VITONGOJI 75 KATAVI KUONDOKANA NA MATUMIZI YA VIBATARI

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akielezea umuhimu wa Mradi huo wa umeme kwa wananchi.

Na Jackson Gelard-Katavi

Mkuu wa  Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amemtaka mkandarasi anae tekeleza mradi wa umeme  wa Rea katika vitongoji  75 kwenye Mkoa wa Katavi  kuhakikisha anatoa fursa  za kazi kwa wananchi  wa Mkoa wa Katavi.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwananvua Mrindoko akisalimiana na Meneja wa Mradi huo Novatus Lyimo 

Mkuu wa  Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amemtaka mkandarasi anae tekeleza mradi wa umeme  wa Rea katika vitongoji  75 kwenye Mkoa wa Katavi  kuhakikisha anatoa fursa  za kazi kwa wananchi  wa Mkoa wa Katavi

Hayo ameyabainisha wakati  wa kikao kifupi cha kumpokea Mkandarasi  kutoka katika kampuni ya M/s Dieynem company Ltd yenye makao makuu yake jijini Dar es salaam.

Mrindoko amewataka wananchi wa Mkoa wa Katavi kuchangamkia fursa za kazi  katika vitongoji mbalimbali vilivyopo katika vijiji vyao ambapo mradi huo unapita  sambamba na kuunganishiwa umeme katika makaazi yao ,maeneo ya taasisi  na katika viwanda vidogo na vikubwa vilivyopo katika maeneo husika.

Kwaupande mwingine Mrindoko amesema kuwa serikali ilikua ikiendelea kusikiliza malalamiko ya wananchi juu ya ukosefu wa umeme katika vitongoji mbalimbali ambayo yamekuwa ya kiwasilishwa kwa njia simu ,mikutano mbalimbali na kwa njia ya redio na kuendelea kuyafanyia kazi ili vitongoji vyote vilivyopo ndani ya Mkoa wa Katavi viweze kuunganishiwa umeme.

Mhandisi Gilbert Furia Meneja wa Miradi ya Rea Mkoa wa Katavi akifafanua mradi huo namna ulivyaanza kutekelezwa kwa wanananchi

Mrindoko ameishukuru Rea kuweza kufikisha umeme katika vijiji 172 vilivyopo katika Mkoa wa Katavi na kuendelea kupunguza changamoto ya ukosefu wa umeme katika maeneo hayo.

Amemtaka Mkandarasi wa Kampuni ya M/S Dieynem Company Ltd kuhakikisha anatekeleza mradi huo kwa ufanisi mkubwa na kwa kuzingatia uharaka wa kazi ili kumaliza kazi hiyo kabla ya muda wa miaka miwili kama mkataba unavyo eleza ili wananchi waweze kunufaika na mradi huo kwa wakati.

Mhandisi Gilbert  Furia Meneja wa Miradi ya Rea Mkoa wa Katavi amesema mradi huo utahusisha ujenzi wa kilomita 150 za msongo  mdogo wa umeme pamoja na ujenzi wa mashine umba (Transfomers) 75.


Gilibert amesema mradi huo utagharimu kiasi cha shilling Bilio 9.5 za kitanzania na mkandarasi amekwisha anza kutekeleza mradi huo.

Amebainisha kuwa mradi huo utatekelezwa katika kipindi cha miezi 24 kuanzia tarehe ya kuanza mradi ambayo ni tarehe  3 september 2024 hadi tarehe 3 september 2026.

Novatus Lyimo meneja Mradi wa umeme kutoka kampuni ya M/S  Dieynem  Company Ltd amesema wamekwisha anza utekelezaji  wa awali wa mradi huo  kwa maana ya usanifu na ndani ya muda mfupi timu ya utekelezaji itakua tayari kwa ajili  ya kuanza utekelezaji wa mradi huo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages