LATCU KUANZA KUFANYA KAZI ZAKE KWA MFUMO WA TEHAMA.

 

Meneja wa Chama Kikuu cha Ushirika (LATCU) Mkoa wa Katavi Pius Kilo.

Na Walter  Mguluchuma, Katavi.

Chama Kikuu cha Ushirika cha  Mkoa wa Katavi(LATCU )kimeanza  kufanya kazi zake kwa  kutumia mfumo wa Tehama na wamejipanga  kuhakikisha vyama  vyote vya Msingi  wanavyovisimamia  navyo viaze  kufanya kazi kwa  kutumia  mfumo wa TEHAMA.

Hayo yamebainishwa hivi karibuni na  Meneja Mkuu wa  Chama kikuu cha  ushirika (LATCU)cha  Mkoa wa Katavi  Pius Kilo, wakati wa nkutano mkuu wa  31 wa  chama  hicho  uliofanyika katika  ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya  Mpanda

Amesema  Dunia  ipo  katika sura za taasisi zote  ziwe    katika  mfumo wa   Kidigitali yaani kwamba shughuli zote ziwe  ni za Kitehama  na wao   kama  LATCU  hawakubaki nyuma  yatari wanao  mfumo  wa Tehama  unao fanya kazi

Hivyo wao  kama  LATCU wanao jukumu  kubwa  la  kuhakikisha vyama vyao  vya msingi vyote wanavyovisinania katika Mkoa wa Katavi  na  vyenyewe  pia  vinakuwa na mfumo wa Tehama .

Amewasisitiza vuongozi wa Amcos na watendaji  kufanya kazi  kwa uaminifu  na uadilifu mkubwa  na sio kuishia hapo  pamoja  na wakulima  wenyewe wanapaswa kuwa hivyo  ili   kuweza  kufanya  madeni yote yanayokopwa  kwenye  mabenki yaweze kulipika yote .

Kilo  ameeleza kuwa  kama wakulima  wasipokuwa waadilifu na waaminifu  kunaweza kusababisha  kushindwa  kurejesha   madeni ya pembejeo  yanayokuwa  wamekopeshwa na  Mabenki kupitia Amcos zao  na wanapo shindwa kukopesheka wakulima wanashindwa kuendelea.

Nae Richald Zengo   Mrajisi Msaidizi anae  simamia vyama  visivyo vya kifedha  kutoka  tume ya maendeleo ya vyama  vya ushirika  wao  kama wasimamizi wao jukumu la kuhakikisha  vyama vyote vya ushirika vina  kwenda  vizuri.

Amesema  bado kuna   baadhi ya vyama viongozi wake wamekuwa sio waadilifu  hivyo  anapenda kuwakumbusha kuwa  hawatasita  kuwachukulia hatua viongozi ambao  watakuwa  hawana uadilifu .

Amesisitiza kuwa sasa hivi wakulima  wanaendea  kwenye  msimu wa  masoko na moja ya uadilifu ni baadhi ya wakulima wa tumbaku wamekuwa wakitorosha tumbaku  yao na wengine wamekuwa hata madeni  hawalipi  hivyo  vuongozi wahakikishe wale wote waliokopeshwa na mabenki  wanalipa ili Amcos ziendelea  kuwa na fisa za kukopesheka .

Ameikumbusha  LATCU  kuhakikisha  changamoto zimazokuwa zinatokea kwenye Amcos  wasishughulikie  mapema  wasibiri mpaka    mrajisi  msaidizi wa Mkoa ndio  ashughulikie .

Kwa upande wake  Mwenyekiti wa  Nsimbo  Amcos  Credo  Kasokola  ni kweli  kwenye  baadhi ya Amcos  wamekuwa sio waaminifu  na wamekuwa wakisababisha kuwepo kwa madeni wengine ni kwa  makusudi na wengune kwa kutofahamu.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages