Na Daniel kimario-Katavi
Katika kuelekea
maadhimisho ya siku ya wanawake Dunia yanayotarajiwa kufanyika Kitaifa Machi 8,
mwaka huu Mkoani Arusha Mtandao wa Polisi wanawake (TPF - NET) Mkoa wa
Katavi Machi 4, 2025 wametoa mahitaji ya vitu mbalimbali kwa mahabusu na
wafungwa wa Gereza la Mahabusu Mpanda.
Katika kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake Dunia yanayotarajiwa kufanyika Kitaifa Machi 8, mwaka huu Mkoani Arusha Mtandao wa Polisi wanawake (TPF - NET) Mkoa wa Katavi Machi 4, 2025 wametoa mahitaji ya vitu mbalimbali kwa mahabusu na wafungwa wa Gereza la Mahabusu Mpanda.
Msaada huo umetolewa
kwa niaba ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa
Polisi (SACP) Kaster Ngonyani na Mrakibu wa Polisi (SP) Sanjukila Wagesa
akiambata na wakaguzi pamoja na askari wa vyeo mbalimbali.
Mahitaji yaliyotolewa
ni pamoja na juice, biscuti, kanda mbili, taulo za kike, mchele, mafuta ya
kupaka, pampasi za watoto, nguo za ndani, sabuni ya unga na kipande, dawa za
meno, miswaki na maziwa ya watoto.
|
|