tukio hili   limeisikitisha  Serikali ya  Mkoa wa  Katavi  kwani   jambo hili  limemuhisisha  mfungwa  ambae   alikuwa  kwenye chombo  cha dola  hivyo jambo hili  linashughulikiwa kwa  mujibu wa  sheria .

Amesema kumekuwepo na  tahaluki juu ya tukio la mtoto ambae jina limehifadhiwa  Mkazi wa  Kijiji cha Kawanzige ambae  anadaiwa kubakwa  na  mfungwa wa gereza hilo  mnamo  tarehe 29  mwezi wa pili  ambapo kwa sasa   tukio hilo   linafanyiwa kazi na vyombo vya Dola .

Mkuu  huyo wa Mkoa wa Katavi anamwagiza  Kamanda wa Polisi wa   Mkoa wa Katavi  na  Mkuu wa  Magreza  wa  Mkoa wa Katavi kuhakikisha wanamchukulia hatua   aliyehusika  kufanya kitendo hicho cha kikatili .

Amewaondoa  mashaka wananchi ambao wamekuwa na mashaka  kuwa  jambo hilo linaweza lisishughulikiwe amewahakikishia wananchi kuwa jambo hili  litashughulikiwa  kwa mujibu wa sheria za  nchi  na wala  hakutakuwa na upendeleo wowote ule wala  kitu  ambachokitakacho  fichwa  jambo hilo  anahakikisha linashughulikiwa  kwa sheria kwa ailimia mia moja .

Amesisitiza kuwa swala  hili  litashughulikiwa   kwa mujibu wa sheria  na  taratibu jambo hili lipo kwenye mikono ya sheria  na  linashughulikiwa kama  ambavyo  linavyoshughulikiwa likitokea kwenye sehemu  nyingine.

Aliwaomba wazazi na jamii ya wananchi wa Mkoa wa Katavi  kwa kuwa matukio ya ubakaji  yamekuwa yakilipotiwa   lakini  kumekuwa na tabia ya  wazazi  wanapotakiwa kwenda kutowa ushahidi Mahakamani  wamekuwa  hawaendi na matokeo yake  wamekuwa wakisababisha watuhumiwa kuachiwa huru .

Amewaomba wazazi wa na walezi ktoa ushirikiano wa ushahidi pindi kesi hizo zinapokuwa zinaendelea katika vyomo vya kutoa haki.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages