WADAU WA HABARI WAIPONGEZA UTPC KWA MIDAHALO NA JESHI LA POLISI


Uongozi wa Jeshi la Polisi na Viongozi wa vyama vya Siasa na wadau wengine wakiwa katika picha ya Pamoja na waandishi wa habari mkoa wa Katavi baada ya mdahalo huo.


Na Paul Mathias-Katavi

Baadhi ya wadau wa maswala ya habari katika mkoa wa Katavi wameupomgeza Umoja wa klabu za waandishi wa Habari Tanzania [UTPC] kwa kuja na mpango maalumu wa kufanya midahalo baina ya Jeshi la Polisi na waandishi wa habari kwa lengo la kudumisha umoja na mshikamano katika utekelezaji wa majukumu yao.

David Mutasya kamishina msaidizi wa Jeshi la Polisi mkoa wa Katavi [kushoto] akibadilishana nyaraka za maazimio ya mdahalo huo na Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Katavi Walter Mguluchuma

Baadhi ya wadau wa maswala ya habari katika mkoa wa Katavi wameupomgeza Umoja wa klabu za waandishi wa Habari Tanzania [UTPC] kwa kuja na mpango maalumu wa kufanya midahalo baina ya Jeshi la Polisi na waandishi wa habari kwa lengo la kudumisha umoja na mshikamano katika utekelezaji wa majukumu yao.

Wadau hao wamebainisha hayo katika Mdahalo wa Nne baina ya Jeshi la Polisi na waandishi wa Habari uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa St Mathias Manispaa ya Mpanda.

Amani Mahela Mwenyekiti wa Jumuiya ya wafanya biashara Mkoa wa Katavi akiwa katika mdahalo huo amesema midahalo itakwenda kupunguza msuguano wa kiutendaji baina ya waandishi wa Habari na Jeshi la Polisi kwakuwa kila mmoja atakuwa ametambua  mipaka ya kazi yake.

‘’Midahalo kama hii naona ilichelewa sana ingefanyika kabla hata ya miaka Kumi ila kwa pekee niwashukuru UTPC kwa kuja na muono huu sasa hatuta talajia migongano ya waandishi wa habari na jeshi la polisi’’-Mahela

Ameeleza kuwa tangu midahalo hiyo ianze kufanyika tangu mwaka jana imekuwa na tija kiundendaji baina ya makundi hayo mawili katika katika kutekeleza majukumu yao.

‘’Kuna kitu ambacho nakiona kimepadwa kizuri kimahusiano lakini pia kinaleta uhuru kwa waandishi wa habari sababu ya midahalo hii’’ –Mahela

Edina Buzima Katibu wa UWT Mkoa wa Katavi akimwakilisha Katibu wa CCM Mkoa wa Katavi akichangia mada katika mdahalo huo amesema waandishi wa habari ni chachu kwa kuchochea maendeleo kupitia kuipasha habari jamii.

Waandishi wa Habari Mkoa wa Katavi wakiwa katika Picha ya Pamoja na viongozi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi na viongozi wa Siasa baada ya Mdahalo huo

Buzima ameeleza kuwa katika vyombo vya habari imefika wakati sasa wa kwenda pamoja na usawa katika majukumu ya kihabari baina ya wanawake na wanaume katika vyumba vya habari na katika kazi mbalimbali za kihabari.

‘’Tunatambua umuhimu wa vyombo vya habari tunashukuru kwa mdahalo huu sisi kama wadau nawapongeza sana UTPC kwa mdahalo huu niwakumbushe tu kuzingatia swala la usawa wa kijinsia katika masuala ya kihabari hasa katika matukio mbalimbali wapeni nafasi waandishi hawa wa kike’’-Buzima

Kwa upande wake David Mutasya Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi mkoa wa Katavi kwa niaba ya kamanda wa Polisi mkoa mkoa wa Katavi amesema kuwa midahalo imekuwa na tija kubwa tangu ianze mwaka jana baina ya waandishi wa habari na jeshi la polisi katika mkoa wa Katavi.

Davidi Mutasya Kamishina Msaidi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi[Kushoto] kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa Habari  Mkoa wa Katavi,Walter Mguluchuma wakisanini maazimio yaliyopitishwa katika mdahalo huo.

’Tangu mwaka jana mwezi wa 11 tumekuwa na midahalo baina ya waamdishi wa habari na Jeshi la polisi kwa lengo la kudumisha uhusiano wa kazi kuptia midahalo hii yote iliyofanyika tumejiwekea maazimio mbalimbali ya utendaji kazi kati ya Polisi na waandishi wa habari’’-Mutasya

Amebainisha kuwa kupitia midahalo hiyo kumekuwa na utamaduni wa kubadilioshana habari baina ya waandishi wa habari na Jeshi la Polisi kwa lengo la kuendelea kuimarisha ulinzi kwa wananchi kupitia taarifa.

Walter Mguluchuma Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Katavi ameushukuru Umoja wa Klabu za waandishi wa habari Tanzania UTPC kwa kuona umuhimu wa kuwezesha midahalo hiyo kufanyika baina ya waandishi wa Habari na Jeshi la polisi.

Mguluchuma ametoa wito kwa waandishi wa habari mkoa wa Katavi kufanya kazi zao kwa kuzingatia weledi wa taaluma zao ili kuepusha migongano isiyokuwa ya lazima katika majukumu yao.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages