Stewart Kiondo Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi akisoma repoti ya utendaji kazi ya kipindi cha miezi mitatu kuanzia Oktoba mwaka jana hadi mwezi Desemba 2024.
Na Walter Mguluchuma, Katavi
Taasisi ya
Kuzuia na Kipambana na
Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi imefanikiwa
kuokoa kiasi cha zaidi ya
shilingi Milioni 90 za chama
cha Msingi Ilangu cha Wakulima wa Tumbaku Wilaya ya Tanganyika
Mkoani Katavi .
Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi Stewart Kiondo amewaambia wandishi wa Habari wabari wakati alipokuwa akitowa taarifa ya utendaji kazi ya kipindi cha miezi mitatu ya kuanzia Oktoba mwaka jana hadi mwezi Desemba.
Amesema
Takukuru Mkoa wa Katavi katika
majukumu yake katika eneo la uzuiaji wa
Rushwa na ufatiliaji wa
miradi ya Maendeleo imefanikiwa
kuokoa kiasi cha
Tshs 91,000,000 za chama
cha Msingi Ilangu AMCOS
kilichopo katika Wilaya ya Tanganyika .
Amebainisha
kuwa Takukuru Mkoa wa Katavi walipata
malalamiko juu ya ubadhilifu
wa mbolea aina ya NPK katika
chama cha Msingi cha wakulima wa
Tumbaku Ilangu kinachoshirikiana na
chama kikuu cha LATCU katika kufanya shughuli zake
za ushrika ,
Kiondo amesema
kwenye Amcos walitakiwa
kupokea mifuko ya mbolea 9500 lakini waliweza kupokea mifuko 8879 kukiwa na upungufu wa mifuko 621 ya
mbolea ya Npk inayotumika kwenye zao la Tumbaku yenye thamani ya tshs
91,000,000 ilichukuliwa na viongozi wa AMCOS ya Ilangu kwa kushirikiana na mtumishi mmoja asiye
mwaminifu wa LATCU .
Baaada ya ufatiliaji wa
Takukuru waliweza kubaini
kuwa kampuni ya NGESACO SERVICE
LIMETED ndio waliolipwa fedha
hizo na
kufuatia kubainika kwa kampuni hiyo kulipwa fedha hizo ambazo
hawakusitahili waliwataka warudishe
fedha hizo.
Ndipo kampuni
hiyo ilipoweza kurejesha kiasi cha
tshs 59,150,000 ambapo mwenyekiti wa Ilangu Amcos nae aliweza kurejesha kiasi cha Tshs 31,850,000 kwa Takukuru zikiwa
ni fedha za Ilangu Amcos
na kufanya fedha zilizo okolewa
kuwa ni tshs 91 000,000 licha ya kurudishwa
fedha hizo Takukuru bado
wanaendelea na uchunguzi wa fedha
hizo ambazo zilikuwa zikichepushwa kwa manufaa binafsi .
Kiondo amesema
katika kipindi hicho
wameweza kufatilia miradi 27 yenye
thamani ya Bilioni 7.6 katika sekta za elimu
afya , ulinzi na usalama
na maendeleo ya jamii katika
miradi hiyo kuna baadhi
wamebaini inachangamoto ambayo
imesababisha miradi kukamilika kwa wakati .
Hivyo
Takukuru wanaendelea kufanya uchunguzi
juu ya hayo waliyoyabaini kwenye miradi hiyo ikiwa ni
kuwepo na manunuzi hewa
ya thamani madawati 50 pamoja na
matofali yenye ubora
kwenye baadhi ya shule za
msingi zenye miradi
hiyo .
Kuhusu
malalamiko ya Rushwa wameweza kupokea jumla ya malalamiko 34 kati
ya malalamiko hayo
taarifa za rushwa zilikuwa
ni 21
na zisizo za rushwa
ni 13 na yalihusisha sekta za uhamiaji , Serikali za mitaa , ardhi , biashara maliasili na Polisi
.
Aidha Takukuru Mkoa wa Katavi wamewakunbusha wananchi wa mkoa huu kuendelea kutowa taarifa za vitendo vya Rushwa pindi wanapokuwa wameona vinapokuwa vinataka kutokea au kutokea kwa kutowa taarifa kwenye Taasisi hiyo ili waweze kuchukua hatua kwa haraka.