TANROADS WAPATA MWAROBAINI WA DARAJA LINALOUNGANISHA KATAVI NA MIKOA YA NYANDA ZA JUU.

Kaimu Meneja wa TANROADS Mkoa wa Katavi Mhadisi Albart Laizer.


Na Walter Mguluchuma, Katavi.

Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Katavi  wamepata  mwarobaini wa kuondoa  changamoto iliyokuwepo  kwa  muda  mrefu wakati wa kipindi cha mvua  kwenye  daraja  la Sitalike  linalounganisha Mkoa wa Rukwa na mikoa mingine ya nyanda za juu kusini.

Kaimu   Meneja wa TANROADS Mkoa wa  Katavi  Mhandisi  Albart Laizer  hivi karibu amesema   Wizara ya Ujenzi  imetowa  kiasi cha shilingi  Bilioni 9.3 kwa ajili ya  ujenzi wa   daraja  la Sitalike   lenye  urefu wa mitaa 55 linalouganisha  Mkoa wa Katavi na Mkoa wa Rukwa ambalo lilikuwa na changamoto kwa muda mrefu wakati wa kipindi cha masika.

Amebainisha kuwa ujenzi wa baraja hilo umeisha anza  na unatekelezwa    na  kampuni  ya  kizawa ya Mselemu ya Mkoani  Rukwa kwa fedha za  Benki ya Dunia ambapo ikumbukwe kuwa   baada ya  mvua za  mwaka jana   daraja linalotumika kwa sasa lilisimama  kwa   kipindi cha mwezi  mmoja na  hali ambayo iliwalazimu watumiaji wa barabara inayopita  katikati ya Hifadhi ya Katavi watumie barabara ya Kibaoni-Sitalike.

Ujenzi wa Daraja la Sitalike ambalo linauganisha Mkoa wa Katavi na Rukwa ambalo litakuwa msaada mkubwa wa kuuganisha mawasiliano ya mikoa hiyo miwili.

Mhandisi  Laizer   amefafanua kuwa ukamilikaji wa  daraja  hili ambalo limeanza kujengwa usiku na mchana kutafanya  magari na abiria kupita kwa kipindi cha mwaka mzima tofauti na hapo awali  unatekelezwa  kwa kipindi cha miezi 15 na utakamilika  mwezi Novemba  mwaka huu kwa mujibu wa  mkataba  chini ya usimamizi  mshauri TANROADS   Mkoa wa Katavi .

Ameeleza  kuwa faida kubwa ya mradi huo wa daraja   utaondoa kabisa changamoto   iliyokuwa inaendelea hasa nyakati za masika  kwa maana daraja lililopo kwa sasa ni dogo  na kufanya lifelike wakati wa kipindi cha masika   hasa kwenye kipindi cha miezi ya Januari  hadi Aprili  sasa baada ya kukamilika kwa daraja hili litakuwa linapitika kipindi chote   itakuwa ni sululisho la kudumu.

Mbali ya  Daraja  hili  wanajenga pia  madaraja  mengine  ambayo ni  daraja la Milumba  lenye  urefu wa mita 60   linalogharimu kiasi cha fedha kiasi cha shilingi Bilioni  6.3 muda wa utekelezaji ukiwa ni miezi 15.

Daraja la tatu  ni la Kilida  ambalo wakati wa mvua lilikuwa lilikata  mawasiliano kati ya wananchi wa bonde la Rukwa na  Mpimbwe ambapo ujenzi wake utaghalimu shilingi  Bilioni  1.78 nalo linajengwa  kwa fedha za Benki ya Dunia.

Hili ni daraja la Sitalike ambalo hapo awali lilikuwa linatumiwa na wananchi wa mikoa miwili ya Katavi na Rukwa.

Mkazi wa kata ya Sitalike wilaya ya Mpanda, Salum Sanga amemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuwapelekea ujenzi wa daraja ambalo ni daraja muhimu linalounganisha mikoa miwili ya Katavi na Rukwa kwani kutaondoa ajali nyingi ambazo zilikuwa zinatokea.

Bahati Bitus amesema kwa kumbuku kumbu zake kuna ajali tatu ziliwahi kutokea siku za nyuma ikiwemo iliyohusisha bus moja la Kampuni ys Sumry lilopata ajali na watu zaidi ya kumi walipoteza maisha.

Aidha ameshukuru hatua nzuri zilizochukuliwa na serikali ya kuanza ujenzi wa daraja  hilo jipya linalojegwa kwani wanaimani litakuwa mkombozi kwao kwa kupunguza au kumaliza kabisa tatizo la ajali katika eneo hilo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages