RC KATAVI WATU WASIO RAI WA TANZANIA KUTOJIHUSISHA NA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA.

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko.

Na Walter  Mguluchuma, Katavi.

Mkuu wa  Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko  amewaonya watu wote wanao  ishi  katika  Mkoa wa Katavi  ambao  sio  Raia wa Tanzania  kutojihusisha  katika  kushiriki  katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa .

Onyo  hilo  amelitowa wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na  maandalizi ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa katika  Mkoa wa Katavi .

Amebainisha  kuwa  Mkoa wa Katavi   kutokana na asili ya Nchi yetu ya  kupokea wageni  wa  kutoka  nchi jirani  hali  hiyo imefanya  Mkoa huu kuweza kupokea wageni  wa kutoka  Mataifa  mbalimbali  wanao ishi  kwenye Mkoa huu ambao sio Raia wa Tanzania .

Kwa  hali hiyo  anatowa  onyo kwa  watu ambao wanaoishi    kwenye  Mkoa wa Katavi ambao sio Raia wa Tanzania   kutojihusisha kwenye  uchaguzi huo  kwa kuwa wao  hawana sifa ya kuhusika  katika uchaguzi wa Serikali za  Mitaa kwa kupiga kura wala kugombea .

Mrindoko  amesema  zoezi hili  ilnawahusu  Raia wa Tanzania  tuu kwa kuweza  kujiandikisha na kupiga  kura na kuchaguliwa ,

Amesisitiza kuwa Serikali ya Mkoa wa Katavi itakuwa  macho  na  kwa wale watakao  bainika  kufanya  udanganyifu wa  aina yoyote  hatua  kali zitachukuliwa dhidi yao ,

Rc  Mrindoko  amesema Mkoa wa Katavi  utakuwa  na vituo  835  katika  ngazi za  vitongoji ,Mitaa na  Vijijivitakavyotumika  katika uandikishaji na upigaji wa kura  katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa vilivyoko   ,kwa  Mkoa   mzima .

Ametowa  wito  kwa wananchi wote wa  Mkoa huu kujitokeza kwa wingi   kuanzia  tarehe  11  hadi  tarehe   20  mwezi huu kujiandikisha kwa wingi  kwa kuzingatia sifa za kuwa Raia wa Tanzania  kuwa  mkazi wa eneo husika na kuwa na umri wa kuanzia miaka  18 na kuendelea   pia kuwa na akili timamu .

Amefafanua kuwa  zoezi ambalo lilifanyika mwezi  julai mwaka huu  la  maboresho la  daftari la kudumu la   maboresho ya tume  huru ya  uchaguzi   linahusika na uchaguzi  mkuu utakaofanyika mwaka 2025 kwa  maana hiyo  uchaguzi wa Serikali za Mitaa  wananchi wote wenye sifa  ta kupiga kura  watahitajika kujiandikisha upya  bila kujari kuwa wamehiandikisha kwenye  daftari la kudumu la mpiga kura .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages