TANESCO KATAVI YAZINDUA KLABU ZA UMEME SHULENI

 

Afisa uhusiano kwa wateja TANESCO Mkoa wa Katavi Proches Joseph akitoa elimu kuhusu matumizi mbalimbali ya umeme kwa wanafunzi wa Darasa la Tano Shule ya Msingi Mpanda

Na Paul Mathias-Katavi

Shirika la umeme Tanzania TANESCO Mkoa wa Katavi katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja imezindua maadhimisho hayo kwa kuanzisha klabu ya umeme Katika shule ya Msingi Mpanda Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.

Shirika la umeme Tanzania TANESCO Mkoa wa Katavi katika kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja imezindua maadhimisho hayo kwa kuanzisha klabu ya umeme Katika shule ya Msingi Mpanda Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.

Afisa uhusiano kwa Wateja TANESCO Mkoa wa Katavi Proches Joseph amesema kuwa katika wiki ya Huduma kwa wateja wameamua kuanzisha Klabu ya umeme shuleni hapo kwa wanafunzi wa Darasa la Tano kwa lengo la kuhakikisha wanafunzi hao wanakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu shirika la umeme na matumizi ya umeme kwa ujumla.

Amebainisha kuwa Elimu kuhusu shirika la umeme Tanzania TANESCO Mkoa wa Katavi pamoja na huduma zinazotolewa kwa wanananchi itakuwa sehemu ya Elimu itakayotolewa kwa wanafunzi hao ili wawe mabalozi wazuri kuhusu huduma za umeme.

Ameeleza kuwa Klabu hiyo itakuwa ya kwanza kwa Mkoa wa Katavi huku akibainisha kuwa mpango mkakati ni kuzifikia shule nyingi zaidi kwa ajili ya kuwapatia elimu sahihi ya matumizi ya umeme wakiwa nyumbani na maeneo mengine.

Wanafunzi wa Darasa la Tano Shule ya Msingi Mpanda wakiwa katika Picha ya pamoja na maafisa wa TANESCO Mkoa wa Katavi baada ya kuanzisha Klabu ya umeme
Afisa huyo  amesema kuwa wamechagua kundi la wanafunzi wa shule ya Msingi kwa kuwa wapo katika umri wa kujifunza mambo mbalilimbali hivyo wakipatiwa Elimu hiyo watakwenda kuwa mabalozi wazuri wa kuisambaza elimu hiyo kwa wengine na kuwasaidia zaidi katika umri wa utu uzima.

“Tumechagua kundi hili la wanafunzi hapa shule ya Msingi Mpanda kwa kuamini wanafunzi hawa wapo kwenye umri sahihi wa kujifunza zaidi hivyo elimu hii kuhusu Tanesko itafika kwa urahisi zaidi kupitia wanafunzi hawa”-Proches

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Mpanda Michael Mwambojoke  amesema kuwa wamefurahishwa na ujio wa Taasisi ya TANESCO Mkoa wa Katavi kwenye shule hiyo kwakuwa elimu hiyo itawasaidia wanafunzi watakao kuwa sehemu ya Klabu ya umeme kufahamu zaidi kuhusu masuala ya umeme na nishati.

Mwambojoke ameziomba taasisi zingine kuiga mfano wa TANESCO Mkoa wa Katavi kwa kuja na utaratibu wa kuanzisha Klabu ya umeme yenye lengo la kuwasaidia wanafunzi kuwa na uelwa zaidi kuhusu umeme wakiwa Majumbani kwao.

‘’Tunawakaribisha sana TANESCO hapa shuleni kwetu uanzishaji wa Klabu hii ya Umeme utasaidia kwa kuwa watoto hawa watakuwa Mabalozi wazuri kuhusu TANESCO na watumiaji wazuri wa umeme wakiwa nyumbani’’Mwambojoke

Maadhimisho ya Wiki ya Huduma kwa Wateja huadhimishwa kila mwaka Mwezi Oktoba  Dunia nzima kwa Mashirika ya Umma na Binafisi kuelezea namna mashirika yanavyo hudumia wateja Maadhimisho hayo yanaenda sambamba na kauli mbiu inayosema ‘’Ni zaidi ya matalajio’’.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages