MBUNGE KAPUFI AWAFUNDA WANACCM KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA NA UCHAGUZI MKUU.
Na IRENE TEMU
Katavi
Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Mkoani Katavi,Sebastian Kapufi amewataka Viongozi na Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuitangaza miradi iliyotekelezwa na serikali kupitia Ilani ya CCM kuelekea Uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi Mkuu 2025.
Kapufi ameyasema hayo katika mkutano wa ndani wa Halmashauri Kuu ya kata Kakese ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake aliyoianza katika kata ya Mwamkulu Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi ya kuzungumza na Viongozi wa Halmashauri kuu za kata 15 zilizopo katika Jimbo lake la Mpanda Mjini
Mbunge wa jimbo la Mpanda mjini Sebastiani Kapufi akizungumza katika mkutano wa ndani wa Halimashauri kuu ya Kata ya kakese
Amewataka Viongozi wa CCM na wanachama wake kuyatangaza mazuri yote yaliyotekelezwa na serikali kupitia Ilani ya Chama cha Mapinduzi huku akiwataka kuwachagua viongozi wazuri katika uchaguzi wa serikali za mitaa watakao kivusha Chama katika uchaguzi Mkuu wa Rais,Wabunge na Madiwani mwakan
i.
"niwaombe sana wanaccm wenzangu,katika uchaguzi wa serikali za mitaa,tuwachague wenyeviti wanaofaa kwa kuwabeba na kuwapigani,tuache makundi ambayo yanaanzishwa na sisi wanaccm wenyewe badala yake tukipiganie chama kwa upendo na mshikamano"Mbunge Kapufi
Baadhi ya wajumbe walio hudhuria katika mkutano huo wakimsikiliza mbunge wakati akizungumza katika mkutano wa ndani wa Halimashauri kuu ya Kakese
Kapufi amewasisitiza pia wanachama wa CCM kuisemea serikali sambamba na miradi iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa ili iwe chachu ya mafanikio katika chaguzi zijazo.
Awali akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleao katika kata ya Kakese,Mtendaji wa kata hiyo Noria Bukuku amemwomba Mbunge Kapufi kuendelea kuisemea kata ya Kakese na vitongoji vyake ili baadhi ya miradi iliyoanzishwa kwa nguvu za wananchi ikiwepo maboma ya shule na kituo cha polisi viweze kupatiwa fedha kwa ajili ya umaliziaji.
Nao baadhi ya wanachama wa CCM akiwepo Rose Charles wamemshukuru Mbunge Kapufi kufika katika kata yao na kumwomba aendelea kujitolewa kwa ajili ya maendeleo ya kata na watu wake kwani amekuwa akiwagusa katika mahitaji na changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi wa kata hiyo.
MWISHO