WATU WATANO WAKAMATWA KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA MENO YA TEMBO VIPANDE 18

 

WATU WATANO WAKAMATWA   KWA TUHUMA ZA KUKUTWA NA MENO YA TEMBO 18

Na Walter Mguluchuma

    Katavi

Watu sita wanashukiliwa na Jeshi la Polisi  Mkoa wa  Katavi kwa tuhuma za kukamatwa na  meno ya  Tembo  vipande 18 wakiwa wameyahifadhi ndani ya nyumba katika  maeneo ya  Manispaa ya  Mpanda  na Inyonga  Wilayani  Mlele  Mkoani  Katavi na   bunduki mbili aina ya gobole  pamoja   na  nyama pori vipande 26.

Kaimu  Kamanda wa  Jeshi la  Polisi  Mkoa wa Katavi  David  Mutasya amewaambia Wandishi wa Habari kuwa watuhumiwa hao wamekamatwa kufatia   msako mkali uliofanywa na  jeshi  la  Polisi  Mkoa wa Katavi



Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Devidi Mutasya akielezea kwa waandishi wa habari juu ya kamatwa kwa watuhumiwa watano wakiwa na meno ya Tembo vipande 18


Amesema watuhumiwa hao    watano walikamatwa  na  meno   ya  tembo  katika  maeneo    mawili tofauti    katika  eneo la Mtaa wa  Ilembo Manispaa ya  Mpanda  na  Inyonga  Wilayani  Mlele .

Mutasya ameeleza kuwa  kabla ya kukamatwa kwa watuhumiwa hao jeshi la polisi lilikuwa  limepata taarifa ya  watuhumiwa hao kuwa wana jihusisha  na maswala ya biashara  haramu ya   meno ya tembo    na ndipo  baada ya kupata taarifa hizo jeshi la polisi  lilianza  msako mkali wa kuwasaka na  waliweza kufanikiwa  kuwakamata watuhumiwa hao wakiwa na vipande 18 vya  meno ya tembo na bunduki  mbili  na vipande  26 vya  nyama ori

Amebainisha kuwa  hadi  sasa  watuhumiwa hao  bado wanaendelea kushikiliwa na  jeshi la  Polisi  Mkoa wa Katavi  na  mara uchunguzi  utakapokuwa  umekamilika  watuhumiwa hao wanafikishwa Mahakamani ili wakajibu tuhuma ambazo zinawakabili


Kaim Kamanda wa polisi akionyesha mbele ya waandisi wa habari vipande 18 walivyo kamatwa na vyo watuhumiwa watano katika Manispaa ya Mpanda na Inyonga wilayani Mlele.

Amesema   katika  kipindi  cha  mwezi  mmoja  wa Agosti  Jeshi la Polisi   limeweza kupata  mafanikio mbalimbali  kufatia    doria ,misako  na operesheni  walizofanya  na kufanikiwa  kukamatwa kwa watuhumiwa  97  wanaojihusisha  na vitendo vya uhalifu  wakiwa na vielelezo  mbalimbali

 Amevitaja  vielelezo  hivyo kuwa ni  bangi  kete 164, walizokamatwa  nazo watuhumiwa 10, watuhumiwa  38 walikamatwa  na pombe haranu gongo  lita  281, watuhumiwa 17 walikamatwa kwa  kujeruhi watu  na watuhumiwa 11 wamekamatwa   katika  matukio tofauti  ya mauaji ,

Vilevile wameweza kuwakamata watuhumiwa  10 wakiwa na mali mbalimbali za wizi    ambazo ni pikipiki  mbili MC ,979 DJR  na  MC  ,482 DVH na  mifuko 30 ya  simenti  yenye  thamani ya  Tshs  1,800,000/

 


Vipande vya meno ya Tembo 18 walivyo kamatwa navyo watuhumiwa watano  na bunduki 2 zilizo tumika kufanyia ujangili huo.

Kaimu  Kamanda  Mutasya  amewaonya wananchi wa Mkoa wa Katavi kutojihusisha  na vitendo vyovyote vya uhalifu na ujangili kwani watakao  jaribu kufanya vitendo hivyo watakamatwa mara moja na kuchukuliwa hatua sitahiki

 

MWISHO

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages