MAHAKAMA YAAMURU MWILI WA MAREHEMU MUISLAMU KUFUKULIWA BAADA YA KUZIKWA KIKIRISTO

Jengo la Mahakama ya Wilaya ya Mpanda ambapo amli imetolewa kwa Mwili wa Marehemu kufukuliwa na kuzikwa upya

 Na Walter Mguluchuma-Mpanda

Mahakama ya Wilaya ya  Mpanda  Mkoa wa  Katavi  imeamuru  mwili wa Marehemu  aliyefakamika  kwa majina ya  Juma  Andrea Bukuku uliokuwa umezikwa  katika Makuburi ya    Kashaulili Manispaa ya Mpanda   ufukuliwe na kuzikwa  upya  baada ya    mke wa marehemu kufungua kesi akidai  marehemu mume wake alizikwa kwa  imani ya Dini ya  Kikiristu badala ya  dini ya  Kiisilamu.

Mke wa Marehemu aliyefungua Shauri hilo akiwa anatoka Mahakamani baada ya hukumu hiyo kutolewa mahakamani hapo

Mahakama ya Wilaya ya  Mpanda  Mkoa wa  Katavi  imeamuru  mwili wa Marehemu  aliyefakamika  kwa majina ya  Juma  Andrea Bukuku uliokuwa umezikwa  katika Makuburi ya    Kashaulili Manispaa ya Mpanda   ufukuliwe na kuzikwa  upya  baada ya    mke wa marehemu kufungua kesi akidai  marehemu mume wake alizikwa kwa  imani ya Dini ya  Kikiristu badala ya  dini ya  Kiisilamu.

Hukumu  hiyo iliiyovuta  hisia za watu  wengi wa    Mji wa Manispaa ya  Mpanda  na Mkoa wa   Katavi  imetolewa   na  Hakimu  Mkazi   Mfawidhi wa  Mahakama ya Wilaya ya  Mpanda  Mh  Gospher  Luoga  baada ya    Mahakama kuridhika  na ushaidi  uliotolewa   Mahakamani hapo  na  upande  wa     mdai    na upande wa mdaiwa

Katika  kesi hiyo   mdai  aitwaye  Rehema  Saidi  ambae  ni    mke wa   marehemu alikuwa  akitetewa na  Wakili    Hamad  Arfi na   mdaiwa  ambae  ni  baba wa marehemu  anaitwa  Andrea  Bukuku  alikuwa akitetewa  Mahakamani hapo na Wakili  Patrick  Mwakyusa

Kesi hiyo  ilifunguliwa  mahakamani  hapo  kwa mujibu wa kifungu  cha  sheria   Namba  95 sura ya 33 ya mwaka 2019 na kifungu   namba 9 ya  Sheria ya  uchunguzi wa     maiti  ambapo  Reremu  alifungua  kesi ya  kudai mwili  wa marehemu   mume wake  Juma  Andrea  Bukuku  ulizikwa   kaburini  ufukuliwe  na  uzikwe  upya  baaada ya kuzikwa  kwa  imani ya diniya  kikiristo  badala ya dini ya  kisramu

Baadhi ya waumini wa Dini ya Kiislamu wakitoka nje ya Mahakama baada ya uamuzi huo kutolewa 

Wakili wa   mdai   Hamad  Arfi   alidai mahakamani hapo kuwa  mwili wa  marehemu huyo  unapaswa  ufukuliwe  na kuzikwa kwa upya kwa kuwa marehemu alizikwa  nje ya  imani yake  ya dini  kwani    kabla ya  kifo chake  kilichotokana  na  kugongwa na gari  marehemu  alifunga ndoa   mwaka 2018 na  mkewe  Rehema  ya kisiramu huko  huko  Kigoma

Alidai kuwa  Rehewa  na  mumewe waliendelea  kukaa  pampja  na  marehemu huyo  hadi  mwaka  2022 ndipo walipotengana    na licha ya kutengana waliendelea kuwa na mahusiano nae ya karibu kwa kuwa alikuwa amezaa nae  mtoto na pia alikuwa  haja mpa  talala.

Hivyo  alidai kuwa marehemu alifariki  Aprili 15  mwaka huu na kuzikwa   Aprili  17  kinyume  na  mafunzo  ya Dini  ya kisiislamu   yanavyoelekeza  kwa hiyo waliomba Mahakama  kutoa   kibali cha  mwili wa  marehemu huyo ufukuliwe  na  kuzikwa upya  kwa imani ya dini  yake .

Madai hayo  yalipingwa  na  Wakili  wa  Baba wa  Marehemu  Wakili  Patrick Mwakyusa  alidai kuwa  wao  wanao  wanafahamu      Jina  la  Marehemu ni   Lwitiko Andrea  Bukuku    na sio   Juma  Bukuku   ni     mkiristu  na alibatizwa  katika  Kanisa  la Moroviani  .
Wakili  Mwakyusa  ameimbia Mahakama  kuwa kwa  maana hiyo  Juma   Bukuku  na Lwitiko Bukuku  ni  watu wawili tofauti  kwani marehemu    wao ka mujibu wa   nyaraka walizo nazo zinaonyesha kuwa ni  mkiristo .

Hakimu   Mkazi      Mfawidhi wa  Mahaka ya  Wilaya  Mpanda    Mh Gospher  Luoaga wakati akisoma  hukumu hiyo   aliiambia Mahakama kuwa  marehemu   baada ya kuwa  mtu  mzima   alifunga  ndoa ya  kiisilamu.

Kwa    hali hiyo  mahakama imejiridhisha kuwa  wakati wa marehemu  anafunga ndoa huko  Kigoma  ndipo  alipobadilisha jina  na kuitwa  Juma   Andrea  Bukuku na kuhamia kwenye  dini  nyingine  ya kisramu

Kutokana  na   umri ambao   tayari  alikuwa amefikia   ilikuwa  sio  lazima  kwenye  maamuzi yake ya kubadili dini amshililishe  mtu  mwingine   kwenye  maamuzi yake yalikuwa ni yake  mwenyewe kwa kuwa alikuwa amekuwa mtu mzima .

Hivyo  alisema   kutokana  na ushahidi wa pande hizo mbili  mahakamu  inatowa hukumu ya mwili wa marehemu kufukuliwa na kuzikwa  upya wa imani ya dini ya kisramu  na  kwenye ufukuaji huo wa mwili wa marehemu kuwepo na usimamizi wa karibu wa jeshi la polisi na maafisa wa afya

Mara baada ya  hukumu  hiyo  Wakili   Mwakyusa  alisema atakata rufaa ya kuomba mwili huo  wa  marehemu kufukuliwa na kuzikwa upya .
Wakili  Hamadi  Arfi  alisema  ameridhishwa  na  hukumu  iliyotolewa  kwani imezingatia sheria kwa kutambua marehemu alikuwa amezikwa kwa imani ya dini   nyingine.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages