DC MPANDA ATANGAZA VITA KWA WATAKAO BAINIKA KUFANYA UKATILI WA KIJINSIA KWA WATOTO KATIKA JAMII.

 

 

DC MPANDA ATANGAZA VITA KWA WATAKAO BAINIKA KUFANYA UKATILI WA KIJINSIA KWA WATOTO KATIAKA JAMII.

Na Walter Mguluchuma

Mpanda

Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph ametangaza vita ya kuwachukulia hatua kali  kwa mtu yeyote ambae atakae bainika kufanya vitendo vya ukatili wakijinsia kwa watoto wadogo na kwenye jamii wanayo ishi.


     Mkuu wawilaya ya Mpanda Jamila yusuph akizungumza na wana nchi wa eneo la  uchimbaji wa Madini ya Dhahabu  rililopo katika kijiji cha Dilifu kilichopo katika Manispaa ya Mpanda juu ya ukatili wa kijinsia wanao fanyiwa watoto wakiume na wakike kwenye jamii

Onyo hilo amelitoa alipokuwa akiwahutubia wananchi wa eneo la uchimbaji wa Madini ya Dhahabu Katika kijiji cha Dilifu kilichopo katika Manispaa ya Mpanda kufuatia kuwepo kwa baadhi ya matukio ya ukatili wa kijinsia kwenye eneo hilo la uchimbaji wa Madini.

Amesema katika eneo hilo kumekuwepo na matukio ya kubakwa na kulawitiwa kwa watoto wa kiume watoto wa kiume sasa hivi wanapitia mazingira magumu sana hivyo nilazima kuweka nguvu kubwa sana ya kuwalinda watoto wa kiume ili wasifanyiwe vitendo vya ukatili.

Dc Jamila amesisitiza kuwa Serikali ya Wilaya ya Mpanda haiku tayari kuona vitendo hivyo vinatokea na watakao jalibu kufanya ukatili huo hatua kali zitachukuliwa dhidi yao kwasababu nao watoto wa kiume wanao  umuhimu mkubwa kwenye jamii yetu.


    Baadhi ya wananchi walio jitokeza kumsikiliza Mkuu wa wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph kuhusu madhara wanayo yapata watoto wa kike na wakiume katika jamii zao.

Amebainisha kuwa changamoto hizo ni nyingi sana hata kwa watoto wa kike kutokana na tabia ya kuwalazamajumbani  watoto wadogo na ndungu wanao kuwa wamefikia kwa wazazi wao kutokana na huwezo mdogo wa nyumba kuwa na vyumba vi chache na kupelekea watoto wadogo kulazwa chumba kimoja na watu wazima.

Ameeleza kuwa kutokana na mchanganyiko huo wa kuwalaza watoto kwenye chumba kimoja kumekuwa kukisababisha mtu mkubwa kumbaka mdogo ama kaka kumlawiti mdogo wake.

Amewasisitiza wakina mama kuwa na utaratibu wa kutumia muda wao kuwakagua watoto wao wakike na wakiume ili kuweza kubaini kama wamefanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia kwani wameisha baini kwenye baadhi ya maeneo watoto wanafanyiwa vitendo vya ukatili pasipo wazazi wao kujua kutokana na wazazi kutokuwa na muda wa kuzungumza na watoto wao.


    Afisa ustawi wa jamii Manispaa ya Mpanda Agines Bulaganya akitoa wito kwa wazazi na walezi kuwa kalibu na watoto wao kwa kujenga urafiki  ili kubaini madhira magumu wanayo pitia

Amewataka wazazi wa kiume nao kukaa na kuzungumza na watoto wao kwani swaala la ulinzi na usalama kwa mtoto si la serikali peke yake lazima ulinzi uanzie nyumbani kwahiyo watoto wa kiume wana mazingira magumu kama ilivyo kwa watoto wa kike na tusipo walinda watoto wetu sasa hivi tuta tengeneza kizazi cha ajabu.

Afisa ustawi wa jamii Manispaa ya Mpanda Agines Bulaganya amesema watoto wengi wanabakwqa na kulawitiwa kwa sababu wanakuwa hawana sehebu ya kusemea wazazi wawe marafiki wa watoto kwa kuwanao kalibu kwa sababu mzazi ananafasi ya kumfanya mtoto akuwe kwenye maadili mema.


Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages