KATAVI WAANZA MKAKATI WA KUTEKELEZA AGIZO LA RAIS

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizumgumnza na watendaji mbalimbali wa Mkoa wa Katavi wakati wa uzinduzi wa Mpango mkakati wa kukabiliana na udumavu.

Na Walter Mguluchuma-Katavi

Mkoa wa Katavi  umeanza kufanya jitihada  ya kuhakikisha  tatizo la  lishe duni  linatokomezwa  huo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais alilolitoa  kwa viongozi wa Mkoa  wa Katavi wakati wa ziara yake  aliyoifanya katika Mkoa huo Julai Mwaka jana .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko[kulia]akimkabidhi mpango mkakati wa kukabilina na udumavu  Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Albert Msovela 

Mkoa wa Katavi  umeanza kufanya jitihada  ya kuhakikisha  tatizo la  lishe duni  linatokomezwa  huo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais alilolitoa  kwa viongozi wa Mkoa  wa Katavi wakati wa ziara yake  aliyoifanya katika Mkoa huo Julai Mwaka jana .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko  amesema kuwa katika kuhakikisha  wanatekeleza  agizo la Rais   Mkoa huo  umezindua  rasmi  kazi ya  mkakati wa  kutokemeza  tatizo la  udumavu  nakuimarisha hali ya lishe  kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi

Uzinduzi wa mkakati huo umezinduliwa  na Mkuu wa Mkoa wa Katavi katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi na  uliudhuliwa na viongozi wa  kutoka Halmashauri zote tano za Mkoa wa  huu,viongozi wa madhebu ya dini, vyama vya siasa ,  viongozi wa  kimila ,wazee  maarufu na wadau mbambali  waliko katika mkoa  wa Katavi .

Amesema Mkoa wa Katavi ni  miongoni  mwa mikoa ya  Nyanda za juu  kusini ambayo inauzalishaji mkubwa  wa  vyakula   mbalimbali   ambavyo vikichanganyika tunapata lishe bora   ila kwa bahati mbaya  ukuwepo na Mkoa wa Katavi  inakabiliwa  na kiwango kikubwa cha  udumavu .

Mrindoko  amesema lengo walilonalo ni kuondoa kabisa tatizo hilo kama ambavyo walivyoagizwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan  wakati wa ziara yake aliyoifanya hapo mwaka jana  katika Mkoa wa  Katavi hapo Julai 24 mwaka jana .

 Amesema wameanza safari kwa kuzindua   mpango mkakati wa  utekelezaji wa kazi ya  kutokemeza  udumavu  na lishe mbaya  ambapo hivi karibuni walikwenda Mkoani Njombe  kujifunza  jinsi mkoa huo unavyo fanya juu ya  kupunguza tatizo la udumavu na lishe  mbaya .

Amesema wamezindua kamati maalumu ambayo itakuwa inafanya kazi kila siku  mpaka ambapo watakapokuwa wamehakikisha udumavu  umetokomezwa kabisa katika Mkoa huu  kwa maana hiyo kila mmoja na kwa kila mdau  watambue kuwa wanayokazi ya kufanya  ya  kutoa ushirikiano wa kumaliza tatizo hilo .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi amemwagiza  Katibu Tawala wa Mkoa huo   kuanza kuwabainisha wadau  wa ndani na  nje ya nchi  watakaoweza kusaidia  upatikanaji wa  fedha  za uwendeshaji  wa mpango mahususi wa kuondokana na tatizo hilo .

Katibu Tawala wa Mkoa wa  Katavi  Albert Msovela  alisema  wakati wa ziara ya Rais mwaka jana aliwaagiza waende wakajifunze kwa wenzao wa Njombe  jinsi walivyoweza  kufanya mikakati ya  kupambana na hali ya udumavu  na timu hiyo iliongonzwa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi.

Alieleza  kuwa kutokana na ziara hiyo wameweza  kujifunza namna ya kupambana kutokomeza   tatizo hilo na ndio maana  kama  mkoa wameanza utekelezaji kwa kuzindua mkakati wa kutokomeza  tatizo hilo  kwa wananchi .

Na  Mzee  Maarufu  Vicenti Nkana amesema kuwa  tatizo la  udumavu  kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi limekuwa likichangiwa na tabia ya wananchi kupenda kula  mlo wa chakula cha aina moja .

Ameshauli  Halmashauri za  mkoa huu  kuanzisha sheria ndogo  ambayo itamtaka  kila mtu  mwenye nyumba kupanda miti ya  matunda mitano .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages