HOSPITALI YA MKOA WA KATAVI KUANZA KUTOA HUDUMA YA UCHUNGUZI WA SARATANI YA SHINGO YA KIKAZI

  1. Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwananvua Mrindoko[kushoto] akimkabidhi Mashine ya kupima Saratani ya Shingo ya kizazi Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Katavi Dk Frank Elisha iliyotolewa na Shirika la Walter Reed
 NA Walter Mguluchuma-Katavi

Wananchi wa  Mkoa wa Katavi wanaondokana na usumbufu waliokuwa wakiupata   kusafiri kwenda umbali mrefu  kwenda  nje ya Mkoa wa Katavi kwenda  kupatiwa matibabu ya   salatani ya shingo ya   kizazi  baada ya kupatiwa   mashine  ya  upasuaji na kupima Saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawak na Taasisi ya  WALTER  REED yenye  thamani ya zaidi ya  shilingi  Milioni  62.


Wananchi wa  Mkoa wa Katavi wanaondokana na usumbufu waliokuwa wakiupata   kusafiri kwenda umbali mrefu  kwenda  nje ya Mkoa wa Katavi kwenda  kupatiwa matibabu ya   salatani ya shingo ya   kizazi  baada ya kupatiwa   mashine  ya  upasuaji na kupima Saratani ya shingo ya kizazi kwa wanawak na Taasisi ya  WALTER  REED yenye  thamani ya zaidi ya  shilingi  Milioni  62.

Msaada huo  umekabidhiwa  kwa  Mkuu wa  Mkoa wa  Katavi Mwanamvua  Mrindoko na    Jofrey  Ndondole Meneja  Mradi  wa (HJFMRJ) katika  hafla ya  makabidhiano  iliofanyika  katika  eneo  la   Hospitali ya  Rufaa ya  Mkoa wa Katavi .

Akizungumnza baada ya kupokea mashine hiyo iliyotolewa na Taasisi ya Walter Reed Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua mrindoko amesema mashine hiyo itakuwa mkombozi kwa wanawake kuepuka kusafiri umbali muda mrefu kufuata huduma hiyo mikoa ya Jirani.

Meneja mradi wa [HJFMTJ] Jofley Ndondole akitoa neno la shukrani baada ya kukabidhi Mashine ya uchunguzi wa saratani ya Shingo ya Kizazi

Amebainisha kuwa  huduma za afya  katika  Mkoa wa  Katavi   zimeendelea  kuboreshwa siku  hadi siku  na kuwapunguzia  wananchi  adha ya kutembea  umbali  mrefu  kwenda  nje ya  Mkoa  na kutumia  gharama kubwa  kwaajiri ya kwenda  kupatiwa huduma hiyo.

Kwa sasa  Hospitali ya Rufaa ya  Mkoa wa  Katavi  ambayo ni  mpya  imekuwa  ikiendelea  kupata   maboresho ya  hatua kwa hatua     kwa  ajiri ya kuimalisha  huduma  muhimu ya afya  kwa ajiri ya wananchi  kwani  wananchi wanaendelea kupata  huduma za  kawaida    na  za kibingwa

Mrindoko   ameeleza  kuwa   vifaa  hivyo  ni  vifaa  ambavyo  vimekuja  kufanya kazi kubwa ambayo  ilikuwa  haifanyiki hapo  awali  katika  Mkoa wa Katavi  hivyo  wahakikishe wanavitunza  na  kuvitumia kwa kazi  mahususi   ambayo imekusudiwa  na kutoa  huduma  bora kwa akina  mama  ambao watakuwa wanafika  hospitalini  hapo kwa ajiri   ya  matibabu  hayo ya   salatani  ya  shingo  ya  kizazi .

Amewataka wanawake wote wa  Mkoa wa  Katavi  wenye  umri wa kuanzia  miaka 21 kufika  hospitalini hapo  ili  waweze kufanyiwa  utafiti  wa  vipimo  ili  kuweza kubaini  kama  wanatatizo la  salatani ya  shingo ya  kizazi   katika    hatua za  awali  ili waweze kupatiwa  matibabu  kwenye  hospitali  hiyo  hiyo ya  Mkoa wa Katavi  badala ya kwenda  nje ya  Mkoa .

Amewasisitiza  viongozi   wote wa  Mkoa huu  kuwafahamisha wananchi kuwa  sasa  wamepata  vifaa  hivyo  kwa ajiri ya  matibabu ya awali  ya  salatani ya shingo ya  kizazi    na waitumie fursa  hiyo vizuri   kwa wananchi wote  hasa wanawake  kwa ajiri ya kupimwa  na kupatiwa  matibabu .

Kaimu   Mganga  Mkuu   mfawidhi wa Hospitali ya  Rufaa ya  Mkoa wa  Katavi  Dk  Frenk   Elisha   amesema  kuwa  tatizo la  ugonjwa salatani ya shingo ya kizazi kwa  wanawake  katika  Mkoa huu lipo kwani   Hositalini hapo  kila mwezi huwa wanapokea wagonjwa  kati ya 20  hadi  40  na wanaogundulika huwa ni wanawake  watatu  hadi  saba  kwa  mwezi .

Uwepo wa  mashine  hizo  kutasaidia upasuaji utaanza  kufanyika hapa  hapa  Katavi   badala  ya  wagonjwa  kwenda  nje ya  Mkoa   na  utawaokoa  sana wanawake wa Mkoa  huu..

Dk  Elisha  ameishukuru  Serikali  kwa  kuwaza kuwatafutia  wadau  ambao wamweza kuwaletea mashine hizo   ambazo   hapa  awali  hazikuwepo  kabisa na pia WALTER  RED wamewapatia na   friji kwa ajiri ya  maabara  na    mawasiliano  simu  kwa ajiri ya  chumba  kimoja  kwenda chumba kingine

Meneja wa  Mradi wa  (HJFMTJ) Jofrey  Ndondole amesema wao  kama  wadau wa   sekta ya  afya wataendelea kuiunga  mkono  Serikali  katika  swala zima la uboreshaji wa  afya  hapa  nchini . 

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages