MWENGE WA UHURU WAZINDUA DARAJA LA UKOMBOZI KWA WANANCHI WA MANISPAA YA NPANDA

Kiongozi wa mbio za mwenge Mwaka 2024 Godfrey Mzava akikagua daraja lililozinduliwa na Mwenge

Na Walter Mgulichuma-Mpanda

Mwenge wa  Uhuru imezindua  daraha   la  Kawaliyowa   ambalo  ambalolitakuwa  ni  mkombozi  kwa  Wanachi wa Manispaa ya  Mpanda  hususani wa Kata ya Ilembo na kuwaondolea wananchi adha waliyokuwa  nayo   hasa kipindi  cha  masika

Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Sebastiani Kapufi akiishukuru serikali kwa kuleta fedha na kufanikisha daraja hilo

Mwenge wa uhuru unezindua Daraja la Kawaliyowa ambalolitakuwa ni mkombozi kwa wanananchi wa Manispaa ya Npanda hususani wa Kata ya Ilembo na kuwaondolea adha wananchi waliyokuwa wanaipata wakati wa Masika. 

Uzinduzi huo  umefanywa na kiongozi wa  mbio za  Mwenge wa   mwaka 2024  Godfrey  Mzava baada ya kuridhika  na  ujenzi wa  daraja  hilo  uliogharimu  kiasi  cha  shilingi   milioni  475,

Akitowa taarifa ya ujenzi wa  daraja  hilo K aimu  Meneja wa TARURA wa  Manispaa ya  Mpanda  Mhandisi   Pascal  Sindani  amesema kuwa  kukamilika   kwa  daraja  hilo  muhimu kutakuwa na  manufaa sana kwa wananchi wa  Manispaa ya  Mpanda    na ametaja  baadhi ya  manufaa hayo  kuwa  ni

Kurahususha  usafirishaji  wa  nazao  kutoka enei ka Kawaliyowa  kwenda  katika  maeneo  mengine ya Manispaa ya  Mpanda  ambapo  hapo  awali  eneo  hilo  lilikuwa   halipitiki  wakati wa  masika   kiurahisi  na  kuwafanya wananchi  wapate adha  kubwa ,




Pia  kutarahisisha  usafiri kwa wanafunzi wa shule za Msingi  na Sekobdari  na  wajawazito wanapokuwa  wanakwenda kutafuta  huduma  kwenye  Zahanati na kwenye kituo cha  afya  kwani  hapo  awali walikuwa wanasubiri wakati wa nasika maji yapungue ndipo wavuke m

 Sindani   amesema  uwepo wa  daraja   hilo  unatoa  furusa   ya ajira  kwa  Vijana  kupitia  shughuli  za  Nodaboda   awa  biashara  hiyo  ilikutana  na  changamoto  ya kutokuwepo kwa  daraja kwenye  eneo hilo.

Kwa upande wake mbunge wa Jimbo la Mpanda mjini Sebastiani Kapufi amemshukuru Rais Dk Samia suluhu Hassan kwa kuwaletea fedha ambazo zimeweza kujenga daraja ambalo lilikuwa ni changamoto wakati wa Masika kwa wananchi.

Amesema kuwa kukamilika kwa daraja hilo itafungua fursa kwa wanananchi kufanya kazi zao za kiuchumi pasipo na tatizo lolote na kuwaomba wananchi kuutunza mradi huo.

Kapufi amesema kuwa miradi ambayo imekuwa ikiletwa na serikali imekuwa na tija kubwa kwa wananchi wa manispaa ya Mpanda.

Kwa upande wake kiongozi wa Mbio za mwenge wa uhuru Mwaka 2024 Godfrey Mzava amelidhishwa na mradi huo na kuwaomba wananachi kuutunza mradi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages