TUME YA RAIS YA MAREKEBISHO YA KODI YAKUTANA NA WADAU KATAVI.

 

   Balozi Mwanaid Maajar Kamishina wa Kamisheni ya Tume ya Rais ya maboresho ya kodi akitoa maelezo mafupi namna ambavyo Tume inavyo sikiliza kero na maoni juu ya maboresho ya kodi.

 Na  Walter Mguluchuma, Katavi

Tume ya Rais  ya  Marekebisho  ya Kodi imekutana na wafanya bishara na wadau mbalimbali  wa Mkoa wa Katavi  na  kupokea  kero mbalimbali zinazo wahusu wafanya biashara  na ushauri wa njia  bora ya ikusanyaji wa mapato yatokanayo  na  kodi .

Kikao hicho kilichowashirkisha  wadau hao wa  Mkoa wa Katavi  kilifanyika  katika ukumbi wa  Halmashauri  ya  Manispaa ya Mpanda na kiliongozwa na Balozi  Mwanaid  Maajar  Kamishina wa Kamisheni wa Tume ya Rais ya Maboresho ya Kodi   ambapo  mgeni rasmi kwenye kikao hicho  alikuwa ni Mkuu wa Mkoa wa Katavi  aliyewakilishwa na  Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu.

   Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa ambae ni Mkuu wawilaya ya Tanganyika Onesimo Buswelu akifungua kikao cha tume ya Rais ya Maboresho ya kodi kilicho washirikisha wafanyabiashara na wadau mbalimbali 

 

Akizungumza na wadau hao  Balozi  Maajar amesema  kumekuwepo  malalaniko mengi kwa  walipa  kodi  kuhusu kero  zinatokazo na mfumo wa  walipa kodi  wanaodai  kuwepo kwa utitili  wa tozo mbambali  na taasisi zinazokusanya kodi .

Amebainisha kuwa kwa hapa  nchini   mchango wa ukusanyaji wa kodi  upo chini sana  ukilinganisha na  nchi za Afrika Mashariki  kwa kuona  hivyo  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt  Samia Suluhu Hassan  akaona  ni vyema kuunda tume  yenye  Makashina tisa  ili  kuweza  kuwafikia wafanya biashara  katika maeneo mbalimbali hapa  nchini .

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu  ameiomba Tume hiyo ya Rais ya  Maboresho ya Kodi  ichukue     kero na mapendekezo  yalitolewa na wafanya  biashara na wadau wengine walioshiriki kwenye kukao hicho na  kuzifikisha kwa Rais ili ziwezekufanyiwa  utatuzi.

Baadhi ya washiriki wa kikao cha tume ya Rais ya maboresho ya kodi na wafanyabishara na wadau wakifuatilia kwa kalibu kikao hicho katikati Mkuu wawilaya ya Mlele Majidi Mwanga

Amesema  maboresho ya kodi  yakifanyika kwa wafanyaniashara wa Katavi kutasaidia  kulipa  kodi  na kuleta maendeleo kwenye Mkoa  na   nchi kwa jumla    kutokana na  furusa nyingi za uwekezaji zilizopo katika Mkoa  wa Katavi .

Mwenyekiti wa  Jumuia yaWafanya biashara    Tawi la     Mkoa wa Katavi  Amani Mahella  amesema ni ukweli usiopingika  kuwa kumekuwepo   na  utitiri wa tozo  kwa wafanya   biashara  hali  ambayo imekuwa ikipelekea watu ambao wanataka kufungua biashara  kukata tamaa na kushindwa kufungua biashara .

Ameeleza kuwa  kodi ya  thamani  imekuwa ni changamoto kubwa   kwa baadhi ya wafanya biashara kama wa  hotel ambao wateja wao wanakonunua bidhaa kama kuku ,viongo  na  matunda   ni wafanya biashara wanao uza bila kuwapatia risiti


 
Anna Nchagwa mwakilishi wawatu wenyeulemavu akiwasisilisha ombi kwa serikali kupunguza kodi ya vifaa vya watu wenye ulemavu ili viweze kuuzwa kwa bei rafiki.

Mwenyekiti  wa  Jumuia ya  Wafanya  biashara Wilaya ya Mlele  Sebastian Haule  amesema  mashine za  EFD zimekuwa sio  rafiki kwa wafanya  biashara   hivyo ameiomba Serikali kupitia kwa wataalamu wake kukaa na kufikiria upya   njia ya kutengeneza mashine zitakazokuwa zinahesabu pesa itaweza kusaidia  kuwabana wafanya biashara wanao kuwa wanatoa taarifa zao ili kukwepa kodi .

Mkuu wa Wilaya ya  Mlele  Majid Mwanga  alishauri kuwepo na   utoaji wa leseni kwa  viwango tofauti kwa wale wanatumia vyombo  vya moto kuendesha  kwa  starehe  leseni zao za udereva ziwe juu itasaidia kuongeza   mapato zaidi ya Serikali.

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages