TCCIA KATAVI WALALAMIKIA WAKULIMA KUUZIWA MBOLEA YA RUZUKU KWA BEI YA JUU

Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Katavi Shabili Dallah akizungumnza katika kikoa hicho

 Na Walter Mguluchuma-Katavi


Chemba ya wafanya  biashara Mkoa wa  Katavi (TCCIA)wamelalamikia  baadhi ya wakulima wa Mkoa huu kuuziwa  mbolea  ambayo  mifuko yake ya kuhifadhia mbolea hiyo imeandikwa Ruzuku wakati wakulima hao  wanauziwa  mbolea hiyo kwa bei  ya juu  ambayo sio ya bei ya Ruzuku .
Chemba ya wafanya  biashara Mkoa wa  Katavi (TCCIA)wamelalamikia  baadhi ya wakulima wa Mkoa huu kuuziwa  mbolea  ambayo  mifuko yake ya kuhifadhia mbolea hiyo imeandikwa Ruzuku wakati wakulima hao  wanauziwa  mbolea hiyo kwa bei  ya juu  ambayo sio ya bei ya Ruzuku .

Malalamiko hayo yametolewa na  Mwenyekiti wa  Chemba ya    biashara , viwanda na  Kilimo Tanzania   Mkoa wa  Katav (TCCIA)i  Shabili  Hassanal  Dallah   mbele ya     Rais  wa  TCCAIA  Tanzania  wakati wa kikao  na  wafanya  biashara  wa Mkoa huu kilichofanyika  katika ukumbi wa  Manispaa ya  Mpanda .

Amebainisha kuwa  kumekuwepo  na  changamoto mbalimbali   za wakulima  katika Mkoa wa Katavi moja  ya  changamoto  hizo ni  mbolea ya   ruzuku  iliyoletwa  katika  mkoa huu zilikuwa  ni za  ruzuku  ambazo  bado bei ilikuwa ni ile ile ya juu.
Amesema wakulima wameshindwa kuelewa  kwa kuuziwa  mbolea  ambayo kwenye mfuko imeandikwa  ni ya  ruzuku  rakini   wameweza kuuziwa  mfuko   mmoja  kwa gharama  ya tshs 150,000 hivyo wameshindwa kufahamu ni kwanini  mbolea iandikwe kwenye mfuko kuwa ni ya ruzuku halafu  wameuziwa kwa bei hiyo .

Amedai kuwa hata  baadhi ya mbolea  iliyoingia  kwenye  Mkoa huu  haikuwa na ubora  hali  ambayo imesababisha  baadhi ya wakulima kuweza kupata  hasara  kutokana na borea hiyo kutokuwa na ubora  unaositahili 

Rais  wa TCCIA  Tanzania   Vicent  Minja  amesema  changamoto   hiyo  ya  mbolea   ya  ruzuku kuuzwa  kwa  bei ya juu na mbolea nyingine kutokuwa na ubora amesema kuwa  ni kweli kumekuwepo na  malalamiko ya wakulima  kutumia mbolea  na  kupata  kitu ambacho wakutegemea kukipata .

Ametowa  mfano   kwenye mbegu za  alizeti  huko  Singida  wenye  viwanda  mwaka jana wameshindwa kuzalisha  mafuta ya  alizeti  kwasababu  mwaka  jana wakulima walipelekewa mbegu ambazo  azikuwa sahihi  wakulima walilima na kupanda  lakini haikuota   na hata  kwa wale iliota  haikuweza kuzaa sawa sawa.
Minja  amefafanua kuwa kwa hali hiyo ya mbolea ni changamoto ambayo ipo Kitaifa   na wao  TCCIA  wanalijua  na wamepanga kulikisha  kwenye  Wizara ya kilimo kwa ajiri ya hatua zaidi .

Kuhusu  masoko ya  mazao hasa  mahindi  na  mpunga  amesema   Waziri wa  Kilimo  Hussen  Bashe  alipoteuliwa  kuongoza wizara ya kilimo  alisema     mkulima  amelima  mwenyewe  mazao yake  wanaruhusiwa kuuza  sehemu yoyote wanako taka kuuza  lakini baada ya muda  mfupi  alisimamisha tena mahindi kuuzwa  nje .

Hali hiyo ya kuzuia  mahindi yasitoke nje  imesababisha   gunia  moja la mahindi lililokuwa likiuzwa  kwa bei ya tshs 110,000 sasa  hivi linauzwa kwa bei ya tshs 30,000 wamepigiwa simu na wakulima wengi sana wanamagunia wengine  kwenye maghala yao mpaka elfu kumi  na  sasa  hivi msimu wa  mavuno umeingia huku  maghala yakiwa yamejaa mahindi
Amesema hali hiyo inaweza kufanya wafanya biashara na wakulima waweze kufilisika  kwa hali hiyo TCCIA  ngazi ya Taifa wanalifanyia kazi  kwa kuwa jambo hilo wanalifahamu   na halipo  katika  Mkoa wa Katavi tuu.

Nae  mkulima  Doto  Sivester amesema  yeye ni mkulima wa zao la tumbaku ambapo mbolea  mfuko mmoja wameuziwa  msimu huu kwa dola 63 na wameambiwa ni ya ruzuku sasa wanashindwa  kuelewa bei  hiyo kama  na ruzuku ipo kwa mkulima kutokana na bei hiyo

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages