Baadhi ya Tumbaku zilizochomwa kwenye Kijiji cha Mtambo Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi. |
Na Walter Mguluchuma-Mpanda
Wakulima wa Tumbaku wa Kijiji
cha Mtambo Wilaya ya
Mpanda wamechomewa zaidi ya Ekari za
15 za Tumbaku zenye thamani ya zaidi ya
shilingi Milioni 40 zilizokuwa zimekaushwa
na nyingine zilizokuwa
shambani kitendo hicho kinadaiwa kufanywa na Askari wa wakala wa Misitu [TFS]
Moja ya Bani la kukaushia Tumbaku lililochomwa huku wakulima wakiwa hawaelewi tumbaku yao watakaushia wapi
Wakulima wa Tumbaku wa Kijiji cha Mtambo Wilaya ya Mpanda wamechomewa zaidi ya Ekari za 15 za Tumbaku zenye thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 40 zilizokuwa zimekaushwa na nyingine zilizokuwa shambani kitendo hicho kinadaiwa kufanywa na Askari wa wakala wa Misitu [TFS]
Tukio la kinyama na
la kikatili limetokea hapo
tarehe 23 mwezi huu
huko katika eneo
la Kijiji cha
Mtambo Halmashauri ya Nsimbo
Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi .
Paul luhanja mmoja wa wahanga wa
kuchomewa tumbaku yake na
mabani matatu ya kukaushia
tumbaku amesema yeye
alikuwa amelima ekari sita za zao
la Tumbaku na
kati ya ekari hizo ekali nne
zikuwa zimevunwa tayari
tumbaku na zilikuwa stoo zikisubiri soko hata hivyo hakuweza kuokoa chochote kile kwani zote ziliteketezwa kwa moto .
Janeth Jailos mmoja ya wakulima walioathirika baada ya Tumbaku yake kuchomwa Moto |
Amesema mbali ya kuchoma tumbaku yake iliyokuwa kwenye stoo askari hao ambao idadi yao ilikuwa sita na walikuwa na silaha mbili bunduki waliweza kuchoma pia Tumbaku nyingine ambazo zilikuwa bado zipo kwenye mianzi ya kukaushia tumbaku na kuzichoma.
Kati ya bani zake
alizokuwa nazo za kukaushia
tumbaku waliweza kumchomea bani tatu zenye tumbaku na bani mbili waliziacha kwa kuwa hazikuwa na
tumbaku na walipokuwa wanawachomea
walikuwa wakiwatolea maneno ya kuwatisha
na kuwaambia pia ngoja wapate hasara .
Amesema kila alipokuwa akijaribu kuwasihi waache kuchoma tumbaku hiyo walikuwa wakimuongezea kichapo
kwa kupigwa fimbo kwenye sehemu mbalimbali za mwili wake licha ya kuchomewa
tumbaku yake waliweza pia kumchome sola yake ya umeme wa jua na waliweza chukua
kiasi cha tshs 58,5000 ambazo zilikuwa
kwenye nguo.
Nae Silivanus Kaponela mkulima mwingine aliyachomewa tumbaku yake siku hiyo
amesema yeye alikuwa yupo shambani kwake na mkewe wanavuna tumbaku na ghafla
aliona askari wanashuka kwenye
pikipiki zao na ndipo waliposhuka na kuanza kuchoma tumbaku
zao
Mwenyekiti wa bodi ya Ivungwe Amcos Nikilias Nicolaus
almeeleza kuwa yeye
tukio la kuchomewa wakulima wake alilipata siki
hiyo hiyo ya tukio na alijulishwa kuwa
kati ya zaidi
ya ekari 15 zilizochomwa ekari zaidi ya 11 zilikuwa za wakulima wa
Amcos yake na ekari nne zilikuwa za
wakulima wa Katumba Amcos .
Amesema imekuwa ni ajabu kuona tumbaku inaadhibiwa
wakati wenye mashamba hayo wapo na wamekuwa wakilima hapo kwa muda
mrefu na athari ilitotokea ni kubwa kwa wakulima wake
ambao kwa kiasi cha wakulima wa Amcos ya
Ivungwe wamepoteza zaidi ya dolla 20,000 na pia
Amcos nayo imekosa mapato ya
Serikali kwa kuchomwa tumbaku hiyo .
Hamadi Juma mmoja ya Mkulima aliechomewa Tumbaku yake kwenye Shambani kwake |
Amebainisha kuwa toka
amekuwa mwenyekiti hawajawahi kuambiwa eneo
hilo kuwa ni eneo la hifadhi
isipokuwa imekuwa tuu ikitokea matukio
ya kupigwa kwa wananchi na askari
wa Maliasili .