TIC YATOA ELIMU YA UWEKEZAJI KWA WAFANYABIASHARA NA WAJASILIAMALI KATAVI

Felix Jonh Meneja uhamasishaji kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania[TIC] akitoa elimu kwa Wafanyabiashara ,wewekezaji na wajasiliamali wa Mkoa wa Katavi kuhusu umuhimu wa kufanya uwekezaji kwenye Sekta Mbalimbali. 

Na Paul Mathias-Katavi

Wafanyabiashara na wawekazaji katika mkoa wa Katavi wameombwa kuchangamkia fursa za uwekezaji wa ndani kwa lengo la kuinua uchumi wa mkoa na kuongeza kipato chao kupitia uwekezaji huo.

Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Albert Msovela akifungua semina ya Wawekezaji wafanyabiashara na wajasiliamali iliyoandaliwa na kituo cha uwekezaji Tanzania

Wafanyabiashara na wawekazaji katika mkoa wa Katavi wameombwa kuchangamkia fursa za uwekezaji wa ndani kwa lengo la kuinua uchumi wa mkoa na kuongeza kipato chao kupitia uwekezaji huo.

Wito huo umetolewa na Felix Jonh Meneja uhamasishaji kutoka kituo cha uwekezaji Tanzania [TIC]wakati akitoa semina kwa wafanyabiashara na wawekezaji wa Mkoa wa Katavi.

Jonh ameeleza kuwa kituo hicho kipo katika kampeni ya kusimamia kampeni ya uwekezaji wa ndani yenye lengo la kuhamasisha wafanyabiashara na wadau wa sekta ya uwekezaji kujitokeza kufanya uwekezaji kwenye Nyanja mbalimbali.

Amesema kuwa kituo cha uwekezaji Tanzania kimefika mkoa wa Katavi kwa lengo la kukutana na wafanyabiashara wajasilaimali na Wawekezaji kwa lengo la kutoa elimu na hamasa kwa kushirikiaana na wadau wa uwekezaji hususani taasisi za kifedha.

Amefafanunua kuwa miongoni wawekezaji waliokutananao katika mkoa wa Katavi wameonyesha moyo wa kuunga mkono uwekezaji katika mkoa wa Katavi.

’Tumeweza kuongea na wanakatavi naamini wametuelewa na wengi wapo tayari kujitokeza kwaajili ya kusajili miradi yao ili waweze kunufaika na vivutio vya kikodi’’-Felix Jonh

Amesema kuwa kwa kushirikiana na wadau wa uwekezaji kupitia kituo cha uwekezaji Tanzania wawekezaji na wafanyabiashara kwa kuwapatia vivutio vya kikodi na kuleta unafuu katika mitaji ya uwekezaji inayohitajika.

Amebainishakuwa wadau wa sekta ya uwekezaji ikiwemo taasisi za kifedha zimekuwa msaada mkubwa katika uwekezaji kwa kuleta unafuu kwa kuwawezesha watanzania  kupata mitaji na hatimae kufikia miradi ya ndoto zao.

Kwa upande wake Katibu tawala mkoa wa Katavi Albert Msovela amesema serikali ya mkoa wa Katavi imekuwa ikiendelea kutengeneza mazingira wezeshi kwa wawekezaji kwa lengo la kuvutia wawekezaji wengi zaidi kuja kuwekeza Mkoa wa Katavi.

Msovela ameeleza kuwa maboresho makubwa yaliyofanywa na serikali katika miundo mbinu mbalimbali ikiwemo Barabara,Maji na umeme imekuwa kivutio kikubwa cha wawekezaji kwa mkoa wa Katavi.

‘’Miundombinu ambayo inawezesha Viwanda viweze kuwepo kwa sababu upatikanaji wa maji upo wa kutosha aridhi ipo ya kutosha na hivi sasa tunaenda kuwa na umeme wa Grid ya Taifa kwahivyo tunawakaribisha wawekezaji wote’’-Msovela

Amebainisha kuwa Mkoa wa Katavi unafursa mbalimbali za uwekezaji ikiwemo Utalii, Mabonde mbalimbali ya Kilimo ambayo yanaweza kusaidia shughuli za kilimo pamoja na aridhi yenye rutuba ambayo inakubalika kwa kilimo cha aina yeyote.

Kuhusu fursa ya Masoko amesema mkoa wa Katavi nimiongoni mwa Mikoa inayopakana na nchi za Congo,Burundi,Uganda na Rwanda hali hiyo hulahisisha upatikanaji wa masoko wa bidhaa mbalimbali kwa wawekezaji wa Mkoa wa Katavi kwa kufanya baishara na watu


Wenslauns Kamtoni mmoja ya wawekezaji waliodhuria semina hiyo amesema kuwa kupitia kituo cha uwekezaji Tanzania kimekuwa kiunganishi kwa wawekezaji kwa kuwasaidia wawekezaji kupata fursa za kuingia ubia wa uwekezaji na watu kutoka nje ya nchi.

Katika hatua nyiningine ameishukuru serikali kwa namna inavyoendelea kuboresha miundombinu ya Barabara ili kurahisisha uchukuzi kwa wawekezaji na wafanyabiashara kwa ujumla.

Sekta ya uwekezaji imekuwa ikitajwa kuwamoja ya sekta ambayo imekuwa ikizalisha ajira nyingi kwa watanzania na kupunguza kwa kiasi flani tatizo la ukosefu wa ajira hususani kwa vijana

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages