KAMPUNI YA PREMIUM ACTIVE TANZANIA YATOA MADAWATI WILAYA YA MLELE

Nicco Roussos Meneja Shughuli kutoka Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA LIMITED kushoto akikabidhi Dawati kwa Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Mlele katika juhudi za kiunga mkono serikali katika sekta ya Elimu .

Na Walter Mguluchuma -Katavi

Kampuni ya ununuzi  wa zao la Tumbaku  ya PREMIUM ACTIVE  TANZANIA LIMITED  limekabidhi  msaada wa    madawati  136 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele  yatakayo saidia  kupunguza  tatizo la wanafunzi kusoma wakiwa wamekaa chini ikiwa ni sehemu ya Kampuni  hiyo  kurudisha   sehemu ya faida yake  kwa jamii kuchangia maendeleo .

Muonekano wa Madawati 1000 yaliyotolewa na Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA Mkoa wa Katavi kwenye maeneo yanayolima zao la  Tumbaku ikiwa ni sehemu ya faida wanayoipata kurudisha kwenye jamii..

Kampuni ya ununuzi  wa zao la Tumbaku  ya PREMIUM ACTIVE  TANZANIA LIMITED  limekabidhi  msaada wa    madawati  136 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele  yatakayo saidia  kupunguza  tatizo la wanafunzi kusoma wakiwa wamekaa chini ikiwa ni sehemu ya Kampuni  hiyo  kurudisha   sehemu ya faida yake  kwa jamii kuchangia maendeleo .

Msaada huu umekabidhiwa  na  Meneja   Shughuli  wa Kanpuni ya Premium Tanzania Nicco  Roussos kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele katika  hafla iliyofanyika katika shule ya Msingi Igombe  msaada huo  ulipokelewa  na   Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo  Beatrice  Rumbeli

Roussos amesema  lengo la utoaji wa  mchango huo  wa  Kampini  ya PREMIUM ni  kurudisha  sehemu  ya  faida wanayopata   kwa maendeleo ya jamii  katika maeneo ambayo  wanafanya  shughuli  za  ununuzi wa zao la Tumbaku .

Nicco Roussos Meneja Shughuli kutoka Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA akielezea namna Kampuni hiyo inavyo shirikiana na serikali kuinua elimu kupitia zao la Tumbaku.
Amebainisha kuwa  hiyo ni moja ya Sera za  Kampuni ya  Premium  Active  Tanzania  kurudisha  sehemu ya faida   yake  kwa jamii  kwa kuchangia  maendeleo  katika  maeneo ya  Elimu , Afya , Maji  Mazingira na uongozi    na  mchango ambao wamekuwa wakiutowa kwenye jamii  unategemea na uzalishaji wa sehemu husika  walivyozalisha Tumbaku kwa msimu huo .

Kwa kuzingatia  uzalishaji  wa msimu wa kilimo  2024 Kampun  imeweza  kutoa kiasi hicho cha  madawati  136kwa Halmashauri hiyo ya Mlele  yenye thamani ya  tshs  9,520,000 kati ya madawati  1000 yatakayo   gawa kwenye maeneo wanayonua tumbaku ya  Wilaya za  Tanganyika ,Mpanda , Chunya , Songwe  yatakayo tumia kiasi cha Tshs   71.070,000.

Amevitaja vijiji  ambavyo vimenufaika  katika Halmashauri hiyo kuwa ni  Wachawaseme wamepata dawati  34,Mgombe dawati  34,Kamsisi  34 na  Inyonga  34.

Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Igombe Halmashauri ya Wilaya ya Mlele wakiwa darasani waliopatiwa msaada wa Madawati na Kampuni ya PREMIUM ACTVE TANZANIA.
Amesema  mbali ya   utoaji huo wa madawati katika maeneo mengine wanayonunua tumbaku wameweza pia kutoa  vingine  kama vile  Computer  , photocopies  , printers, executive ,tables  executive  chairs,Aluminun Windows cements na  office  cabinets  zenye  thamani ya  tshs  112 , 469,890.

Roussos  amesema  utoaji wa vifaa hivyo  unazingatia  maombi ya  wanufaika  pamoja na fedha inayokuwa imetengwa  kutokana na  uzalishaji wa wilaya  husika   au  kata  husika   hivyo wanaendekea kusisitiza   uzalishaji  bora wa  wakulima  ambao utakuwa na tija  kwa jamii na wakulima  pia  wanasihi wakulima  waendelee kutunza  mazingira kwa kupanda miti  na kuboresha majiko yanayotumia  kuni kidogo  za  matawi.

Meneja  shughuli na Mhusiano wa  Kampuni ya Premium Yusuph  Mahundi  amesema  msaada huo waliootowa ni sehemu ya kampuni yao katika kuisaidia Serikali   kwenye maswala ya kuisadia Serikali  kwenye maswala ya maendeleo ya jamii .

Ameeleza kuwa  kwenye  Halmashauri hiyo ya Wilaya ya Mlele  kampuni  hiyo inafanya kazi na vyama  vitatu vya Msingi katika ya vyama  50 wanavyofanya navyo kazi hapa  nchini  pia  pamoja   na  madawati hayo pia wanatowa ushuru   kwenye Halmashauri katika maeneo yote wanayonunua tumbaku  ambazo ni zaidi ya Dola 107 000 na kwa Mkoa wa  Katavi wanalipa zaidi ya Dola  6,000  kwenye   halmashauri  zinazolima Tumbaku .

Kaimu Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Wilaya ya Mlele  Beatrice Rumbeli amesema    msaada huo wameopokea  kwa mikono miwili na wataendelea kuiinga  mkono kampuni hiyo kwa jitihada zake kubwa za kutunza mazingita

Kaimu  katibu  Tawala wa Wilaya ya Mlele  Geofey Uwahanja  amesema  tatizo la upungufu wa   madawati lipo  karibu kwenye maeneo ya Halmashauri zote mbili za Wilaya hiyo hivyo Kampuni hiyo isisite tena kutowa msaada kama huo.

Kaimu  afisa elimu   elimu ya  Msingi wa  Wilaya  ya Mlele  Peter  Nyamafu   ameeleza kuwa  kampuni isiwachoke kwani Halmashauri  hiyo inaupungufu wa  madawati 4524 hivyo upingufu bado ni mkubwa  hivyo wanawaomba wawaongezee tena  ili  wawaweze kupunguza upungufu uliopo .

Amesema  vilevile wanaonba wasaidiwe vitu vingine  kwani  kwenye swala la elimu bado kuna vitu vingine  vinahitajika kama vile  madarasa  na matundu ya vyoo.        

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages