Mpanda-Katavi.
Na Mwandishi wetu
Wananchi katika Halimashauri ya
Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wameilalamikia mamlaka ya barabara za mjini na
vijijini (TARURA) kuzibua mitaro na kuhamishia udongo kwenye nyumba zao.
Wakipaza sauti kwa vyombo vya
habari wananchi wa mtaa wa Sokoine Kata ya Kashaulili Manispaa ya Mpanda Katavi
wamesema changamoto hiyo uwenda ikapelekea maafa makubwa kama kubomokewa nyumba zao kutokana na mvua
zinazo nyesha .
Idd Mvano Mkazi wa mtaa Sokoine kata ya Kashaulili ametaja kukumbana na changamoto ya njia wakati wa kuingia
na kutoka nyumbani kwake kutokana na njia kuzibwa na udongo unao tolewa kwenye
mitalo na kuwekwa pembeni mwa nyumba.
Katika hatua nyingine Zuber
Maulidi ambae pia ni mkazi wa wa maeneo hayo ameioba (TARURA) kuchukua hatua za
haraka kuondoa udongo uliopo katika nyumba zao na kutoa elimu kwa wakandarasi
wanao zibua mitaro ili wananchi waweze kuepuka changamoto hizo.
Nao baadhi ya wananchi wa Mtaa wa
Ikulu kawajense wanawaomba TARURA kuona namna ya kufanyia usafi baadhi ya barabara zilizopo
kati kati ya Mji wa Manispaa ya Mpanda kwa
kufyeka nyasi zilizopo pembezoni mwa barabara hali
ambayo imekuwa ikihatarisha
usalama wa watembea kwa miguu na watumiaji wa vyombo vya moto .
Geoge Maiko amaitaja barabara mojawapo ambayo nihatarishi inayo toka baa maarufu ya Waiti Jirafu kuelekea Laiki vyu nimiongoni mwa barabara ambayo ni hatarishi sana kwa watembea kwa miguu na watumiaji wa vyombo vya moto kutokana na barabara hiyo kuwa na nyasi nyingi pembeni mwa barabara hali inayopelekea sehemu inayo tumiwa abayo haina nyasi kuwa ni ndogo hata magari yamekuwa yakipishana kwa shida.
![]() |
Muonekano wa barabara kwa watembea kwa miguu na watumiaji wa vyombo vya moto na watembea kwa miguu iliopo katikati ya mji wa Mpanda. |