WAZIRI BASHUNGWA AAGIZA KAMPUNI YA CRSG ISIPEWE UJENZI WA BARABARA MPYA.

Waziri wa Ujenzi Innocent Bashugwa akitoa maelekezo kwa Mkandarasi anaejenga Barabara ya Kibaoni Sitalike Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi


 Na Walter Mguluchuma-Katavi

Waziri wa Ujenzi  Innocent Bashungwa  amemwangiza  Mtendaji  Mkuu wa TANROADS   Tanzania   kutoipatia  mkataba wowote wa kutengeneza  Barabara mpya hapa  nchini   kampuni  ya kichina ya CHINA RAILWAYS SEVENTH GROUP COMPANY LIMITED [CRPSG] mpaka hapo kampuni hiyo itakapo kuwa imekamilisha miradi iliyonayo kwa sasa kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini.

Kaimu Mtendaji Mkuu w Tanroads Tanzania Doroth Mtenga akisoma taarifa ya Mwenendo wa ujenzi wa Barabara ya Sitalike Kibaoni kilomita 50 mbele ya Waziri wa Ujenzi Innocent Bashugwa alipotembelea Mradi huo.

Waziri wa Ujenzi  Innocent Bashungwa  amemwangiza  Mtendaji  Mkuu wa TANROADS   Tanzania   kutoipatia  mkataba wowote wa kutengeneza  Barabara mpya hapa  nchini   kampuni  ya kichina ya CHINA RAILWAYS SEVENTH GROUP COMPANY LIMITED [CRPSG] mpaka hapo kampuni hiyo itakapo kuwa imekamilisha miradi iliyonayo kwa sasa kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini.

 Maagizo hayo  ameyatoa  baada ya kukagua barabara inayojengwa na  Kampuni  hiyo kwa kiwango cha lamikutoka   Kibaoni  hadi  Sitalike  yenye  urefu wa kilometa  50 ambayo   ujenzi wake  unasusua   umefikia asilimia  `14.7 na upo  nyuma kwa asilimia  23.71.

Mkuu wa Wilaya ya Mlele Majid Mwanga akimwelezea Waziri wa Ujenzi Innocent Bashugwa umuhimu wa Barabara ya hiyo kwenyw Wilaya ya Mlele

Bashugwa  amekagua   barabara  hiyo  na hajaridhishwa   na kasi ya kampuni hiyo ya Kichina ambayo imekuwa ikisusua   kwenye miradi mingine  hapa  nchini   ambayo wanaitekeleza .

Kufuatia hali hiyo Waziri Bashugwa amemwagiza  Mtendaji  Mkuu wa Tanroads Tanzania kutoipatia kazi  kampuni hiyo mpaka itakapokuwa imekamilisha miradi yake ambayo imepewa na  Serikali kwenye maeneo mengine hapa nchini.

Meneja wa Mradi wa Barabara ya Kibaoni Sitalike wa Kampuni hiyo ya Kichina [CRSG ]akiwa na Mhandisi Mshauri Ramdhani Mnyanzi msimamizi wa mradi[ CTC] wa kwanza ambae waziri ameagiza mshauri huyo kuomdolewa kusimamia mradi huo.

Ameeleza kuwa mpaka  sasa kuna miradi mitano wanayoitekeleza hapa mchini huku wakitekeleza miradi hiyo kwa kusuasua.

Aidha  Bashungwa amepata  mashaka  kwa kuwepo na mitambo mingi  ikiwepo   magari   yanayotumiwa na  mkandarasi huyo kuwa   ni  mabovu   hivyo amemwagiza Katibu  Mkuu wa Wizara ya  ujenzi  kupeleka timu ya wataalamu kwenye mradi huo   kuikagua ili kuweza kufahamu mangapi yanafanya kazi  pamoja na kuchukua hatua kimkataba  kwa mwandisi  mshauri .

Amebainisha kuwa  Serikali imeendelea kuboresha  miundo  mbinu ya Barabara katika Mkoa wa Katavi  inayounganisha   Mkoa huu na mikoa mingine  kama vile barabara ya lami Mpanda  Vikonge kwenda Kigoma km 37 inafanya kazi  Vikonge  Luhafe   km 25 ujenzi wake upo asilimia  57.4.

Amezitaja  Barabara  nyingine kuwa ni  Luhafe Mishamo   pamoja na  barabara inayoelekea   Bandari ya  Karema  kuanzia  Kagwira  yenye  urefu wa kilimota  zaidi ya 112  mkandarasi wake ameisha   patikana na   Serikali  ipo  kwenye hatua za mwisho za  kumkabidhi  Barabara  mkandarasi iliaweze kuanza   kazi .

Diwani wa Kata ya Kibaoni Victor Kabanga akimuomba waziri wa Ujenzi Innocent Bashugwa jitihada zifanyike kukamilisha Barabara hiyo kwa wakati.

Kaimu Mtendaji Mkuu waTanroads  Mhandisi   Doroth   Mtenga  amesema kuwa ujenzi wa Barabara hiyo ya kutoka  Kibaoni  kuelekea  sitalike  unagharimu kiasi cha shilingi   Bilioni  88.725 kutoka  mfuko mkuu wa Serikali  kwa asilimia 100 .

Mhandisi  Mtenga  amefafanua kuwa  mradi huo kuwa  nyuma ni pamoja  utekelezaji wake  kuwa  tofauti ukilinganisha na  mpango kazi wake  na   kuchelewa kuleta wataalamu wake  kwenye  mradi  kama ilivyotakiwa kimkataba .

Awali Mkuu wa  Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko  alimweleza   Waziri Bashungwa  kutoridhishwa  na kasi   ya ujenzi wa  barabara  hiyo  ambayo   inatakiwa  kukamilika  June   2025.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages