WAFANYABIASHARA KATAVI WAHIMIZWA KUJIUNGA NA TCCIA

Rais wa Chemba ya Biashara,Viwanda na Kilimo Tanzania [TCCIA] Vicent Minja akizungumnza na wafanyabiashara wa Mkoa wa Katavi.

Na Walter Mguluchuma-Katavi

Wafanya Biashara Mkoa wa Katavi wameshauriwa  kujiunga  na  TCCIA  ili waweze  kuwa na nguvu ya  pamoja ya kuweza kuungana na nguvu ya pamoja katika  kujadili changamoto zao kwenye Biashara na kuziwasilisha sehemu husika ili ziweze kufanyiwa kazi .

Rais wa TCCIA Taifa akiwa akiendesha kikao cha Wafanyabiashara mkoa wa Katavi akiwa na viongozi wa TCCIA Mkoa wa Katavi na Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi.

Wafanya Biashara Mkoa wa Katavi wameshauriwa  kujiunga  na  TCCIA  ili waweze  kuwa na nguvu ya  pamoja ya kuweza kuungana na nguvu ya pamoja katika  kujadili changamoto zao  kwenye Biashara   na kuziwasilisha sehemu husika ili ziweze kufanyiwa kazi .

Wito huu umetolewa na Rais  wa Chemba  ya  Bishara ,Viwnda  na  Kilimo  Tanzania (TCCIA) Vicent  Minja  wakati  wa kikao  chake na Wafanyabiashara  mbalimbali wa Mkoa wa Katavi  kilichofanyika  katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda kwenye ziara ya siku mbili Mkoani hapa .

Amesema wafanya biashara wa Mkoa wa Katavi hawezi kufanikiwa kwenye kutatua  changamoto zao  kama hawatakuwa wameungana   na kujiunga na TCCIA kwakuwa chombo hicho ndicho chenye mamlaka ya kusikiliza kero zao na kuzipeleka katika ngazi za juu za zenye mamlaka.

Baadhi ya Wafanya biashara walio hudhuria kikao hicho wakimsikiliza Rais wa Chemba ya Wafanyabiashara,Kiwanda na Kilimo Tanzania Vicent Minja.

Amebainisha kuwa Chemba hiyo imeshuka katika ngazi ya Wilaya  na  Mkoa   ili wafanya biashara waungane na kujadili  changamoto zao  na kuzipeleka   Serikalini   ili ziweze kufanyiwa kazi .

Minja amesema wafanyabiashara hao watafanikiwa katika kutatua changamoto zao kwa kuungana kupitia Mwavuli wa [TCCIA] hivyo nilazima kuhakikisha wanatumia umoja huo ili kufanikisha Malengo yao ya Kibiashara.

Amewasisitiza  waweze  kutumia  Chemba ya wafanya biashara ya Katavi kwakuwa serikali hutatua changamoto za wanananchi kwa kuangalia idadi ya wahusika katika jamii husika 

Amesema changamoto kubwa  ambayo ameiona Katavi  watu  hawatumii  vizuri  ofisi ya  Chemba ya Mkoa wa Katavi  kwani  mjasiliamali yoyote anaweza kuwa  mwanachama wa  Chemba  hata kama  ni wakulima  wenye  kikundi  kitendo cha watu  kutojiunga  ndicho kinachowafanya washindwe kusikilizwa changamoto zao .

Ameeleza kutokuwa na  elimu  sahihi  ya  kodi kuna waumiza sana wafanya biashara na hilo  amekuwa akilizungumza yeye  kwenye  mikoa yote anayopita na kuwashauri  chemba za mikoa kuweka wahasibu ambao watakuwa sehemu ya kuwasaidia wafanyabiashara kuhusu Kodi.

Mwenyekiti wa TCCIA  Mkoa wa Katavi  Shabili Hassanal  Dhalla  alisema kumekuwa  na changamoto ya wafanya biashara wa  Mkoa huu  kutoana  umuhimu wa kujiunga na  chemba ya wafanya biashara ila wanapokuwa wamepatwa na changamoto  ndipo wanapoona umuhimu.

Amemwomba  Rais wa TCCIA kutowa  nafasi ya utendeleo kwa  wafanya biashara wa Mkoa wa Katavi  pindi inapokuwa imetokea nafasi ya  kwenda  nje ya  nchi kwa ajiri ya mafunzo  wawe  wanamchukua  hata  mmoja wa kutoka katika Mkoa huu.

Ameoimba Serikali  kufungua mikapa ya kwenda kuuza mazao ya wakulima hasa kwenye   nchi za  Uganda   Kenya   na Kongo  ambako   Mahindi na  mpunga walikuwa wakiiuza huko  kwani kwa sasa  mazao hayo hayana soko  huu na yamejaa kwenye maghara  ya wafanya biashara .

 Mhasibu wa  TCCIA   Mkoa wa  Katavi  Kelvin Mbogo amesema  wanaanzisha dawati maalumu la Kodi  kwa wafanyabiashara  kwa lengo la kuwaelimisha  maswala  mbalimbali   yanahusu kodi  kutokananan na baadhi yao kutokuwa na elimu sahihi ya Kodi.

Judithi  Baraga Mzabuni wa chakula  katika  Mkoa huu  amesema wao wamewekwa  kwenye VAT  wakati manunuzi yao   karibu  asilimia 90  hayakatwi lisiti  za  mashine ya  EFD matokeo yake wamekuwa  wakilipa VAT asilia 18 kwa  hela  nyingine  za  mfukoni mwao .

Ameeleza Changamoto ya kutolipwa  kwa wazabuni  madeni yao  kwenye Halmashauri  pindi anapokuwa  amehamishwa  Wakukurugenzi  kwenye  Halmashauri  na  kuja    kwa  wakurugenzi  wapya imekuwa  ni sababu ya wazabuni kutolipwa Fedha zao kwa wakati .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages