TPF NET YATOA MSAADA WA VIFAA TIBA ZAHANATI YA POLISI KATAVI.

 

Jeshi la polisi Mkoa wa Katavi likiongozwa na SACP Kaster Ngonyani wakati wa ugawaji wa vitendea  kazi katika zahanati ya Polisi Mkoa wa Katavi

Na Daniel Kimario -KATAVI

Katika kuadhimisha kilele cha siku 16 za kupinga ukatili, Mtandao wa Polisi Wanawake (TPF Net) Mkoa wa Katavi kwa kushirikiana na Dawati la jinsia na watoto wametoa msaada wa vitendea kazi na vifaa tiba katika zahanati ya Polisi Mkoa wa Katavi. 




 

Akikabidhi vifaa hivyo Desemba 10, 2024 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Kaster Ngonyani amebainisha kuwa Mtandao wa Polisi Wanawake umetoa vitendea kazi hivyo ili kurahisisha  utendaji kazi na kuongeza chachu katika utoaji huduma kwa wagonjwa wanaohudumiwa na Zahanati hiyo. 



Akizungumza baada ya kupokea msaada huo Mkuu wa kikosi cha Afya Mkoa wa Katavi Mkaguzi Msaidizi wa Polisi (A/INSP) Dr. Denis Wambura ameushukuru Mtandao wa Polisi wanawake Mkoa wa Katavi kwa kuguswa kutoa vifaa tiba hivyo ambavyo vitaraisisha utoaji huduma bora kwa wagonjwa wanaofika kupata huduma za kiafya katika zahanati hiyo. 

 

Vitendea kazi na vifaa tiba vilivyokabidhiwa ni pamoja na mzani wa kupima urefu na uzito, kiti cha maguruduma cha kubebea wagonjwa pamoja na vifaa mbalimbali vya kufanya usafi.

           MWISHO

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages