Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akiwahutibia wananchi wa Mkoa wa Katavi wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria inayojulikana kama Samia Legal Aid Campeing |
Mkoa wa Katavi umezindua kampeni ya siku kumi ya
msaada wa kisheria wa Mama Samia inayotekelezwa Tanzania Bara na
Zamzibar yenye lengo ya kulinda, kukuza na upatikanaji wa haki kwa
watu wote kupitia huduma ya msaada wa kisheria
hapa Nchini .
Mkoa wa Katavi umezindua kampeni ya siku kumi ya msaada wa kisheria wa Mama Samia(MSLG) inayotekelezwa Tanzania Bara na Zamzibar yenye lengo ya kulinda, kukuza na upatikanaji wa haki kwa watu wote kupitia huduma ya msaada wa kisheria hapa Nchini .
Uzinduzi huo umefanyika katika uwanja wa
shule ya Msingi Kashaulili na umezinduliwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi
Mwanamvua Mrindoko na huduma hiyo itatolewa na wanasheria wa
kutoka Wizara ya sheria na Katiba ,wanasheria wa Halmashauri
mawakili wa kujitegemea na wasaidizi wa kisheria .
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba
Franklin Rwezumula amewaambia wananchi wa Mkoa wa Katavi na
Watanzania kwa ujumla wakati wa uzinduzi huo kuwa Wizara ya
Katiba na sheria inatekeleza kampeni hiyo kwa mujibu wa ibara ya 13
ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayotamka usawa
mbele ya sheria na utekelezaji wa msaada wa kisheria yam waka
2017 ambapo inatowa mwongozo wa utoaji wa msaada wa kisheria kwa
wananchi wote wasiokuwa na uwezo .
Amee;eza uzinduzi wa kampeni hii ilizinduliwa
na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassimu
Majaliwa mwaka 2023 Mkoani Dodoma na utekelezaji wa
kampeni hii sasa umefika katika mikoa 11 na kwenye
kampeni kama hiyo ilizinduliwa Mkoani Katavi
itazinduliwa katika mikoa sita na kufanya mikoa itakayokuwa imefikiwa
kuwa 17
Utekelezaji wa Kampeni hiyo unaenda sambamba na
utoaji wa elimu wa Uraia na utawala bora kwa viongozi wa
ngazi mbalimbali wakiwemo wajumbe wa kamati za usalama za Mikoa
wilaya wakuu wa vitengo vya vivisheni wa mikoa na Wilaya na
watendaji wote wa Kata wa Mikoa yote ambayo itafikiwa na
kampeni .
Rwezumula amebainisha kuwa malengo ya mkakati huu ni
pamoja na kuwajengea uwezo washiriki kuhusu haki na
wajibu wao kikatiba na kuwaongezea uwelewa washiriki
kwenye maswala ya uraia , haki za binadamu misingi ya utawala bora na
demokrasia na katika kuhakikisha kuwa
uendelevu wa huduma za msaada wa kisheria Wizara imeanzisha
madawati ya msaada wa kisheria katika Halmashauri zote
nchini .
Amesema madawati hayo kwa kushirikiana na mashirika ya utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria na wasaidizi wa kisheria chini ya wasajiri wasaidizi ngazi ya Mkoa na Halmashauri yataendelea kutowa huduma hata baada ya kumalizika kwa kampeni hiyo amemwomba mkuu wa Mkoa kuendelea kuwapa ushirikiano ili waweze kuwafikia wananchi kwa wakati .
Baada ya uzinduzi huo kampeni hiyo kwa Mkoa wa Katavi itaendelea
hadi tarehe mbili mwezi wa pili 2025 na lengo la Wizara
ya Katiba na sheria ni kuzifikia Halmashauri zote na kila
halmashauri watazifikia kata kumi na kila kata
watafikia vijiji au mitaa mitatu na timu za wataalamu
zitafika pia kwenye shule za msingi na sekondari na kutowa
elimu ya maswala ya ukatili wa kijinsia haki na
wajibu wa wanafunzi .
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amesema
ni muhimu kwa wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kusimamia
kampeni hiyo kwa ukamilifu ili wananchi waweze kujitokeza kwa wingi na
kuweza kupatiwa msaada huo muhimu wa kisheria .
Mrindoko amesema vema kwa wananchi wa Mkoa wa
Katavi wakatumia vizuri nafasi hiyo ya kampeni ya msaada wa
kisheria ili kuwa na uwelewa mpana zaidi katika maswala
yanayohusu sheria na kuweza kutetea haki zao za msingi na
kupinga ukiukwaji wa haki za binadamu na pia kuimalisha maswala ya
utawala bora .
Amasema kama ambavyo Wanzania wanavyofahamu Rais
Samia Suluhu Hassan adhima yake ya kukuza na kutetea
wanyonge na kupinga uvunjaji wa haki za binadamu na pia
kuimarisha misingi ya utawala bora kuepukana na kuelimika
kutokana na maswala ya kijinsia na kuimiza kuheshimu sheria
na utawala katika ngazi zote na kwa kila mwanamchi wa
Tanzania .
Ameeleza kuwa Rais amekuja na kampeni yake ya
R4 ambayo inahusisha maridhiano usitahimilivu
mageuzi pamoja na kujenga upya misingi ya sheria na
utawala bora na haki za binadamu katika nchi yetu ya
Tanzania hivyo ni vema msaada huu wa kisheria
ukawafikia wananchi kwa kupata elimu inayohusiana na sheria .
Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge
utawala Katiba na Sheria Boniface Butondo ameushukuru
uongozi wa Mkoa wa Katavi kwa jinsi walivyojipanga vizuri na kuhakikisha
kampeni hiyo ya msaada wa kisheria kisheria inafanikiwa vizuri kutokana
na maandalizi yao mazuri waliofanya .
Amesema pamoja na jitihada za maendeleo zinazofanywa
na Rais Samia maendeleo yamekwenda yamefika kila mtaa na kijiji
lakini Rais akasema hapana jambo la kisheria ni
la msingi sana ndio maana akaona ni lazima kuanza
jitihada kubwa sana za kuhakisha umma wa Watanzania
wanaanza kupata elimu na ufahamu juu ya mswala mbalimbali ili
waweze kuwa na haki ya kutetea haki zao za msingi
Salome John Mkazi wa Manispaa ya Mpanda ameishukuru Serikali kwa kuona umuhimu wa kuwaletea huduma hiyo muhimu mpaka kwenye maeneo ya kwenye mitaa na kwenye vijiji,