Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akitoa taarifa ya uzinduzi wa Kampeini ya Msaada wa Kisheria kwa Mkoa wa Katavi inayojulikana kama Samia Legal Aid Kampeini |
Na Walter Mguluchuma-Katavi
Wananchi wa Mkoa wa Katavi
wanatarajia kunufaika na huduma ya msaada wa Kisheria wa Mama Samia (LEGAL AID KAMPEINI) itakayotolewa kwenye maeneo ya Halmashauri zote tano zilzopo katika Mkoa wa Katavi pasipo malipo ya aina yoyote .
Wananchi wa Mkoa wa Katavi wanatarajia kunufaika na huduma ya msaada wa Kisheria wa Mama Samia (LEGAL AID KAMPEINI) itakayotolewa kwenye maeneo ya Halmashauri zote tano zilzopo katika Mkoa wa Katavi pasipo malipo ya aina yoyote
Mkuu wa Mkoa wa Katavi
Mwanamvua Mrindoko amesema
uzinduzi wa huduma hizo za
msaada wa kisheria utafanyika
Januari 24 katika uwanja wa shule ya msingi Kashaulili uliopo katika Manispaa ya Mpanda .
Amebainisha kuwa kampeni hiyo ya Mama
Samia itafanyika kwa muda wa siku
kumi siku hiyo ya tarehe 24 itakuwa ni siku ya uzinduzi
na baada ya hapo kazi itafanyika katika maeneo yote ya Halmashauri
za Mkoa wa Katavi.
Lengo la Kampeni hii ambayo Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ameridhia ifanyike ni
pamoja na kuhakikisha kwamba wananchi
wasio na uwelewa wa kisheria
wanapata uelewa kuhusu mambo ya
kisheria na pia itahusika na utatuzi wa changamoto mbalinbali za kisheria
ambazo wananchi watakuwa wanaziwasilisha
kwenye timu za wanasheria wasaidizi watakao kuwa wanafanya kazi hiyo ,
Mrindoko amesema kampeni hiyo
itakuja kutowa msaada wa kisheria kwa
wananchi ndani ya Mkoa wa Katavi na kuwafanya
wananchi waweze kupata haki zao za msingi za kisheria kwa kufuata
maelekezo na taratibu .
Amefafanua kuwa kampeni hii inakauli mbiu inayosema MSAADA WA SHERIA KWA
HAKI USAWA AMANI NA MAENDELEO na kauli mbiu hii inaashiria kulinda
na kutetea haki za wanyonge na
kupinga uvunjaji wa haki za Binadamu na
kuelewesha wananchi misingi ya utawala bora na kupinga ujatili wa
kijinsia pamoja na kuendelea kuwaelimisha wananchi kutii sheria na ueawala
bora .
Mkuu wa Mkoa Mrindoko amemshukuru Rais Samia kwa kuridhia
kufanyika kwa kampeni hii katika Mkoa wa Katavi ambapo kwenye kila Halmashauri itafanyika
kwenye Kata kumi na vijiji kumi kwenye kila Halmashauri kwa maana hiyo kwa Mkoa huu itafanyika kwenye
Kata 45, mitaa 26 na vijiji 114 kwa mkoa
mzima wa Katavi