MGONJWA ASAFIRISHWA NA GARI LA WAZI LA PADRI UMBALI WA KILOMITA 112 KWA KUOSA GARI LA WAGONJWA

Mgojwa akiwa akisafirishwa katika gari la wazi kutoka Kata ya Karema hadi Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi kwa kutumia Gari la Kanisa Katoriki.

Na Walter Mguluchuma-Katavi

Katika  hali isiyo ya  kawaida  gari aina ya  Pikapu  likiwa wazi  la Parokia ya Karema limetumiwa kumsafirisha   mgonjwa  aitwaye  Peter  Lungu umbali wa kilometa 112 kutoka kituo cha Afya cha Karema  alikokua  amelazwa  hadi  katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi baada ya kituo hicho kukuwepo kwa gari la kubebea wagonjwa .

Mgojwa huyo akiwa amefikishwa hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi baada ya Safari ya muda kutoka Karema 

Katika  hali isiyo ya  kawaida  gari aina ya  Pikapu  likiwa wazi  la Parokia ya Karema limetumiwa kumsafirisha   mgonjwa  aitwaye  Peter  Lungu umbali wa kilometa 112 kutoka kituo cha Afya cha Karema  alikokua  amelazwa  hadi  katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi baada ya kituo hicho kukuwepo kwa gari la kubebea wagonjwa

Gari hilo  la pikapu  lililombeba  mgonjwa huyo  ilikuwa  na  namba za  usajiri  T  176 BGU mali ya  Kanisa  Katoliki  Jimbo la Mpanda  lillilokuwa   likiendeshwa na  Padri  Emili Sibomana paroko  msaidizi wa   parokia ya Karema

 .
Akizungumza kwa masikitiko makubwa    mke wa  mgonjwa  huyo   Eliza  Apolonali   ambae alikuwa  amemsindikia  mume wake  hadi kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa  wakiwa wanatokea kwenye  kituo cha  afya  Karema walikokuwa wakipatiwa matibabu .

Amesema  mume wake  alikuwa amelazwa  kwenye kituo cha  Afya cha Karema kwa  muda wa siku mbili   kwa tatizo la  ugonjwa wa shikizo la  damu (BP)kutokana na hali yake kuendelea kutokuwa  nzuri siku ya   jumanne  tarehe  10  makaktari  wa kituo cha  afya Karema walitowa rufaa ya  mgonjwa huyo  kwenda kutibiwa katika  hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa  Katavi .
Amebainisha kuwa  baada ya kuwa wamepewa rufaa hiyo waliendelea kusubiria  kupatiwa gari la kubeba wagonjwa ambalo halikuwepo kituoni hapo  pasipokuwa na mafaniko yoyote yale  licha ya mgonjwa wao   hali yake kuendelea kuwa kuwa mbaya 

Kutokana hali ya  mgonjwa kuendelea kutokuwa  nzuri  siku iliyofuata walipata wazo la kwenda   kwenye  Parokia ya  Kanisa  Katoliki ya  Karema kwenda kuomba   msaadawa usafiri ili waweze  kuokoa uhai wa ndugu yao.

Eiza ameeleza kuwa  baada ya kufika  parokiani Karema  walimkuta    Paroko   msaidi  Padri  Emili Sibomana  paroko wa  parokia  wa parokia  hiyo  Padri  Nicodemo Kiyumana  alikuwa yupo  safari hata hivyo   paroko msaidizi  alikubali kuwapatia  msaada wa  gari la Kanisa hilo aina ya pikapu la azi

Nae  Padri  Sibomana  amesema    ndugu wa mgonjwa huyo walifika   parokiani kwake   majira ya saa  tano asubuhi  na  baada ya kusikiliza  shida waliokuwa nayo ya usafiri alilazimika kutowa     gari  Kanisa aina ya pikapu  licha ya kuwa gari hilo sio  maalumu la kubebea mgonjwa  lakini  alilazika kutowa msaada huo .

Ameeleza  ilipofika saa tano  na nusu  aliweza  kufika  kwenye kituo hicho cha  afya  Karema na waliweza  kumpakia   mgonjwa  huyo na kulaza   kwenye  bodi ya  gari  ambalo aliweka godoro  na  kisha walianza  safari ya  kumsafirisha  mgonjwa  kumpeleka  katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa huku wakiwa wameambatana na dakitari  mmoja wa kituo hicho 

.Kutokana na kipindi hiki  cha  masika kuwa na mvua  huku  gari hiyo ikiwa ipo wazi  aliona safari hiyo kuwa  ilikuwa ni ngumu sana   hali  ambayo ilkuwa ikimlazimu alipokuwa njiani  akikutata wingu la  mvua kusimamisha  gari alikuwa akiendesha  na kuanza kusali kumwomba Mungu  awasaidie   ili  mvua  isimnyeshee    ili  aweze kumfikisha  salama  hospitalini mgonjwa huyo

Padri  Sibomana  amesema  kutokana hali  hiyo    safari ya kumfikisha  mgonjwa  ilichukua muda  mrefu   waliweza kutumia zaidi ya   saa   sita  hadi kufika  kwenye  Hospitali ya  Rufaa ya  Mkoa waliweza kufika  majira ya saa kumi na moja na nusu jioni

Nao  baadhi ya watumishi wa kituo hicho waliongea  na  Jamhuri kwa nyakati tofauti  kutotaka kutajwa kwa majina yao wamesema  kituo hicho cha   Afya  Karema  kinahudumia wagonjwa wanaokuwa wamepewa  rufaa kutoka  kwenye  Zahanati  sita  zilizopo  kwenye  Tarafa   hiyo ilipo  mwambao mwa ziwa Tanganyika  inayopakana  na  Nchi ya   DRC.

Wamebainisha kuwa  kituo hicho kimekuwa  na changamoto kubwa ya kutokuwapo kituo hapo na  gari la  kubebea wagonjwa licha ya Serikali  kutowa  gari kwa ajiri ya kubebea wagonjwa   gari la kituo hicho limekuwa halikai kwenye kituo    cha  Afya na  badala yake linakaa   Majalila  yalipo makao makuu ya Wilaya  umbali wa zaidi ya kilometa 130.

Wamesema kutokana na  gari  la kituo hicho  kuwa mbali na  kituo mgonjwa  anapokuwa amepewa rufaa      huwa wanalazimika kutuma  taarifa yalipo  makao makuu Halmashauri yao  kwa ajiri ya kumchukua  mgonjwa  alipewa rufaa .

Wamebainisha hata  hivyo mara  nyingi gari limekuwa  halifiki kituoni hapo kwa wakati   unaweza ukaomba gari  leo  saa  nane  mchana      gari linafika kesho yake saa mbili au saa tatu asubuhi  matokeo yake   ya kuchelewa kuwasafirisha wagonjwa kumekuwa kukisababisha  baadhi ya wagonjwa  kupoteza uhai wakiwa  njiani na wengine kufikishwa  hospitalini wakiwa wamechoka .

Wamedai kuwa kumekuwapo na tabia ya kutoa  kipaumbele zaidi  cha kuwasafirisha wajawazito  pindi wanapokuwa wameomba  usafiri wa gari la wagonjwa  kuliko wagonjwa wengine  kwani kunawakati wamekuwa wakiambiwa gari la wagonjwa  halina mafuta .

wamesema watu wamekuwa wakipata changamoto ya kuwasafirisha kwa boda boda wagonjwa kutoka  kwenye  zahanati kuwapeleka  kwenye kituo cha  afya  Karema kutokana na gari la kituo hicho cha Afya  kutuwepo

Mbunge wa  Jimbo  la  Mpanda  Vijijini  Wilaya ya  Tanganyika  Moshi Kakoso amekiri kuwepo  kwa changamoto  ya gari la kubebea wagonjwa kwenye kituo hicho cha  afya kilichoko mwambao mwa Ziwa Tanganyika 

Amesema kuwa   Halmashauri ya  Tanganyika inavituo vya  Afya  vitatu  ambapo  magari ya kubebea wagonjwa yapo  mawili tuu hivyo kulingana na jografia ya Wilaya hiyo ndio maana  magari   yanalazimika  kukaa kwenye  Makao makuu ya  Wilaya yaliko    katika Mji wa  Majalila


Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages