Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akielezea Mafanikio ya Miaka 3 kwa Mkoa wa Katavi Chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan |
Na Walter Mguluchuma-Katavi
Mkoa wa Katavi umenufaika na Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake kwa kupokea zaidi ya shilingi Tilioni 1.2 kwa ajiri ya utekelezaji wa miradi mbambali ya maendeleo na kutatua changamoto kwa wananchi .
Mkoa wa Katavi umenufaika na Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake kwa kupokea zaidi ya shilingi Tilioni 1.2 kwa ajiri ya utekelezaji wa miradi mbambali ya maendeleo na kutatua changamoto kwa wananchi .Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akiwa katika kongamano hilo la kuelezea Mafanikio ya serikali ya Awamu ya Sita kwa Mkoa wa Katavi.
Amebainisha kuwa Mkoa wa Katavi ulipoanzishwa mwaka 2012 haijawahi kupatapa fedha nyingi ambazo zimetekeleza zimesaidia kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kama vile Barabara ,Maji Afya Elimu na ujenzi wa Bandari .
Amesema Mkoa wa Katavi huwezi kulinganisha na ile ya miaka ya nyuma ni sawa na kulinganisha usingizi na kifo kwani kwenye kifo hakuna kuamka kwani Mkoa huu kwa sasa umeamka unasonga mbele kwa maendeleo makubwa kwasababu ya Serikali inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan .
Mrindoko amesema Rais ameweza kuwaletea fedha nyingi zaidi ya Tilioni 1.246 kwa ajiri ya kutatua kero mbalimbali kwa ajiri ya kuongeza upatikanaji wa huduma za jamii na kuongeza miundo mbinu mbalimbali katika kuhakikisha uchumi wa Mkoa wa Katavi na Taifa unaendelea kukua .
Kiasi hicho cha fedha zilizoletwa zimeenda kwenye sekta mbambali kama Ofisi ya utawala ya Mkoa , Halmashauri zote tano za Mkoa huu , Mawasiliano Tanesco , Tanroads , Ruwasa ,Muwasa Tarura , ujenzi wa Bandari ya Karema , Miradi ya umwagiliaji, Misitu , Tasaf fedha zilizopelekwa kwenye miradi hiyo ziweeza kufikia kiasi cha tshs Tilioni 1.246.
Amesema wameweza kujenga shule mpya 28 ambazo hazikuwepo tangu Mkoa ulipoanza ambazo zimejengwa katika kipindi hiki cha miaka mitatu ambazo hazikuwepo kati ya shule hizo za Sekondari ni 12 na shule za Msingi ni 16 ambazo hazikuwepo kabisa kati ya shule hizo moja ni shule maalumu ya wasichana iliyogharimu kiasi cha zaidi ya shilingi Bilioni 3 ambapo shule zote hizo zimeisha anza kutoa huduma .
Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu akielezea mafanikio yaliyopatikana katika Wilaya ya Tanganyika chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan
Kuhusu Afya amesema umbali kwa
kwenda kupata huduma za afya kwa wanachi umepungua sana na
gharama za kwenda kutafuta matibabu kwenye Hospitali za Rufaa
umepungua baada ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi kuanza
kutowa huduma.
Mrindoko amesema kwa sasa wananchi wa Mkoa
huu wanapata huduma za kibingwa hapa hapa kwenye Hospitali
ya Rufaa ya Mkoa kwa maana hiyo Rais Dkt Samia
amewahakikisia wananchi uwepo wa afya bora kwa kupata tiba
kamili za kibingwa hapa hapa .
Amefafanua kuwa kuna zaidi ya vituo 20 vya afya zimejengwa katika kipindi hiki na zahanati 36 hivyo hivyo yapo magari kumi na sita ya kubeba wagonjwa na kama kunakuwepo na changamoto yoyote ya mgonjwa magari hayo yamekuwa yakiwafikisha kwenye maeneo husika na kuweza kuokoa uhao wa watu .
Kuhusu upatikanaji wa maji vijijini kwa sasa upatikanaji wa maji kwenye Mkoa huu ni asilimia 73.7 hali ambayo imesaidia kupunguza tatizo kabisa la ugonjwa wa milipuko kama vile kipindupindu hasa katika Wilaya ya Tanganyika ambako mara nyingi kulikuwa kunatokea mlipuko wa ugonjwa huo na upatikanaji wa maji mjini ni asilimia 60.
Ameeleza kuwa kwa mara ya kwanza Mkoa huu unatarajia kuanza kutumia umeme wa gridi ya Taifa kuanzia mwishoni mwa mwezi june mwaka huu ambapo kwa sasa wanatumia umeme wa jenereta hali ambayo ilikuwa ikiathiri shughuli nyingi za kiuchumi .
Meya Mstaafu wa Manispaa ya Mpanda ambae ni Diwani wa Kata ya Majengo Willy Mbogo amesema kuwa zamani swala la mtoto kufaulu shule ya Msingi na kwenda Sekondari lilkuwa ni jambo geni kutokana na uchache wa shule za sekondari .
Mkuu wa Wilaya ya Mlele Majid Mwanga akieleza mafanikio yaliyopatikana kwenye Wilaya hiyo katika kipindi cha Miaka 3 ya Rais Samia Suluhu Hassan |
Godfrey Sadala mkazi
wa Manispaa ya Mpanda amesema kuwa hali ya miundombinu ya
barabara kwa pindi hiki cha miaka mitatu imeboreshwa sana kwani barabara za kutoka na kuingia zinapitika kwa muda wote
na sasa hivi wananchi wanasafiri na kufika
Dares salaam kwa siku hiyo hiyo tofauti na hapo nyuma walikuwa
wanatumia siku tatu .