WANANCHI WATISHIA KUHUJUMU MRADI BWAWA LA MAJI KWA MADAI YA KUTOLIPWA FIDIA

Baadhi ya wananchi katika Manispaa ya Mpanda wanaolalamikia kutolipwa fidia zao ili kupisha mradi wa Maji wa Miji 28.

Na  Walter Mguluchuma-Katavi

Wananchi wapatao  kaya  zaidi ya   500 wa  Mitaa ya  Shanwe, Mtemi Beda  na  Mtaa wa Kigamboni  katika Manispaa ya Mpanda  Mkoa wa Katavi  wametishia kuujumu  mradi wa   maji wa  bwawa la  milala  unaotekelezwa kwa zaidi ya  Shilingi Bilioni 22 kwa  madai ya kutolipwa  fidia ya maeneo yao   kwa   muda  mrefu wanayoishi  na wanayofanyia   shughuli  za kibinadamu.


Wananchi wapatao  kaya  zaidi ya   500 wa  Mitaa ya  Shanwe, Mtemi Beda  na  Mtaa wa Kigamboni  katika Manispaa ya Mpanda  Mkoa wa Katavi  wametishia kuujumu  mradi wa   maji wa  bwawa la  milala  unaotekelezwa kwa zaidi ya  Shilingi Bilioni 22 kwa  madai ya kutolipwa  fidia ya maeneo yao   kwa   muda  mrefu wanayoishi  na wanayofanyia   shughuli  za kibinadamu.

Wananchi hao wa mitaa  mitatu  hiyo wametowa  kauli  hiyo walipokuwa wakizungumza  na vyombo  mbalimbali vya  habari kuhusiana na kilio chao hicho cha  madai ya  maeneo yao  wanayoishi na wengine kuhama kwenye maeneo hayo  kwa ajiri ya kupisha  mradi huo unao simamiwa  na   mamlaka ya  Maji sahi na  usafi wa Mazingira (MUWASA)Manispaa ya  Mpanda .

Mradi huo wa Maji wa miji 28 katika halmashauri ya Manispaa ya Mpanda unatekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano wa Serikali ya India ambao hadi kukamilika kwake unatarajia kugharimu kiasi cha shilingi Bilioni 22.

Mwenyekiti wa  wahanga hao Peter  Matiyampula  amesema  toka  mwaka mwaka jana walipofanyiwa tathimini  kwa lengo  ya kulipwa fidia yao ya  makazi yao na  maeneo wanayofanyia  shughuli zao za kilimo  lakini  hadi sasa  hawajalipwa  fidia yao .

Baadhi ya Mabomba ya Maji yakiwa katika eneo la mradi ambao wananchi wanalalamikia kutolipwa fidia zao
Amebainisha kuwa  pamoja  na  wao kutolipwa  fidia zao  wanashangaa ni wao kuona  mradi huo umeanza kutekelezwa  huku wao wakiwa  hawajalipwa  fidia zao zaidi ya  wao kuambiwa wasiendelee kufanya  shughuli  yoyote kwenye  maeneo yao  hayo .

Amesema wapo  baadhi ya watu nyumba zao zimeanguka  na wamelazimika kwenda kupanga  nyumba kwenye maeneo  maeneo  mengine kwa kutegemea malipo ya fidia kwenye maeneo hayo.

Jonh Konchela mmmoja wa wanananchi hao amesema kuwa wanaimani mradi huo wa maji utakuwa muaroabaini wa tatizo la maji kwa manispaa ya Mpanda lakini kanuni na taratibu za kisheria zifuatwe za kulipwa fidia wanannchi ambao maeneo yatapitiwa na mradi huo.

Konchela anaiomba serikali kuwalipa fidia zao kwa wakati kwakuwa kuna wanananchi wanamashamba wamezuiliwa kuyaendeleza kwa minajiri kupisha mradi.

Kwa upande wake Penina Victor ameeleza kuwa amekata tamaa kwakuwa tangu waanze kufatilia malipo hayo ya fidia imekuwa muda mrefu sasa bila ya mafanikio yeyote.

Peter Matyampula mwenyekiti wa wahanga waliopisha ujenzi wa mradi wa Maji wa Miji 28 akizungumzia ucheleweshaji wa Malipo ya fidia kwenye Mradi huo.
Ameimba serikali kufanya haraka malipo ya fidia ili waendelee na maisha yao kama kawaida na familia zao kwakuwawamekuwa wanadanganywa kama watoto wadogo na sasa hivi wanaishi katika mazingira magumu kwakuwa hawaruhusiwi kuendeleza maeneo yao kwa kipindi cha miaka miwili sasa tangu zuio la kuwataka kutoendeleza maeneo hayo.

Mwajuma Ramadhani anaeleza kuwa jambo hilo limekuwa kero kwao kwani kila siku wamekuwa wakilifatilia sula hilo kwa muda mrefu sasahuku wakitumia gharama kubwa kwaajili ya kufatilia madai yao ya fidia.

Anafafanua kuwa katika kufatilia madai hayo wamekuwa wakipigwa dana dana na viongozi kwa kuwaahidi ahadi hewa ambazo hazitekelezeki licha mthamini kuwaeleza kuwa baada ya uthamini fedha zao zitalipwa baada ya miezi Sita kitu ambacho mpaka sasa hakuna kilichofanyika zaidi ya kuendelea kusubiria.

Rafael changuvu amesema kuwa hawako tayari kuona mradi huo ukiendelea bila ya kulipwa fidia zao kwa kuwa imekuwa kero kwani wanananchi hao wanateseka na kuomba serikali kuwalipa fidia kwa haraka.

Ameeleza kuwa anashangazwa kuona mradi huo ukiendelea kujengwa bila ya malipo yao kulipwa huku akiiomba serikali kupitia mamlaka husika kuwalipa malipo yao kwakuwa uthamini umeshafanyika kwa kipindi kirefu sasa.

Kufutia hali hiyo chombo hiki kimemtafuta Rehema  Nelsoni Kaimu Mkurugenzi mamlaka ya maji safi na usafi wa Mazingira Manispaa ya Mpanda [MUWASA] ameeleza kuwa uthamini kwaajili ya malipo ya wananchi hao umeshafanyika tangu mwezi wa tano mwaka huu wa kuhakiki madai  yao.

Rehema amebainisha kuwa mchakato wa malipo yao unaendelea chini ya Wizara ya fedha na wizara ya Maji na kuwaomba wananchi hao kuendelea kuwa wavumulivu na hawezi kutoa majibu ya moja kwa moja kuwa fedha hiyo italipwa lini.

Amewahakikishia wanananchi hao kuwa kila aliefanyiwa tathimini kwenye eneo lake atalipwa fedha yake na hakuna yeyote ambae hatolipwa fidia hiyo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages