RC AMLALAMIKIA MKANDARASI MBELE YA WAZIRI KWA KUTORIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA BARABARA

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akitoa maelezo ya Miradi mbalimbali ya Barabara iliyo chini ya Wizara ya Ujenzi  


Na Walter Mguluchuma-Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amemlalamikia Mkandarasi anaejenga barabara ya Kibaoni sitalike kwa kujenga mradi huo kwa mwendo wa kinyonga hali ambayo inawasabishia usumbufu wananchi wanaotumia barabara hiyo katika shuguli za kiuchumi.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko[Kulia] akitoa taarifa ya miradi ya Barabara inayojengwa katika mkoa wa Katavi mbele ya Waziri wa Ujenzi Innocent Bashugwa[Kushoto]

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amemlalamikia Mkandarasi anaejenga barabara ya Kibaoni sitalike kwa kujenga mradi huo kwa mwendo wa kinyonga hali ambayo inawasabishia usumbufu wananchi wanaotumia barabara hiyo katika shuguli za kiuchumi.

Malalamiko hayo ameyatoa mbele ya Waziri wa Ujenzi Innocent Bashugwa alipofika mkoa wa Katavi katika zaiara ya siku moja ya kujionea kazi zinazotekelezwa zilizo chini ya wizara yake.

Mrindoko amebainisha kuwa Mkandarasi anaejenga Barabara hiyo ya Kibaoni Sitalike yenye Urefu wa Kilomita 50 umekuwa unaenda kwa kusuasusua na kumuomba Waziri kuona namna ili kasi iongezeke na wanananchi wanufaike na mradi huo.

‘’Tunatatizo katika mradi wa Kibaoni sitalike mradi huu hauendi katika kasi iliyokusudiwa na kweli kama mkoa na wananchi wake hatuliziki kabisa na mwenendo wa mradi ule’’-Mwanamvua

Waziri wa Ujenzi Innocent Bashugwa akielezea namna Wizara yake inavyotekeleza ujenzi wa Miradi ya Barabara katika mkoa wa Katavi

Amesema kuwa mradi huo unakipindi cha miaka Miwili sasa lakini bado haujakamilika ukiwa umefikia Asilimia 14.8 hali ambayo kwa nanma moja au nyingine inachelewesha maendeleo ya wananchi wa mkoa wa Katavi kupitia shughuli za kiuchumi kwenye barabara hiyo.

‘’Barabarabara hii ni mhimu sana kwa wananchi wa mkoa wa Katavi kwa sababu halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe ni halmashauri ya kilimo tunatoa mchele mwingi sana kule asilimia 50 ya mavuno ya Mpunga,Alizeti na Mazao mengine yanatoka huko barabahii ni uti wa Mgongo kwa uchumi wa mkoa wetu’’-Mwananvua

Amebainisha kuwa pamoja na juhudi zinazofanywa na serikali za kuhakikisha mkandarasi anatekeleza mradi huo kwa kasi bado mwenendo wa mradi huo umekuwa unaenda kwa mwendo wa konokono.

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi Innocent Bashugwa amesema kuwa kutokana na uwepo wa taarifa za mkandarasi huyo anaejenga Barabara ya Kibaoni Sitalike kuwa na kiwango kisicho lidhisha imemlazimu kufika na kujionea hali hiyo ili kubaini tatizo lililopona hatua ambazo tunaweza kuzichukua.

‘’Hata mimi kwa taarifa nilizonazo barabara hii nimeona nifike mwenyewe nione kama ninaweza nikaleta msukumo mpya wa utendaji, Barabara hii wamekuja viongozi mbalimbali akiwemo Naibu waziri Kasekenya na viongozi wa Chama’’-Bashugwa

Bashugwa ameeleza kuwa katika maeneo mengine ambayo mkandarasi huyo amekuwa akitekeleza miradi ya barabara kumekuwa na kusukumana katika utekelezaji wa majukumu yake kwenye miradi hiyo.

Waziri huyo wa ujenzi amemwakikishia Mkuu wa Mkoa wa Katavi na Wananachi wa Mkoa wa Katavi kwa ujumla kuwa suala hilo amelichukua na anakwenda kulifanyia kazi.

Ujenzi wa Babarabara ya Kibaoni Sitalike yenye Urefu wa Kilomita 50 ilianza kujengwa Rasmi 23/6/2022 huku matalajio ya kukamilika kwa Barabara hiyo ikiwa ni 22/6/2025.

Mradi huo unagharimu kiasi cha shilingi 88,725,676,540 chini ya Mkandarasi China Railways Seventh Group Company limited.

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages