RC AWAWEZESHA USAFIRI WAANDISHI WA HABARI KATAVI


Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwamamvua Mrimdoko [Kulia] akimkabidhi ufunguo wa Pikiki Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa Habari Mkoa wa Katavi Walter Mguluchuma.

Na Paul Mathias-Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amekabidhi Pikipiki moja kwa klabu ya waandishi wa Habari Mkoa wa Katavi kwa lengo la kusaidia kuifikia jamii kwa urahisi katika utekelezaji wa majukumu ya kihabari.

Walter Mguluchuma Mweyekiti wa Klabu ya waandishi wa Habari[kushoto]akitoa shukrani kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko baada ya kukabidhi Pikipiki hiyo kwa waandishi wa Habari.


Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amekabidhi Pikipiki moja kwa klabu ya waandishi wa Habari Mkoa wa Katavi kwa lengo la kusaidia kuifikia jamii kwa urahisi katika utekelezaji wa majukumu ya kihabari.

Akikabidhi Pikipiki hiyo kwa viongozi wa Klabu ya waandishi wa Habari Mkoa wa Katavi,Mkuu huyo wa mkoa amesema lengo la kutoa chombo hicho cha usafiri ni kuwafikia wanananchi wa maeneo mbali katika majukumu ya kihabari na katika kutatua changamoto zao pamoja na kuziona kazi mbalimbali zinazofanywa na serikali kwa wananchi.

‘’Nakukabidhi rasmi pikipiki hii ili kurahisisha kazi za kihabari na kuwafikia wananchi maeneo ambayo wananchi ambao hawawezi kuwafikia waandishi wa habari kwa uharaka’’Mrindoko.

Ameeleza kuwa kupitia pikipiki hiyo itasaidia kupata mrejesho wa kazi zinazofanywa na serikali ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kupitia habari pindi watakapo fikiwa na waandishi wa habari katika maeneo yao.

Mrindoko amewaomba waandishi wa habari kuendelea kuonyesha ushirikiano na serikali na wadau mbalimbali  kama ambavyo wamekuwa wakionyesha kupitia kazi mbalimbali za kihabari kwa wananachi na jamii nzima kwa ujumla.

 
Katika hatua nyingine amewakumbusha waandishi wa Habari wa Mkoa wa Katavi kufanya kazi zao kwa weledi kwa kuzingatia kanuni na taratibu kwenye majukumu ya kuhabarisha umma.

‘’Niwaombe kuzingatia sheria kanuni na maadili katika utendaji wenu wa kazi kwa mkoa wetu wa katavi sina wasiwasi mnafanya kazi zenu vizuri tunawashukuru kwa namna mnavyo utangaza mkoa wetu wa Katavi’’Mrindoko.

Walter Mguluchuma Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Katavi  amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua mrindoko kwa kuona umuhimu wa kuwapatia usafiri huo waandishi wa habari kwakuwa utasaidia kuwafikia wananchi kwa usalama na kwaharaka zaidi.

Mguluchuma amesema kuwa waandishi wa Mkoa wa Katavi wataendelea kufanya kazi na serikali ya mkoa wa Katavi na serikali kwa ujumla.

Amesema kuwa uongozi wa Klabu za waandishi wa habari Tanzania [UTPC] kupitia kwa Mkurugenzi wa UTPC Taifa Keneth Simbaya amemshuru Mkuu wa Mkoa wa Katavi kwa kuonesha mfano hai kwa kutambua mchango wa waandishi wa habari wa Mkoa wa Katavi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages