RC AZINDUA UANDIKISHAJI DAFTARI LA MKAZI KWA WANANCHI ILI KUSHIRIKI UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko [kulia] akishriki katika zoezi la uandikishaji wa daftari la wakazi katika Mtaa wa ilembo Manispaa ya Mpanda kwaajili ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa.

Na Paul Mathias-Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amezindua zoezi la uandikishaji la Daftari la wakazi Katika Mtaa wa Ilembo Manispaa ya Mpanda kwaajili ya kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwamanvua Mrindoko[Mwenyekilemba cheusi] akiwa na wananchi wa Mtaa wa Ilembo katika foleni ya kuandikisha wananchi kwaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amezindua zoezi la uandikishaji la Daftari la wakazi Katika Mtaa wa Ilembo Manispaa ya Mpanda kwaajili ya kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa

Akizungumnza muda mchache baada ya kujiandikisha kwenye mtaa huo  mrindoko amesema zoezi hilo limeanza leo 11/10/2024 na litakamilika mnamo 20/10/2024.

Ameeleza kuwa wahusika wataokaojiandikisha katika Daftari la wakazi kwenye maeneo yao ni raia wa Tanzania wanaoishi katika mitaa,Vitongoji,na Vijiji husika ili waweze kushiriki katika zoezi la uchaguzi wa serikali za mitaa 27/11/2024.

Katibu Tawala Mkoa wa Katavi,Albert Msovela [kulia] akiandikishwa katika Daftari la Mkazi mtaa wa ilembo Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi

‘’Sifa za kujiandikisha uwe raia wa Tanzania umri wa miaka 18 na kuendelea na uwe mkazi halali wa eneo unaloenda kujiandikisha hapa tupo mtaa wa ilembo kwahiyo wakazi wa mtaa huu wanapaswa kuja kujiandikisha’’Mrindoko

Mrindoko amewaomba wananchi katika maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Katavi kuendelea kujitokeza kwa wingi kujiandikisha ili waweze kutumia haki yao ya kikatiba kuwachangua viongozi wa mitaa na vijiji.

‘’Niwashukuru kwa wale wote ambao wameshajiandikisha kwa takwimu tulizonazo hadi tunaondoka kwenye kituo hiki tayari wananchi 55 wamejiandikisha huu ni mwanzo mzuri hii inaonyesha nikwanamna gani wananchi wamehamasika ukiangalia muda wa saa moja tu watu hawa tayari wamejitokeza’’ Mrindoko

Katika hatua hatunyingine amewaagiza wakuu wa Wilaya kuongeza hamasa ya zoezi hilo kwa wananchi ili kuhakikisha wananchi wote wanajiandikisha kwenye daftari la wakazi pasipo na changamoto yeyote.

Haule Jonh Mkazi wa Mtaa wa Ilembo Manispaa ya Mpanda akiandikishwa katika daftari la Mkazi ili aweze kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Sophia kumbuli Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda na Msimamizi wa uchaguzi Manispaa ya Mpanda amesema manispaa ya Mpanda inajumla ya vituo 141 kwaajili ya uandikishaji kwa wananchi.

 Kumbuli ametoa rai kwa wanananchi kutumia siku hizo kumi kikamilifu kwa kujitokeza kujiandikisha kwenye daftari hilo ili wapate fursa ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa.

Amina juma Mkazi wa Mtaa wa ilembo amesema ametokeza kwaajili ya kujiandikisha ili aweze kupata nafasi ya kumchagua kiongozi wa mtaa pindi wakati utakapofika

Ameeleza kuwa kunafaida ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa kwakuwa kiongozi atakae mchagua atakuwa na uwezo wa kupanga mipango ya maendeleo kuanzia ngazi ya mtaa na kijiji.

Uchaguzi wa serikali za mitaa umepagwa kufanyika 27,Novemba Mwaka huu nchinzima .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages