Na Jackson -Gerald
Jeshi la polisi Mkoa wa katavi limeshiriki kufanya zoezi la usafi na uchangiaji damu katika
hospitali ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi ikiwa ni sehemu ya kusherekea maazimisho ya kilele
cha miaka 60 ya Jeshi la hilo.
Askari wa Jeshi Polisi Mkoa wa Katavi wakifanya usafi kwenye Hospitali ya Manispaa ya Mpanda
Jeshi la polisi Mkoa wa katavi limeshiriki kufanya zoezi la usafi na uchangiaji damu katika hospitali ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi ikiwa ni sehemu ya kusherekea maazimisho ya kilele cha miaka 60 ya Jeshi la hilo.
Akizungumza baada ya kumalizika kwa zoezi hilo leo Septemba 17, 2024. Kaimu
Kamanda wa jeshi la Polisi David Mtasya amesema Jeshi la Polisi katika
kusherekea maazimisho ya kilele cha miaka 60 ya jeshi hilo limeamua kufanya
usafi na kutoa damu katika hospital ya wilaya ya Mpanda ili kuonyesha kuwa jeshi hilo lipo karibu na
jamii.
Mtasya amesema Jeshi la polisi limevutiwa kufanya zoezi hilo katika
hospitali kwakua ni moja ya sehemu zinazo vuta hisia za watu wengi kuliko
kwenda maeneo mengine lakini pia kuwasaidia watu wenye uhitaji wa damu ili
kupunguza vifo vinavyo tokana na ukosefu wa damu kwa makundi mbalimbali yenye uhitaji.
Amesema hospitali ni sehemu inayo hitaji usafi wa hali ya juu katika kudhibiti mlipuko wa magonjwa ambayo yanababishwa na mrundikano wa uchafu. Kwa sababu hiyo jeshi la Polisi limeamua kushiriki kuongeza nguvu ya uwajibikaji katika kuhakikisha maeneo yote ni safi.
Katika hatua nyingine Mtasya ametoa wito kwa taasisi nyingine kushiriki
kutoa damu, kufanya usafi na kuwasaidia wasio jiweza ili kuwa sehemu ya jamii yenye
upendo na uajibikaji.
Mganga mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Mpanda, Dk Paul Lugata amelishukuru Jeshi hilo kwa kuchangia
damu kwa sababu watu wenye uhitaji ni
wengi katika hospitali hiyo akitaja ajali nyingi kuongezeka, Watoto
wadogo kuishiwa damu na mama wajawazito
wanao jifungua kuishiwa damu makudi yote yanahitaji damu.
Vilevile amewashukuru askari walio jitolea kufanya usafi katika maeneo mbalimbali yanayo zunguka hospitali hiyo na kuwaomba waendelee kujitolea kushiriki kufanikisha mambo mbalimbali ya kuisaidia jamii.
Abdala Makwavi, Ni moja ya askari polisi walio changia damu amesema
jukumu la askari polisi ni kulinda watu na mali zao lakini wameona vema jambo
jema kuwa sehemu ya jamii katika kuhakikisha watu wenye uhitaji wa damu
wanapata damu ili kuokoa uhai wao.
Septemba 17, 2024 ni kilele cha maazimisho ya miaka 60 ya
Jeshi la polisi nchini ambapo maazimisho ya kitaifa yamefanyika Mkoa wa
Kilimanjaro katika chuo cha mafunzo ya kijeshi Moshi.