Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko [katikati] akioneshwa mchoro wa ramani ya jengo la kusafisha Damu litakalojengwa katika hospitali ya Rufaa mkoa wa Katavi. Picha na Paul Mathias |
Na Walter Mguluchuma-Katavi
Wananchi
wa Katavi wanaondokana na changamoto
ya adha waliokuwa nayo ya
kusafiri umbali mrefu na wengine
kuhamisha makazi kwenda katika Mikoa
mingine kutafuta huduma ya
usafishaji wa damu baada ya
Hospitali ya Mkoa wa Katavi kupatiwa
fedha zaidi ya shilingi Milioni 190 kwa ajiri ya ujenzi wa jengo la huduma
ya usafishaji wa damu .
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi,Dk Serafini Patrice mwenye Miwani akimuonyesha Eneo mkuu wa Mkoa wa Katavi mwanamvua mrindoko ambalo litajengwa jengo la kusafisha damu |
Wananchi wa Katavi wanaondokana na changamoto ya adha waliokuwa nayo ya kusafiri umbali mrefu na wengine kuhamisha makazi kwenda katika Mikoa mingine kutafuta huduma ya usafishaji wa damu baada ya Hospitali ya Mkoa wa Katavi kupatiwa fedha zaidi ya shilingi Milioni 190 kwa ajiri ya ujenzi wa jengo la huduma ya usafishaji wa damu .
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua
Mrindoko amesema usafishaji
wa damu ni kilio ambacho
walikuwa nacho kama Mkoa kwa muda
mrefu lakini sasa
wanamshukuru sana Rais DK
Samia Suluhu Hassan akishirikiana na viongozi wengine wanao usimamia Mkoa wa Katavi moja kwa moja kama
vile Waziri wa TAMISEMI na Waziri wa Afya .
Amewapongeza kwjitihada kubwa
walizofanya za kuhakikisha Mkoa unapata
fedha za ujenzi wa jengo hilo ambapo mashine
za kisasa za kusafishia damu zilikuwa
zimeisha letwa katika Hospitali
hiyo ila zilikuwa hazijaanza kufanya
kazi kutokana na kutokuwepo kwa jengola kutolea huduma hiyo
Mashine za kusafisha Damu zikiwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Katavi huku ujenzi wa jengo hilo ukiwa unakaribia kuanza. |
Amesema
Serikali ya Mkoa ili
kabidhiwa na kuaminiwa
kujenga na kusimamia ujenzi wa Hospitali ya Mkoa katika ujenzi wa kwa awamu mbalimbali na
wamesimamia na wataendelea kusimamia ili
kuhakikisha kila fedha inayokuja inatimiza malengo yaliyokusudiwa .
Amesema Rais Samia
ameendelee kuujali Mkoa wa Katavi
kwa kuendelea kuboresha huduma za
afya katika Mkoa huo ambao haukuwa
na hospitali na sasa
tayari ipo imekamilikana imeanza kufanya kazi.
Mganga Mkuu
mfawidhi wa Hositali ya Rufaa ya Mkoa wa
Katavi Dkt Serafini Patrice amesema kuwa kwa
sasa hospitali hiyo haitowi
huduma ya usafishaji wa damu licha ya kuwa wameishapatiwa mashine za
kusafishia damu kutokana na kutokuwa na jengo la
kutolea huduma hiyo .
Amefafanua kuwa jengo hilo
linahitaji kiasi cha shilingi
milioni 400 lakini fedha
hizo milioni 196
zitaweza kujenga kwa awamu ya kwanza na huduma zikaanza kutolewa bila
shida na wanatarajia kuanza kutowa
huduma kwa vitanda sita kwa wakati
mmoja na
tayari wanazo hizo mashine sita za kuchuja damu
Dkt Patrice amesema
mchakato wa ujenzi wa jengo hilo umeisha
anza na wanatarajia baada ya
miezi miwili au mitatu ujenzi huu utakuwa umekamilika na huduma zitaanza
kutolewa kwa wananchi na
wataondokana na changamoto ya kusafiri kwenda umbali mrefu kutafuta
huduma hiyo .
Amesema wananchi wengine wa Mkoa
huu sasa hivi wapoMwanza, Mbeya
Dodoma na kwingineko
kufuata huduma ya uchujwaji wa
damu na wanazaidi ya miaka miwili sasa wamelazimika kupanga vyomba huko
ili kupata huduma hiyo na kuziacha familia zao
kwa hiyo huduma hiyo sasa watarudi huku
na kuendelea kupata huduma hiyo .
Yeye
kama Mbunge anayofuraha kubwa kuona huduma
hiyo intolewa kwenye Mkoa
huu imekuwa ni kama ndoto kwa jinsi ambavyo ilikuwa ni changamoto kwa mtu alipokuwa akiandikiwa kwenda
rufaa kupata huduma hiyo kwenye
hospitali za Kanda .
Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidari Sumry amesema kuwa Serikali imefanya kazi kubwa ya kuboresha huduma za afya na kwa mfano tuu ni wananchi wa Mkoa huu walikuwa wakisafiri kwenda kwenye mikoa mingine pia kutafuta huduma za meno lakini sasa hivi hospitali hiyo imeletewa vifaa vya kisasa na huduma wananchi wanapatiwa hapo.