WANANCHI WASHIRIKI NA MBUNGE WAO KUJIANDIKISHA KWAAJILI YA UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA

Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Sebastini Kapufi [Mwenyeshati la bluu] akiwa katika foleni ya uandikishaji na wananchi wa Mtaa wa kichangani aliposhiriki zoezi la kujiandikisha kwaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa.

 Na Paul Mathias-Mpanda

Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Sebastiani Kapufi amewaomba wananchi katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kujitokeza kwa wingi katika kuajimdikisha katika Daftari la Mkazi ili wawaeze kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mbunge wa jimbo la Mpanda Mjini,Sebastiani Kapufi akiwa katika zoezi la kujiandikisha katika ofisi za mtaa wa Kichangani Kata ya Nsemlwa Mpanda Mjini

Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Sebastiani Kapufi amewaomba wananchi katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda kujitokeza kwa wingi katika kuajimdikisha katika Daftari la Mkazi ili wawaeze kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

Wito huo ameutoa baada ya kushiriki kujiandikisha katika ofisi za mtaa wa Kichangani Kata ya Nsemlwa Manispaa ya Mpanda ambapo amesema nivyema wananchi kutumia fursa ya kujiandikisha ili wawaeze kuwa sehemu ya kuwachagua viongozi kwenye uchaguzi ujao wa serikali za mitaa.

‘’Nitoe wito kwa wananchi wajitokeze kwa wingi kuja kujiandikisha ili kupata tiketi ya wao kutumia haki yao ya kikatiba ya kumchagua mwenyekiti wa mtaa,Mwenyekiti wa Kijiji na Kitongoji na wajumbe wake bila kujiandikisha huwezi kuwa sehemu ya kumchagua kiongozi wa serikali ya mtaa,,Kapufi

Ameeleza kuwa fursa hiyo ya wananchi kujiandikisha katika daftari la mkazi kwaajili ya uchaguzi wa serikali ni shemu ya namna ambayo serikali inaheshimu misingi ya utawala bora kwa kuwahusisha wananchi moja kwa moja katika kuwachagua viongozi wao kupitia sanduku la kura.

Amesema kuwa zoezi hili ni tofauti na lililofanyika la urekebishaji wa kudumu la mpiga kura kwakuwa lilikuwa linahusisha kwaajili ya uchaguzi mkuu wa Rais Wabunge na madiwani lakini zoezi hili linahusisha uchaguzi wa serikali za mitaa.

Mwajuma Haruna mkazi wa Mtaa wa Kichangani amesema kuwa ameshiriki kujiandikisha ili aweze kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa na kuwaomba wananchi kujitokeza kwa wimgi kwaajili ya kujiandikisha

‘’Nimefurahi kujiaandikisha nina Imani nitashiriki katika uchaguzi wa kumchagua kiongozi wangu wa mtaa bila tatizo lolote’’Mwajuma

Zoezi la unadikishaji wa Daftari la Mkazi kwaajili ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa limeanza rasmi leo 11/10/2024 na linatatalajia kukamilika 20/10/2024 huku uchaguzi wa serikali wa mitaa ukiwa umepagwa kufanyika 27/11/2024 hapa mchini.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages