MAKAMPUNI YA TUMBAKU YATAKIWA KUIGA MFANO WA PREMIUM ACTIVE TANZANIA

Nicco Russos [kulia]Meneja wa Shuguli kutoka PREMIUM ACTIVE TANZANIA akimkabidhi Madawati Lincolin Tamba [kushoto] Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika

 Na Walter Mguluchuma-Katavi

Uongozi wa Serikali ya Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi wameyaomba Makampuni ya ununuzi wa zao la Tumbaku kuiga mfano wa Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA ya kurudisha sehemu ya faida yao kwenye Jamii kwaajili ya kuchangia maendeleo kama inavyofanya Kampuni hiyo.

Uongozi wa Serikali ya Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi wameyaomba Makampuni ya ununuzi wa zao la Tumbaku kuiga mfano wa Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA ya kurudisha sehemu ya faida yao kwenye Jamii kwaajili ya kuchangia maendeleo kama inavyofanya Kampuni hiyo.

Wito huo umetolewa na Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Lincolin Tamba ambae ni Katibu tawala wa Wilaya hiyo ya Tanganyika  aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya kwenye hafla ya kukabidhiwa Madawati 456 kutoka Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA kwaajili ya Halmashauri ya Wilaya hiyokwenye maeneo wanayolima zao la Tumbaku.

Amesema kuwa Wilaya hiyo imepokea Madawati 456 kutoka Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA ikiwa ni sehemu ya kurudisha sehemu ya faida yao kwenye Jamii kwaajili ya kuchangia maemdeleo hususani kwenye sekta ya Elimu.

Lincolin Tamba Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika ambae pia ni Katibu Tawala Wilaya ya Tanganyika akitoa neno la Shukrani kwa Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA kwa msaada wa Madawati 456.

Amebainisha kuwa madawati hayo yenye Thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 31 ambazo siosehemu ya tozo wala ushuru.

Amesema Vijiji vitakavyo nufaika na Madawati hayo nipamoja na kijiji cha Isubangala,Busongola,Majalila,Isenga,Lugufu,Isungwe,Kabanga,Kamjela,Igagala,na Kabungu ambavyo kwa sehemu kubwa vinajihusisha na kilimo cha zao la Tumbaku.

Amesema kuwa Tumbaku inayozalishwa katika Wilaya ya Tanganyika kwa asilimia tisini imekuwa ikinunuliwa na Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA na ndio wanunuzi wakubwa wa zao hilo kwenye wilaya hiyo kwani katika vyama Tisa vya Msingi vinavyozalisha zao la Tumbaku imeonekana kampuni hiyo hufanya kazi na vyama 8 vya Msingi namatokeo yake yanaonekana kwa kupatiwa Madawati hayo 456.

Tamba ameeleza kuwa kwa kipindi cha Mwaka jana Halmashauri hiyo ilipata ushuru unaotokana na zao la Tumbaku zaidi ya Milioni 800 ambazo zilitumika katika Shughuli mbalimbali za maendeleo kwenye Wilaya hiyo.

Amemshukuru Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kutengeneza mazingira wezeshi kwa Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA  kufanya shughuli zake katika Wilaya hiyo bila kikwazo cha aina yeyote.

Amesema Halimashauri hiyo inaupungufu mkubwa wa Madawati hivyo Madawati hayo 456 yatakwenda kupunguza tatizo la uhaba wa Madawati kwa kaiasi frani yatakwenda kupunguza uhaba huo na hawajapokea Madawati tu bali wamepokea madawati mazuri na yenye ubora yaliyotengenezwa kwa kiwango.

Amewahakikishia Kampuni hiyo kuwa serikali ya Wilaya hiyo itaendelea kuwapa ushirikiano zaidi na kuhamasisha uzalishaji wa zao hilo kwa wakulima wa Wilaya ya Tanganyika .

Hivyo ameomba Makampuni mengine ya ununuzi wa Tumbaku kuiga mfano mzuri ulionyeshwa na kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA kwa kutoa msaada huo wa Madawati 456 kupitia sehemu ya faida .

Kwa upande wake Nicco Russos Meneja wa Shughuli Kutoka PREMIUM ACTIVE TANZANIA amesema kuwa mwaka huu 2025 Kampuni hiyo imetoa Madawati 456 ambayo yanathamani ya shilingi Milioni 31920,000 kwa Wilaya ya Tanganyika kwa mkoa mzima wa Katavi wametoa Madawati 1000 yenye Thamani ya zaidi ya shilingi Milioni 71.

Russos amewasihi wakulima kuendelea kupanda miti kwaajili ya kuboresha mazingira na kutumia yanayotumia kuni kidogo kwaajili ya kukaushia zao la Tumbaku.

Meneja shughuli  na mahusiano Yusuph Mahundi amesema katika Wilaya ya Tanganyika kwa msimu uliopita walifanya kazi na vyama vya Msingi 9 kwa msimu huu wanafanya kazi na vyama vya msingi 8 kati ya vyama 50 vya msingi wanavyofanya navyokazi hapa nchini.

Amesema Wilaya ya Tanganyika kwa Kampuni hiyo ni Wilaya ya Kipekee kwa kwa sababu kwa Mkoa wa Katavi Tanganyika inazlisha ya nusu ya Tumbaku inayozalishwa Mkoa wa Katavi na wanaiangalia kwa jicho la pekee.

Mahundi amesema kuwa kwenye eneo la ulipaji wa ushuru mwaka huu Kampuni hiyo imelipa zaidi ya Dola 342000 za kimarekani kati ya Dola zaidi ya Laki sita zinazolipwa kwa Mkoa wa Katavi.

Amewahakikishia Wakulima wa zao la Tumbaku kwa Mkoa wa Katavi kuwa sehemu hiyo waliyoitoa wataendelea kutoa kila mwaka kama ambavyo wamefanya mwaka huu.

Ojungu Sabaya Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika amesema Halmashauri hiyo inaupungufu wa Madawati 25000 kwa msaada huo waliowapatia niwakipee kwani utakwenda kupunguza upungufu wa madawati na wameisadia serikali.

Sabaya ameendelea kuwaomba isiwe mwisho hapo bali wasaidie kwenye miundombinu mingine kama sera yao inavyosema.

Sadam Juma Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Mpanda ndogo amesema wanashukuru kwa msaada huo kutoka Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA na kuahidi kusoma kwa bidii.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages