WIKI YA MWANAKATAVI KUANZA OCTOBA 25, 2024.

 

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko.

Na Walter Mguluchuma, Katavi.

Wiki ya Mwanakatavi itafanyika Octoba 25, 2024 hadi Octoba 31, 2024 ambapo wananchi wa ndani nan je ya Mkoa wa Katavi watapata fursa kubwa ya kujifunza na kuinua uchumi wao.


Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko amesema hayo leo ofisini kwake wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari namna ambavyo tukio hilo maalumu litakuwa jukwaa bora kwa wafanyabiashara na wadau mbalimbali kujikwamua kiuchumi.

Mrindo amesema “Hii ni mara ya tatu tutaadhimisha wiki ya Mwanakatavi ambayo lengo lake ni kumpatia mwananchi wa Mkoa wa Katavi fursa ya kujifunza teknolojia mbalimbali zinazohusiana na sekta za kiuchumi, kijamii na uzalishaji sambamba na kubadilisha uzoefu na mikoa na nchi mbalimbali kuhusiana na fursa za kiuchumi, kijamii na uwekezaji”.

“Kuweza kuonesha bidhaa, maliasili na rasilimali tulizo nazo ndani ya Mkoa wetu wa Katavi kwa wananchi wetu” Amesisitiza Mkuu wa Mkoa huo.

Ameweka wazi kuwa mwaka huu tukio hilo la mwanakatavi lina kauli mbio “ Katavi Yetu Chagua Viongozi bora Imarisha Uchumi kwa Maendeleo endelevu” ambapo ameeleza kuwa kauli mbiu hiyo inahamasisha wananchi katika shughuli za uchumi na kuimarisha uchumi wao kwa kuongeza tija na kuendelea kujivunza kutoka kwa watu wengine.

Ameongeza “Kwa kuwa ni mwaka mahususi kwa uchaguzi wa serikali za mitaa pia kauli mbiu hii inasisitiza kuhimiza kila mwananchi kujitokeza na kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa kwa maana hiyo nitumie nafasi hii kuwakaribisha wananchi wa mkoa wa Katavi na nje kushiriki kwa pamoja”

Wiki ya mwanakatavi itakuwa na matukio mbalimbali kwa wiki nzima ambapo kwa siku ya kwanza ya Oktoba 25, 2024 itakuwa ni siku ya ufunguzi na yatakuwepo maonesho katika uwanja wa CCM Azimio Manispaa ya Mpanda Mkoani hapo.

Maonesho hayo yataanza asubuhi hadi saa moja jioni kila siku kwa muda wa wiki moja na maonesho kwa maana ya kuonesha bidhaa, kujifunza masuala ya fursa za uwekezaji, utalii, kilimo, mifungo, uvuvi, utamamduni wa Katavi pamoja na upatikanaji wa fedha za kuichua uchumi.

Octoba 26, 2024 itakuwaa siku ya michezo na mazingira ambapo kutakuwa na mbio zitakazo julikana kwa jina la Katavi Hip run zitakazo jumuisha Km 5, Km 10 na Km 21 na kwenye mazingira kutakuwa na uhamasishaji wa utunzaji wa mazingira na kuhamasisha masuala ya matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Octoba 27,  2024 itakuwa siku mifugo  na uvuvi ambapo washiriki watapata fursa ya kujifunza fursa zilizopo katika sekta ya kilimo na uvuvi.

Octoba 28, 2024 itakuwa ni siku ya uwekezaji na biashara ikihusisha sekta za madini, viwanda, biashara za hotel na maduka na kutangaza sekta za kifedha ambazo zinawawezesha wananchi katika shughuli za biashara na uwekezaji.

Octoba 29, 2024 itakuwa ni siku ya Utalii na Uhifadhi ambapo kutakuwa na tukio maalumu la kuadhimisha miaka 50 ya Hifadhi ya Taifa Katavi na kutembelea mbuga hiyo kama sehemu ya kufanya utalii.

Octoba 30, 2024 itakuwa ni siku ya Kilimo na Ushirika ambapo fursa mbalimbali zitaonekana pamoja na kufanya tathimini ya mahala tulipo na waedapo ili kuhakikisha kilimo kinakuwa na tija.

Na Octobaa 31, 2024 itakuwa siku ya kilele ambapo mambo yatakayo fanyika ni pamoja na kuzindua msimu wa akilimo wa mwaka 2024/25. Aidha amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kwenye maonesho hayo yenye fursa kubwa kiuchumi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages