WANANCHI WATAKIWA KUSHIRIKI KWA WINGI SIKU YA WANAWAKE.



Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu alie muwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Katavi kwenye uzinduzi wa maazimisho ya siku ya wanawake duniani akitangaza kuzinduliwa kwa maazimisho ya siku ya wanawake duniani mbele ya waandishi wa 


Na Walter Mguluchuma, Katavi.

Wananchi wa Mkoa wa Katavi wa jinsia zote wamealikwa  kushiriki  maadhimisho muhimu ya siku ya Wanawake Duniani  ambayo yatawashirikisha wanawake wote  wa mkoa huo ili kusherekea kwa pamoja na kujiwekea  mikakati  itakayo  wawezesha wanawake kufikia malengo yao ya ustawi wa kiuchumi.

Wito huu umetolewa na Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa  ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu  wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya siku ya wanawake Duniani ambapo kimkao yatafanyika  katika  uwanja wa Kashaulili Manispaa ya Mpanda.

Alisema  maadhimisho  hayo muhimu  yatawashirikisha wanawake wote  na wananchi wa Mkoa huu ili  kuweza  kusherekea  kwa pamoja na kujiwekea mikakati mbalimbali  ili kuweza kufikia malengo ya ustawi wao wa kiuchumi.

Hivyo  wananchi wote, Wadau wa maendeleo , Taasisi za umma na binafsi, Viongozi wa dini na vyama vya siasa  wanaalikwa kwenye maadhimisho hayo.

Buswelu alisema kwenye  maadhimisho hayo  yataambana na shughuli mbalimbali  ambapo baadhi ya shughughuli hizo ni  kufanya  kongamano la wanawake , kuwatembelea watoto walio  kwenye mazingira  magumu na kuwafanyia matendo ya huruma  na kutembelea  mradi wa machinga.


Amefafanua kuwa  mwaka 1977 Umoja wa Mataifa  ulipisha azimio  lililozitaka  nchi wanachama  kila ifaikapo machi 8 kila  mwaka  kufanya maadhimisho haya  ili kuenzi  mchango  wa  mwanamke  katika ujenzi  wa Taifa  husika  kwa Tanzania siku ya mwanamke Duniani  ilianza kuadhimishwa 1997.

Kauli mbiu  ya mwaka huu ni wanawake  na wasichana  2025 tuimarishe  haki  usawa na  uwezeshaji.


Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages